STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Dubai 24.01.2018
RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amekutana na kufanya
mazungumzo na Mtukufu Sheikh Mohammed bin Rashid Al Makhtoum, Makamo wa Rais na
Waziri Mkuu wa nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Mtawala wa Dubai
ambapo viongozi hao wameahidi kushirikiana katika sekta mbali mbali za
maendeleo zikiwemo za biashara, uwekezaji na utalii.
Viongozi hao walifanya
mazungumzo hayo katika ukumbi wa Makaazi ya Sheikh Mohammed bin Rashid, mjini Dubai,
ikiwa ni muendelezo wa ziara ya Dk. Shein katika nchi za Umoja wa Falme za
Kiarabu (UAE).
Katika maelezo yao
viongozi hao walieleza azma yao ya kuendeleza uhusiano na ushirikiano wa muda
mrefu ambao ni wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania ikiwemo Zanzibar na Dubai.
Dk. Shein alimueleza
kiongozi huyo juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Zanzibar katika kuhakikisha
sekta ya utalii inazidi kuimarika sambamba na ongezeko la watalii hivi sasa
pamoja na malengo yaliyowekwa na Serikali katika kufikia watalii laki tano
mnamo mwaka 2020, malengo ambayo yanaweza kufikiwa kabla ya mwaka huo kutokana
na ongezeko la watalii kila uchao.
Aidha, Dk. Shein
alimueleza kiongozi huyo vivutio kadhaa vya asili vilivyopo Zanzibar vikiwemo
Mji Mkongwe wa kihistoria, fukwe za bahari, viungo, utamaduni na silka za
Wazanzibari, mazingira, ukarimu pamoja na mambo mengineyo bila ya kusahau amani
na utulivu mkubwa uliopo ambao ndio chachu ya kuimarisha sekta ya Utalii
Zanzibar.
Pamoja na hayo, Dk.
Shein alimueleza kiongozi huyo mikakati iliyowekwa katika kuhakikisha sekta
hiyo inaimarika zaidi hasa katika kuendeleza sekta hiyo kwa sayansi na
teknolojia iliyopo jambo ambalo bado linataka kuungwa mkono ili liweze kuleta
tija.
Pia, Dk. Shein
alimueleza kiongozi huyo hatua zinazoendelea kuchukuliwa katika kuimarisha
sekta ya uwekezaji na biashara hasa ikizingatiwa kuwa Zanzibar ina historia
kubwa ya kibiashara kati yake na nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE)
ikiwemo Dubai huku akisisitiza haja kwa Kampuni ya ndege ya “Emirate” kufanya
safari kati ya Dubai na Zanzibar ili kuzidi kuimarisha sekta hizo.
Nae Sheikh Mohammed bin
Rashid Al Makhtoum alimuhakikishiaDk. Shein kuwa atahakikisha juhudi za
makusudi zinachukuliwakatika kuhakikisha uhusiano na ushirikiano wa muda mrefu
ulipo kati ya pande mbili hizo unaimarishwa.
Aidha, kiongozi huyo
alimueleza Rais Dk. Shein kuwa nchi yake inathamini uhusiano na ushirikiano
uliopo na kuahidi kuuendeleza kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar katika kuimarisha sekta zake za maendeleo ikiwemo utalii, uwekezaji
na biashara.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa
Kampuni ya ndege ya Emirate Sheikh Ahmed Bin Saeed Al Makhtoum alimuhakikishia
Rais Dk. Shein kuwa Kampuni ya ndege ya “Fly Dubai” chini itazidi kuonngeza
safari zake kati ya Zanzibar na Dubai.
Wakati huo huo,
Dk. Shein alifanya mazungumzo na Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wawekezaji na
Wenyeviwanda wa Dubai na kuwakaribisha huku akiwataka kuendelea kuekeza
Zanzibar na kueleza kuwa Jumuiya hiyo imeundwa na wanachama wenye uzoefu mkubwa
katika sekta ya biashara, viwanda, utalii na uwekezaji ambapo mchango wao
umeifanya Dubai kupata maendeleo ya haraka ambayo ni mfano duniani kote.
Hivyo, kwa kutunia
uzoefu walionao, Dk. Shein aliwataka wawekezaji hao wa Jumuiya ya
Wafanyabiashara, wawekezaji na wenye viwanda wa Dubai kuchangamkia fursa za
uwekezaji zilizopo Zanzibar katika sekta zote za uwekezaji zilizopo.
Dk. Shein aliwahakikishia
kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kwa jumla zina usalama na amani ya kutosha jambo ambalo limekuwa ni
chachu ya maendeleo yanayoendelea kupatikana hivi sasa.
Aidha, Dk. Shein
aliwaeleza mipango ya Serikali ya kuhakikisha kuwa rasilimali za wawekezaji
zinaleindwa kutokana na kutunga sheria mbali mbali zenye lengo la kuimarisha
uwekezaji pamoja na kulinda rasilimali za wawekezaji.
Baada ya kusema hayo,
Dk. Shein alimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Uwekezaji, Vitega
Uvhumi Zanzibar (ZIPA), Salum Khamis Nassor kutoka maelezo na ufafanuzi juu ya
fursa na mikakati ya Serikali pamoja na Sheria zilizopo katika nyanja mbali
mbali za uwekezaji.
Aidha, alitoa ufafanuzi
juu ya masuala mbali mbali yaliyoulizwa na wanachama wa Jumuiya ambao nao kwa
upande wao wakiongozwa na Mwenyekiti wa Jumiya hiyo Majid Saif Al Ghurair ambaye
alitoa shukurani kwa Dk. Shein kwa kwenda kukutana nao na kumuhakikikishia
kwamba Jumuiya yake itaandaa mikakati maalum itakayowawezesha kuzifahamu na
kuzitumia fursa za wawekezaji zilizopo Zanzibar.
Mapema,
Dk. Shein alitembelea na kuona jinsi Bandari ya Jebel Ali inavyoendeshwa kwa
kutumia teknolojia ya kisasa na kuifanya kuwa ni miongoni mwa Bandari yenye ufanisi wa hali ya juu duniani
Dk. Shein alipata
maelezo kutoka kwa uongozi wa Bandari hiyo kwa jinsi inavyofanya kazi na
kuelezwa maslahi ya wafanyakazi, juu ya usalama wa bandari pamoja na mipango
iliyowekwa kayika kuhakikisha mizigo yote inatolewa salama na kwa wakati muwafaka
kwa kutumia teknolojiaya kisasa.
Katika ziara yake hiyo,
Dk. Shein alipendezewa na taarifa zilizotolewa na viongozi wa Bandari hiyo juu
ya mikakati ya utoaji wa mafunzo, kulinda na kuimarisha maslahi ya wafanyakazi
pamoja na mipango ya baadae iliyowekwa katika kuhakikisha sekta ya usafiri na
usafirishaji mizigo inaimarika.
Aidha, Dk. Shein alitembelea mradi wa mji mpya wa kisasa wa Nakheel pamoja na Mradi wa Palm Jumeirah
na kupata fursa ya kuona jinsi unavyoendeshwa na kuutembea huku akipataa
maelezo juu ya hatua zilizofikiwa katika mradi huo ikiwa ni pamoja na ufukiaji
mkubwa wa bahari uliofanyika na kueleza historia pamoja na jinsi sekta ya
utalii na biashara zilivyoimarika katika eneo hilo.
Pia. Dk. Shein alipata
maeleza juu ya uendelezaji sambamba na hatua zilizochukuliwa katika kuuimarisha
mji wa Dubai tokea miaka ya 1950 pamoja na azma ya ujenzi wa mji mpya wa kisasa
wa Nakheel na Mradi wa Palm Jumeirah ambao ni maarufu kwa utalii, uwekezai na
biashara kutokana na eneo hilo kuwa na nyumba za kuishi za kisasa, hoteli,
sehemu za kibiashara, burudani na za mapumziko.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment