Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Ndugu Rodgers William Sianga wakati akiwasili kwenye kilele cha maadhimisho ya siku Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa kwenye Viwanja vya kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Bahame Tom Nyanduga (kulia) alipotembelea banda lao wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa kwenye Viwanja vya kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere mjini Dodoma
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Bahame Tom Nyanduga (kulia) alipotembelea banda lao wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa kwenye Viwanja vya kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere mjini Dodoma
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa kwenye Viwanja vya kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere mjini Dodoma.
Sehemu ya wahudhuriaji wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere mjini Dodoma(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
`Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameziagiza Taasisi zote zenye usimamizi kuhakikisha
zinasimamia vyema jukumu lao la kutumia nafasi zao kuongeza juhudi katika
kuimarisha misingi ya Utawala Bora, Uwazi, Uadilifu na Uwajibikaji.
Makamu wa Rais aliyasema hayo leo wakati wa
Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa
yaliofanyika kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere mjini Dodoma.
Makamu wa Rais alisema Vita dhidi ya
ukiukwaji wa Maadili haiwezi kupiganwa na Serikali peke yake, “Ni jukumu la
kila mwananchi kuhakikisha kuwa vitendo vya rushwa, ubadhirifu na maovu mengine
vinatokomezwa”
Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kuweka
mikakati madhubuti ya kisera na kisheria ambayo itahakikisha vijana wanakuzwa
kimaadili kwani hakuna Taifa Duniani linaweza kupata maendeleo bila kuwa na
utamaduni unaozingatia maadili alisema Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais alisisitiza kuwa ili kujenga
Utawala Bora ni lazima kuweka uwiano wa
yanayofanyika na serikali kuu hadi serikali ya mitaa nchi nzima.Serikali
ilizindua Rasmi mkakati wa Taifa Dhidi
ya Rushwa na Mpango wa Utekelezaji Awamu
ya Tatu (NACSAP III) Desemba 2016.
Makamu wa Rais alisema kutokana na
kutoridhishwa na utendaji wa baadhi ya Ofisi za Serikali, Serikali imeamua
kufuatilia uhalali wa vyeti vya Watumishi, Idadi halali ya Watumishi wa Umma na
ulipaji wa Mishahara Hewa na kusisitiza zoezi ili litakuwa endelevu.
Mwisho, Makamu wa Rais aliwaeleza wananchi
na Watumishi wa Umma kwa ujumla kuwa Maadili ni nguzo muhimu katika maendeleo
ya nchi yetu. “Ni imani yangu kuwa Wakuu wa Taasisi hizi kuwa mtahakikisha misingi ya
haki za binadamu, utawala bora na viwango vya Maadili ya Viongozi wa Umma
vinasimamiwa ipasavyo ili kuimarisha nidhamu ya Maafisa na Watumishi wa Umma”.
Kuimarishwa na kudumishwa kwa nidhamu ya
utendaji, huduma zitolewazo Serikalini, Ukusanyaji wa mapato na matumizi bora
ya fedha za Serikali kutaleta mafanikio katika kuelekea uchumi wa kati.
No comments:
Post a Comment