Na.Haji. Nassor - Pemba.
Tume ya Ukimwi Zanzibar ZAC, ofisi ya
Pemba imesema kazi kubwa wanayoifanya ya kuihamasisha jamii ili kudhibiti
maambukizi mapya ya VUU na unyanyapaa kwa watu wanaoishi na Ukimwi,
haitofanikiwa iwapo watu hawatobadili tabia zao.
Tume hiyo,
imesema inaamini jamii ya wazanzibar kwa asilimia 99, wameshafikiwa na elimu ya
Ukimwi kwa kupitia njia mbali mbali, na sasa kazi iliopo mbele yao na watu hao
kubadili tabia, ili kufikia malengo ya kutokuwa na mgonjwa wowote mpya mwenye
VVU.
Kauli hiyo
imetolewa na Mratbu wa Tume hiyo, kisiwani Pemba, Nassor Ali Abdalla, wakati
alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mjini Chakechake kuelekea
maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani.
Alisema kazi
ya mtu kubadili tabia ni yake binafsi, na wao kama Tume, hiyo ndio mipaka yao,
hivyo kilichobaki ni kuwabembeleza, ili wabadili tabia ya kufikia malengo ya
Tume na ya jamii kwa ujumla.
Alisema
ingawa takwimu za maambukizi ya VVU yameshuka hasa kwa kisiwani Pemba, kutoka
kila watu 1000 kuwa sita (6) wana VVU hadi kufikia idadi kama hiyo, kwa watu
watatu (3), lakini hilo isiwe sababu kuacha kubadili tabia.
Alieleza
kuwa, Tume ya Ukimwi kazi yake kubwa ni kupanga mikakati, kutoa mbinu,
kuelimisha na kuhakikisha inayafikia makundi yote ndani ya jamii, kisha watu
wenyewe ndio wafuate miongozo yao.
“Hivi sasa,
sisi ndani ya Tume tunajivunia kuwa, kazi tulioifanya kwa kushirikiana na wadau
wetu kama vijana, viongozi wa dini vyombo vya habari, viongozi wa serikali na
sekta binafsi, imezaa matunda, lakini jamii ibadili tabia ili tufikie malengo” ,alieleza.
Katika hatua
nyengine Mratibu huyo wa Tume ya Ukimwi Zanzibar ofisi ya Pemba, Nassor Ali
Abdalla, alisema bao Ukimwi upo na kuwatahadharisha wananchi kuwa, wilaya ya
Chakechake inaendelea kuwa tishio.
Alisema
hilo, linatokana na tafiti mbali mbali zilizofanywa na, kuonyesha maambukizi
bado yako juu, hasa kutokana na mchanganyiko mkubwa wa wageni uliopo.
“Sehemu kuu
za starehe kwa Pemba ziko wilaya ya Chakechake, wageni wote wanaanzia
Chakechake, nyumba za kulala wageni na hoteli nzao zinapatikana hapa, ambapo
hivyo na vyengine vinachangia kuibuka kwa watu wapya wenye VVU”,alibainisha.
Hata hivyo,
alisema wanakusudia hadi ifikapo mwaka 2020, iwe tayari kila wazanzibar 1000, basi
99 wawe wameshapima na kujua afya zao.
Kuhusu
matayarisho ya kuadhimisha siku ya Ukimwi duniani, alisema wao kwa Zanzibar
watatangulia kwa siku moja kabla ya Disemba mosi, kutokana na siku yenyewe kuwa
ni ndogo kiimani.
Hata hivyo,
alisema kwenye maadhimisho hayo, pamoja na hutuba ya mgeni rasmi, watu
wanaoishi na VVU watakuwa na maonyesho ya biashara zao mbali mbali, watatoa
ushuhuda pamoja na shamra shamra nyengine.
Omar Hassan
Abeid, wa Chakechake alisema, elimu ya Ukimwi bado inahitajika ndani ya jamii,
hasa kutokana na dira ya ZAC ya kutaka kuondoa wagonjwa wapya wa VVU.
Othaman
Yahya Iddi, anaesihi na VVU mwaka wa nne sasa, alisema mpango wa ZAC wa
kutegemea wafadhili hata kupita kwenye mabaa na migahawa kutoa elimu, basi
wasitarajie kuwa kuna siku hakutakuwa na wagonjwa wapya.
Kwa upande
wake, Khadija Ali Waziri wa Madungu, alisema suala la kubadili tabia, ni vyema
viongozi wa dini wakawaelimsha wafuasi wao, kila wanapokutana kwenye nyumba zao
za ibada.
Tokea
kugundulika kwa mgonjwa wa kwanza Zanzibar mwenye VVU mwaka 1986, kisiwani
Pemba wapo wananchi wastani wa 1,200 wanaoishi na virusi vya Ukiwmi, ambapi kati
ya hao zaidi ya 300, wamekubali kujitangaaza na kujiunga kwenye Jumuia ya watu
wanaoshi na VVU.
No comments:
Post a Comment