Na mwandishi wetu.
MWEZI Julai mwaka
huu, Makamu wa pili wa rasi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, alifanya uzinduzi
wa uchumaji wa zao la karafuu, kwenye kijiji cha Changaweni wilaya ya Mkoani,
kisiwani Pemba.
Ni
eneo lenye idadi kubwa ya mikarafuu, ambapo mwambao huo, unaelekea Tironi, Manyaga,
Fumbani na ukiamua kukosa sana hadi mabonde ya Wambaa kama sio Makombeni.
Kwa
ujumla Mkoa wa kusini Pemba, uanounda wilaya za Chakechake na Mkoani, ndio
wenye idadi kubwa ya Mikarafuu, kuliko wilaya za Micheweni na Wete, zilizoko
Mkoa wa kaskazini Pemba.
Zoezi
la uchumaji wa zao hilo, bila shaka kuliashiria pia ukodishwaji wa mashamba
yale ya serikali, umaarufu eka tatu tatu, ambazo ukweli ni urithi wa akili ya
rais wa kwanza wa Zanzibar, sheikh Abeid Amani Karume.
Eka
tatu ni mashamba maalumu yaliokatiwa wananchi wa nchi hii, tokea uhai wake,
ambapo wamiliki wa mwanzo wanapofariki, hutakiwa wale wanaotaka kuyaendeleza
wayaombe serikalini.
Wapo
waliofanya hivyo kwa karne, maana walikuwa wanajua, na wengine wapo
waliojichukulia, aidha kwa ujanja ujanja au kwa kujua kuwa, wanalinda na
kuienzi mali ya serikali.
Miaka
nenda miaka mirudi, serikali hii ya Mapuinduzi ya Zanzibara ya awamu ya saba,
inayoongozwa na rais wake mahiri Mhe: dk Ali Mohamed Shein ikionyeshwa kuchoka
kuibiwa.
Ndio
maana sasa, ndani ya msimu huu au kabla ya kuanza, ikadhamiria kwa nia safi
kabisa, kuyasaka, kuyatafuta, kuyazinga, kuyarudisha mashamba yote ya serikali
na hasa ambao hata waliomilikishwa wameshafariki.
Hapo
zoezi la pata shika nguo chanika kisha shoneka, ikaanza kwa Wizara ya Kilimo,
Maliasili, Mifugo na Uvuvi, kuwa kinara wa zoezi la ukosdishaji na utambuzi.
Matamu ya ukodishaji
Kamati
ya ukodishwaji ikaundwa chini ya Mwenyekiti wake Haji Mussa Haji, ambae ni
mtendaji ndani ya wizara ya Kilimo, ili kuhakikisha wanapita wilya zote nne
kufanya kazi ya ukodishaji.
Kazi
ya kuingia msitu hadi msitu, mabonde na milima ikaendelea kwa kuchupa mito,
mizizi, kupita vichaka kadhaa vya wilaya zote nne, ili kuhakikisha zoezi
linakamilika tena kwa mafanikio.
Kumbe
serikali inayoa mashamba kadhaa, ambayo yalikuwa mikononi mwa wachache, wakila,
wakinywa, wakivaa na kujitibia kwa mali ya umma.
Maana
kamati hiyo ya ukodishwaji na wizara kwa ujumla, ilidhamiria kuhakikisha
inayaibua mashamba walau 1,525 kisiwani Pemba pekee.
Na
hapo iliona kwa wastani kama yakipatikana na mashamba hayo, na yakikodishwa
kisha waliokoadi kuamua kulipa fedha kama ilivyo kwenye mikataba ya zoezi hilol
basi serikali hii, ingejipatia shilingi zaidi ya bilioni 2.393.
Lakini
kutokana na kazi nzuri, iliofanywa na Kamati ya ukodishwaji mshamba ya
serikali, ikiambatana na wakuu wa mikoa na wilaya, basi haikufanya vibaya sana,
maana waliyapata mashamba 1,451.
Ingawa
hapa fedha ambazo zimeshaingia kwenye accounti ya serikali, kama sio wizara
husika ni wastani wa shilingi milioni 900.661.
Walishasema
wahenga kuwa, mpango sio matumizi wala, mwenye nacho hamjui mkosaji, na ndio
maana inawezekana waliokodishwa wameshachuma, lakini kurejesha wanahitaji mtutu
wa bunduki.
Kumbe
azma ya serikali ya kuyatafuta kwa udi na uvumba mashamba yake, ni kuona sasa
kwa misimu ijayo, wanayatambua mashamba, na kuachana na ule wa mpango wa zamani
eti kuvuna milioni 100 pekee kwa ukodishwaji.
Zuri
ambalo pia limezingatiwa na kamati hii pamoja na mamlaka nyengine za juu, kama
sio sheria husika, ni kuhakikisha mara mnada wa ukodishaji umalizikapo, ni
kumsikiliza anae lilea shamba.
Mwenyekiti
wa kamati hiyo, Haji Mussa Haji, anasema bei yoyote iliofikiwa iwe kubwa au
ndogo, lazima wa kwanza kuulizwa iwapo ana mudu kulikodai shamba ni anaelilea.
Kwa
mfano shamba limefikia shilingi milioni 18, basi anaelishughulikia ndio huulizwa
iwapo anazo fedha hizo na yuko tayari kulikodi.
Zuri
ambalo limo kwenye mikataba ya ukodishaji, ni kuwepo kwa fedha, za
anaelishughulikia umaarufu ‘kifuta jasho’ ambacho ni asilimia 40 ya bei
iliofikiwa.
Kwa
mafano shamba limekodishwa kwa bei ya shilingi milioni moja, basi
anaelishughulikia hata kama amelikodi yeye, atajikusanyia shilingi 400,000.
Nakumbuka
hadi leo hii, kwenye zoezi la uzinduzi wa ukodishwajia wilaya ya Chakechake,
mtendaji wa wizara ya kilimo aliemwakilisha Afisa Mdhamini Kilimo, bwana Said Juma
Ali, alitamka mengi mazuri.
Moja kwamba, mara baada ya bei kufikiwa, ya
mtu aliekodi shamba la serikali, hutakiwa kulipa asilimia 25 ndani ya siku
mbili na kumaliza asilimia 75 ndani ya wiki mbili kama mkataba unavyotaka.
Tena
kabla ya kuanza kwa zoezi hilo, kwanza masharti ya mkataba huo, ulikuwa
ukisomwa hadharani, kusudi kila mmoja, asikie yaliomo na kuangalia uwezo wake.
Maana
wazee wa zamani walishatuwachia usemi kuwa, kila mwenda mbio hushauri nyonga
yake, ni sawa na yule mbeba mzigo mzito hungalia nguvu zake.
Kubwa
zaidi ambalo linakuja kuwa ni tamu pindi wale wanaodaiwa shilingi bilion 1.492
wakizilipa na kuingia serikali, ambapo itachapuzi maendeleo ya taifa letu.
Wizara
ya Kilimo, ilifanikiwa kuyakodi kimakosa mashamba zaidi ya 75, kisiwani Pemba
lakini baada ya wenyewe kuzuka na vielelezo husika, ililazimika kuyarejesha kwa
wamiliki halali.
“Zozi
hili halipo kwa ajili ya kuwachukulia wananchi haki zao, bali ni kuhakikisha mali
ya serikali inarudini mikononi mwa serikali na sio kuliwa na wachache”,alisema
Afisa Mdhamini Kilimo Sihaba Haji Vuai.
Mchungu ya ukodishaji.
Walishasema
waliotangulia kuwa, hakuna jambo lenye faida likakosa na hasara na hasa kwa
yale yote yalioasisiwa au kutengenezwa na binadamu.
Maana
moja ya donda ambalo limejitokeza kwenye zoezi hili la ukodishaji wa mashamba
ya mikarafuu ya eka tatu tatu ni kuzuka kwa malalamiko kwa wale waliokuwa
wakiyalea.
Kombo
Abdalla Kombo akiwakilisha wenzake, alilia sana baada ya kupewa taarifa kuwa,
shamba analolishughulikia linataka kukodishwa.
Shamba
hili lililopo mabonde ya Chonga wilaya ya Chakechake, anasema alichokifikiria
kwa vile wizara husika, iliyatekeleza kwa zaidi ya miaka 20 mashamba hayo,
wengesubiri msimu huu ukamalizika, ndio wakayatafuta.
Akili
yake inampelekea kuhoji iweje zaidi ya miaka 20 analilee shamba hilo, bila ya
kuulizwa hadi hapo msimu huu ulionawiri, ndio leo hii aelezwe kuwa linatakiwa.
Uchungu
aliokuwa nao zaidi, ni baada ya kupigwa mnada na kufikia shilingi milini 18,
kwa kuwepo watu aliowaita madalali, wakipandisha bei ili limshinde.
“Mimi
hili shamba nimeshapanda mikarafuu 100 mipya, na mikongwe iliomo haizidi 80, na
mazao wa mwaka huu wala haukuwa mkubwa, sasa leo linakodishwa kwa mnada wa
hadhara bei hiyo, hee”,aliguna.
Abdalla
kama walivyowenzake, yeye aliona ushauri wake ni mashamba ambayo yanalelewa na
watu, basi kwanza yengefanyiwa tathmini na wizara husika, kisha kuulizwa iwapo
wanauwezo ya kuyakodi, na wakishindwa ndio uitishwe mnada wa hadhara.
Chungu
jengine lililoibuka kwenye zoezi hilo, ni kwa wananchi iwe kwa wanaoyalea au
wamiliki halali, kutopata taarifa sahihi ya zoezi hilo, wakidai kuwa lilikuwa
kama la kushitukia.
Taarifa
nyengine mbaya na za kusikitisha, wakati wizara ya kilimo ikionekana kuja juu
kuyasaka mashamba hayo na kuwataka masheha, watoe ushirikiano, hali ni tofauti
maana watendaji wenyewe wa wizara husika wengine sio wasafi.
Kwa
vile ZAECA ilikuwa bega kwa bega kwenye zoezi la ukodishaji na utambuzi wa
mashamba ya serikali, yenyewe iliyafichua mashamba 30, ambayo yanadaiwa
kufichwa na watendaji wa serikali hii.
Maana
Mdhamini wa ZAEC Pemba, Suleiman Ame Juma, anasema, mashamba hayo yamo ndani
yake yaliofichwa na masheha, watendaji wa wizara ya kilimo au wananchi
wanaoelewa zaidi.
“Hivi
sasa tunamshikilia mtendaji wa wizara ya kilimo Pemba, ambae alitengeneza
kizuka bandis ili shamba moja lililopo Mizingani wilaya ya Mkoani libakie
mikononi mwake”,anasema.
Mdhamini
akaenda mbali zaidi kuwa, baada ya maofisa wake kufanya kazi walioajiriwa,
walimgundua Hassan Hija Maduhushi, kutengeneza kizuka na kumpa ushauri wa siri
kwa lengo la shamba hilo, kuwa mikononi mwake.
Baada
ya kumuhoji mtendaji huyo wa wizara ya Kilimo, ZAECA iligundua kuwa, shamba
hilo, mtendaji huyo lilikuwa la babayake kabla ya kufikwa na umauti, na
kushindwa kulirejesha serikali.
Hapa
unagundua kuwa kama mtendaji wa serikali kupitia wizara ya kilimo,
analishikilia shamba la serikali kwa njia hiyo, sasa la kujiuliza wengine
watafanya nini.
Kwa
sasa Maduhushi yuko mikononi mwa ZAECA, akisubiri taratibu za kisheria, ili
akumbanae na kifungu cha 37 cha sheria no 1 ya mwaka 2012 ya Kuzuia rushwa na
uhujumu wa uchumi Zanzibar.
Ingawa
ZAECA inamshikilia mtendaji huyo, hata wizara yenyewe inakusudia kuwakabidhiwa,
wananchi wanaodaiwa zaidi ya shilingi bilioni 1.492 zinazotokana na ukodishwaji
wa mikarafuu, ambao hawajalipa fedha hizo.
Ni
kauli ilitolewa na Afisa Mdhamini wa wizara hiyo, kisiwani humo Sihaba Haji
Vuai, wakati alipokuwa akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, juu ya mwenendo wa
ukodishaji na namna ya wananchi waliokodi walivyolipa fedha hizo.
Yeye
alisema tayari mashamba 1,451 yameshakodishwa kwa wananchi mbali mbali kisiwani
Pemba, ambapo kama ingekuwa wameshalipa, serikali ingepata zaidi ya shilingi bilioni
2.393, ingawa hadi sasa, ni zaidi ya shilingi milioni 900.661 zilizokwishalipwa
.
Sasa
baada ya kuona, hili linaelekea ndivyo sivyo, hatua inayofuata wakaona, ni
kuwakabidhi kwa ZEACA, ili hatua za kisheria sasa zichukuliwe dhidi yao.
Lakini
ZAECA, imesema inaendelea kuyatafuta mashamba mengine, iwapo yamefichwa au laa,
na wakibaini hilo na wanaamini watayapata, basi ni kuwafungulia mashiataka
wahusika.
Ingawa ZAECA wanasema suala la kukodishana
mitu na kuwepo kwa mkataba, ni suala la madai hivyo, na wao wanashughulikia
zaidi jinai, ingawa wanavipitia vifungu kuona wanawashika.
No comments:
Post a Comment