Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Vifaa vya kufanyia Usafi Katibu wa Baraza la Vijana wa Wilaya ya Magharibi B Unguja Farida Juma,wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika eneo la Nyumba za Wazee Sebleni Unguja.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amesema kuwa hakuna mbadala wa usafi hivyo wananchi wote
wanapaswa kuwa wasafi wao wenyewe pamoja na mazingira wanayoishi.
Dk. Shein aliyasema
hayo leo mara baada ya kushiriki kikamilifu katika uzinduzi wa usafi wa
mazingira uliofanyika katika nyumba za wazee Sebleni mjini Zanzibar ikiwa ni
mwanzo wa shamrashamra za miaka 54 ya Mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964.
Dk. Shein alisema kuwa
usafi ukikosekana kuna kila sababu za mwanaadamu ama jamii kupata maradhi na hatimae
kupelekea kuathirika na kupata matatizo ya afya ikiwemo kupata maradi ya
kipindupindu.
Katika suala zima la
usafi, Dk. Shein alisisitiza kuwa mwanaadamu ni usafi hasa katika usafi wa
mazingira, sehemu anazoishi, anazokula, kunywa na kuvaa na ndio maana dini zote
zinasisitiza suala zima la usafi.
Dk. Shein alieleza haja
ya kuendelea kufanya usafi na kusisitiza kuwa usafi huo uwe endelevu na usiwe
kwa leo pekee na kwa kila mmoja afanye juhudi katika suala zima la usafi na
yule ambaye hawezi kufanya usafi wakiwemo wazee wasaidiwe ili waendelee kuishi
maisha bora.
Alisisitiza haja ya
wananchi kuungana na Serikali yao ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwaenzi na
kuwatunza wazee.
Aidha, Dk. Shein
alipongeza juhudi za Mkoa wa Mjini Magharibi za kuwapa ajira vijana 3630 ambao
watapata nafasi ya kujiongezea kipato chao kupitia fedha zitakazokusanywa kwa
huduma za uzoaji taka kutoka nyumba za wananchi na maeneo ya biashara.
Alieleza kufurahishwa
na Mpango Mkakati wa kuimarisha usafi na
kupelekea Mkoa wa Mjini Magharibi kuwa safi huku akitilia mkazo kwa wale wote
watakaokwenda kinyume na taratibu
zilizowekwa na Mkoa huo ikiwa ni pamoja na adhabu kwa atakaeegesha gari maeneo
ya barabarani.
Dk. Shein aliwataka
viongozi wa Mkoa kuyashughulikia na kuongeza njia na kutaka Mikoa mengine ije
kuiga na kwa vile kila Jumaamosi wameamua kufanya usafi na yeye ametangaza kuwa
ameamua kuwa kila Jumaamosi ya mwisho wa mwezi atakutakana na uongozi wa Mkoa
wake ili aisikie nini wanafanya katika kila mwezi na kutaka miezi sita
wamefanya nini.
Alisikilize
utekelezaji waliofikia katika Mpango huo wa kuimarisha usafi na kuendezesha mji
na kumpataka Mkuu wa Mkoa kusimamia yeye
na wasaidizi wake kwani sheria na kanuni vyote bvipo na kutaka mpango huo
utekelezwe.
Sambamba na hayo, Dk.
Shein aliwataka wananchi kuwayenzi, kuyaendeleza na kuyapa heshima Mapinduzi ya
Januari 12, 1964 kwani ni uhai wa nchi na yameleta Muungano uliopo wa Tanzania
kwani hakuna mbadala wake na lazima wawe imara katika kuyatunza na kuyaendeleza
ili nchi ipate tija.
Alisema kuwa Zanzibar
itajengwa na Wazanzibari wenyewe, na hivi sasa tayari miaka 54 imeshafikiwa
huku Zanzibar ikiwa imepiga hatua kubwa sana kutokana na mabadiliko makubwa
yaliopatikana ya Maedendleo yanayotokana na Mapinduzi.
Dk. Shein alisisitiza
kuwa ni vyema Mapinduzi yatunzwe na yaenziwe na kuendelezwa kwa kuijenga
Zanzibar kwa ari na nguvu kubwa ili maendeleo yazidi kupatikana.
Alimpongeza Mkuu wa
Mkoa kwa zoezi hilo kufanyika katika eneo la Sebleni lenye historia kubwa huku
akieleza maagizo ya Ilani ya ASP yaliotanagzwa na Marehemu Mzee Abeid Amani
Karume ikiwa ni pamoja na afya, elimu sambamba
na kujengwa kwa nyumba za wazee, kwani ilikuwa ni Sera ya ASP
iliyowakomboa wananchi wote wa Unguja na Pemba.
Pamoja na hayo, Dk.
Shein alisisitiza kuwa Serikali ina wajibu wa kuwatendea mema watu wote bila ya
ubaguzi kwani Serikali ni ya wote.
Nae Mkuu wa Mkoa wa
Mjini Magharibi Ayoub Mahmoud alieleza kuwa Mpango uliwekwa na Mkoa wake ni
mashirikiano ya pamoja kati ya viongozi wa Serikali, Mkoa, Majimbo na Shehia za
Mkoa huo.
Nae Katibu Tawala
Hamida Mussa Khamis akisoma taarifa ya uzinduzi wa Mpango wa Kuimarisha Usafi
na Kupendezesha Mji katika Mkoa wa Mjini Magharibi alisema kuwa Mkoa umepanga
kutekeleza Mapngo huo kwa kipindi cha majaribio cha miaka miwili.
Alieleza kuwa lengo ni
kuhakikisha mwishoni mwa mwaka 2019 Mkoa wa Mjini Magharibi uwe msafi na wenye
mvuto na usiwe hatarishi katika kuchangia kuenea kwa maradhi ya mripuko.
Alieleza matamko
yaliyoazimiwa na Mkoa huo ikiwa ni pamoja na kila nyumba italazimika kuchangia
fedha za uzoaji wa taka taka ambazo zitachukuliwa kutoka zilizopo na kupelekwa
katika eneo lililotengwa kukusanyia taka TZS mia moja kila siku ambazo zitakuwa
ni jmla ya TZS elfu 30 kwa mwezi.
Mtu yeyote
atakaebainika kutupa taka ovyo, kutema mate na kujisaidia ovyo atawajibika kwa
kulipa faini kama zilivyoanishwa katika kanuni za uchafuzi wa mazigira.
Kila mwenye nyumba,
ofisi au aneo la bishaara lililopo barabarani analazimika kuweka ‘Interlock’ au
bustani ili kuweka haiba nzuri na kila mfanyabiashara anawajibu wa kuweka
vyombo maalum vya kutupia taka huku Mkoa ukipanga kuwa kila siku ya Jumaamosi
ya kila wiki kuwa ni siku ya usafi kuzia saa 12:00 hadi saa 4:00 asubuhi.
Aliongeza kuwa gari
zote zinazolazwa au kuegeshwa katika maeneo ya barabarani hazitaruhusiwa tena
na kwamba kuanzia sasa gari zote zitachukuliwa na gari maalum za Manispaa
ambapo mhusika atalazimika kulipa fidia ili apewe gari yake.
Hamida aliongeza kuwa
Mkoa wa Mjini Magharibi unaweza kuwa Mji wa mfano endapo wananchi wataunga
mkono jitihada za Serikali za kuimarisha usafi wa mazingira.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment