STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 17.11.2017
RAIS wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za
pongezi Sultan wa Oman,Sultan Qaboos Bin Said Al Said pamoja na wananchi wa
nchi hiyo kwa kuadhimisha Siku ya Taifa hilo.
Salamu hizo zilieleza kuwa wananchi wa Zanzibar
wanaungana na ndugu zao wa Oman katika kusherehekea siku hii adhimu kwa Taifa
hilo.
Aidha, katika salamu hizo, Dk. Shein
alimuhakikishia Sultan Qaboos Bin Said Al Said kuwa Zanzibar itaendeleza
uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo kati yake na Oman sambamba na
kuimarisha udugu uliopo kati ya wananchi wa Oman na wananchi wa Zanzibar.
Sambamba na hayo, salamu hizo zilieleza kuwa siku
hii adhimu inaendelea kutoa nafasi zaidi ya mashirikiano kati ya pande mbili
hizo pamoja na kupongeza juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Oman katika
kuiunga mkono Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha sekta mbali
mbali za maendeleo.
Dk. Shein alimtakia kiongozi huyo pamoja na
familia yake na wananchi wote wa Oman afya njema na sherehe njema katika
kuadhimisha siku hiyo huku akimtakia kiongozi huyo mafanikio zaidi katika
kuendelea kuipatia maendeleo zaidi ya kiuchumi nchi hiyo kwa madhumuni ya
kulinufaisha Taifa hilo pamoja na wananchi wake.
Oman ilipata uhuru wake kutoka ukoloni wa Kireno
mnamo Novemba 18 mwaka 1650 chini ya kiongozi na muasisi wa Taifa hilo Imam
Sultan Bin Saif Bin Malik Al Yarubi ambaye alisimamia kung’oka kwa koloni hilo
kutoka nchini Oman pamoja na bandari zote za nchi hiyo zilizokuwa chini ya
Ureno.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment