HABIBA ZARALI, PEMBA
TANI 3,101 za
karafuu kavu zenye thamani ya shilingi bilioni 43.4 kutoka kwa wakulima wa Unguja
na Pemba, zimeshanunuliwa na Shirika la Biashara la Taifa ZSTC tokea kuanza kwa
msimu mwezi Julai mwaka huu.
Katika kisiwa cha
Pemba pekee, Shirika hilo limeshanunuwa tani 3,072 zenye thamani ya shilingi
bilioni 43, na kisiwa cha Unguja limenunuwa tani 28.2 zenye thamani ya shilingi
milioni 400.
Akizugumza katika
ziara yake ya ukaguzi wa ununuzi wa zao la karafuu Mkoani kisiwani Pemba,
Mkurugenzi Muendeshaji wa shirika hilo Said Seif Mzee, alisema shirika la hilo,
bado lina uwezo wa kununuwa karafuu ambazo zitapelekwa kuuzwa.
Alisema ZSTC ipo kwa
ajili ya wananchi, hivyo ni vyema wakaitumia kuuzia zao hilo, ili kufanikisha
malengo yaliyokusudiwa.
“Wananchi wasiwe na wasiwasi
kuhusu shirika hili, waendelee kuleta karafuu zao na kuziuza bila ya hofu, na
zitanunuliwa zote”,alisema.
Mkurugenzi huyo
alifahamisha kuwa, wakati wa kuzipeleka karafuu zao kwa ajili ya kuziuza,
wahakikishe zimekauka vizuri na wameziondowa uchafu, zikiwemo takataka, ili
ziweze kununuliwa kwa sifa na kuondokana na hasara isiyo ya lazima.
Akizungumzia kuhusu
elimu iliyotolewa kwa ajili ya wakulima wa zao hilo, imefahamika kutokana na
wananchi waliowengi huzipeleka karafuu zikiwa katika hali nzuri.
“Karafuu zinapoletwa ZSTC
zikiwa kavu na safi, zinarahisisha kazi kwa Shirika na kwa muuzaji pia kwani
hakumbani na tatizo lolote ikiwemo la kurejeshwa kuanikwa na kuzidondowa takaka
mara mbili.
Wakati huohuo, aliwashauri wananchi kuacha
tabia ya kuzichuma karafuu zikiwa changa kwani zinakuwa nyepesi na hupelekea
kukosa faida kwa mkulima.
Kwa upande wake
mkulima wa zao hilo kutoka kangani Ali
Nassor Khamis, alilishauri Shirika hilo,
kuwaongezea mezani ya kupimia katika kituo kilichopo Mkoani, kwani hulazimika
kukaa foleni kubwa hasa katika siku ya Jumatatu na Ijumaa kwa vile watu wengi
wanakwenda kuuza karafuu zao.
“Pamoja na kuweko kwa
vituo katika vijiji vyetu lakini mzigo ukiwa mwingi ndo tunaona tuje huku
kuondokana na usumbufu wa kupima kidogo kidogo,alisema.
Nae mkulima Jide Said Rashid kutoka Tironi
Mkoani alisema changamoto inayowakabili katika kufikisha zao hilo ZSTC ni
kutokuwa na usafiri katika kijiji chao, jambo ambalo linawapa ugumu wanapotaka
kuuza zao lao.
“Sisi katika kijiji chetu cha Tironi, hatuna
usafiri wa kuzileta karafuu zetu ZSCT kwani tuna ubovu wa barabara na karafuu
ziko nyingi hufika pahala tukashindwa hatuna la kufanya”,alisema.
Alifahamisha hadi sasa mezani ya kupimia ni
nzuri na haina tatizo lolote na kuwashauri wakulima wenzake,
wazipeleke karafuu zao katika shirika hilo kwa ajili ya mauzo.
Mdhamini wa shirika hilo Pemba Abdalla Ali Ussi
alitowa maelekezo kwa wakulima ambao wako vjiji vya ndani ambako ni vigumu
kupata usafiri wa kuzipeleka karafuu zao ZSTC wajikusanye pamoja na kutowa
taarifa kwa kwa ajili kupewa usafiri.
“Lakini ni vyema wakajikusanya kwa pamoja ili
tukizichukuwa zikawa nyingi tusije tukawapelekea usafiri ikawa ni hasara baada
ya faida”alifahamisha.
Hivyo
aliwashukuru wakulima wanaoendelea kupeleka karafuu zao katika shirika hilo, na
kuwataka wengine kufanya hivyo, ili kuweza kuunga mkono na kutimiza lengo
lililokusudiwa
No comments:
Post a Comment