Na/HASINA KHAMIS--- PEMBA.
KAMATI ya udhibiti na usimamizi wa ujenzi (DCU)
imezinduliwa rasmi katika Mkoa wa Kusini
Pemba, kwa lengo la kudhibiti ujenzi wa
kiholela pamoja na kuweza kulinda usalama wa majengo na kuboresha mji kuwa
wenye kivutio.
Kamati
hiyo ilizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mwanajuma Majid Abdalla ,katika ukumbi wa Ofisi
ya Mkuu wa Mkoa huyo Chake Chake Pemba.
Alisema
hali ya mazingira Katika Mkoa wa Kusini Pemba ni Milima, hivyo baadhi ya Wananchi kukata milima ovyo na kusababisha
mafuriko pamoja na maporomoko kwenye Milima.
“Zamani
Pemba ni nadra kusikia milima kuporomoka au mafuriko lakini sasa baada ya
kujenga bila kufuata sheria kumesababisha maafa, hivyo ninafarijika kwa kamati
hii ya DCU kuzinduliwa na imani yangu itaweza kudhibiti hali hiyo “, alieleza.
Mkuu
huyo wa Mkoa, alisema kumekuwa na tabia ya kujenga Wananchi kwa kutafuta kibali
kwa Sheha ,Diwani na baada ya kupata huanza kujenga bila ya kufata taratibu
nyengine za Baraza la mji .
Hivyo
kusababisha maeneo ya kilimo kuweza kujengwa Nyumba za kuishi na kusababisha
usumbufu kwa Serikali na Mabaraza ya mji.
Mwanajuma,
aliahidi kushirikiana na kamati hiyo kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa
na Serikali ili kuona maendeleo ya Mji yanaonekana.
Mwenyekiti
wa kamati hiyo, Dkt, Muhammed Juma, alisema hali ya ujenzi kwa Zanzibar,
imekuwa kwa kasi hivyo ni vyema kufuata taratibu zilizowekwa na DCU pamoja na
kukata kibali cha ujenzi ili kuweza kuondoa usumbufu baada ya kujenga .
Alisema”kamati
ya DCU, ina malengo ya kuweka miji ya Zanzibar na majengo yake kuwa imara na
usalama wa hali ya juu, mazingira ya
kuvutia baadae, hivyo ni vyema kwa wananchi kufuata taratibu kwenye ujenzi”.
Mwenyekiti
huyo, alisema ipo haja kwa Masheha na Madiwani kupewa elimu juu ya utoaji wa
kibali kwani jamii inaona ikipata kibali kwa watu huo kuwa inatosha kwa kujenga
bila ya kutaarifu Serikali za Mji.
Mipango
Miji, imekuwa na nafasi kubwa ya kupambana na miji ili kuweza kuweka katika
hali ya kuvutia na kuondoa migogoro ya ardhi kwa wananchi.
Muhammed
Faki Machano, Mjumbe wa Sekreteriti ya Kamati alisema ni lazima kuondoa muhali
pale panaposemwa kuwa sehemu haifai kujengwa kwani DCU inafata Sheria ya
mipango miji na ipo kitaifa.
Hata
hivyo alisema Serikali kuu na Serikali za mitaa zitafanya kazi pamoja kujenga Miji
za Zanzibar pamoja na kupeana elimu na kutatua migogoro itakayo tokea ,ikiwa
ni pamoja na mapato yatakayo kusanywa na kamati hiyo kulenga zaidi miradi ya Mabaraza
na kubuni miradi ya maendeleo ya miji ambayo itaweza kuonekana moja kwa moja na
Wananchi.
No comments:
Post a Comment