Habari za Punde

Jeshi la Zimamoto Yajiweka Tayari Kwa Maokozi Majini.

 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye katika picha ya pamoja na Kikosi cha Maokozi cha Jeshi hilo, wakati alipotembelea Kikosi hicho kilipokuwa kikionesha zoezi la maokozi, kushoto ni Mrakibu Msaidizi wa Zimamoto Bashiri Madhehebi ambaye ni Mkuu wa kikosi hicho.
 Wazamiaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakimuonesha Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo (hayupo pichani), jinsi wanavyoweza  kufanya maokozi katika maji alipotembelea eneo la daraja la Mwalimu Nyerere Kigamboni walipokuwa wakifanya zoezi hilo, mapema leo asubuhi (kushoto) ni Sajini wa Zimamoto Salehe Salla na aliyevaa boya maalum kwa ajili ya maokozi ni Koplo wa Zimamoto Omary Katonga.
 Mzamiaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Sajini wa Zimamoto Saidi Sekibojo akiwa katika mazoezi ya uzamiaji katika eneo la Daraja la Mwalimu Nyerere mapema leo asubuhi, lengo ni kujiweka tayari kwa ajili ya Maokozi majini pindi ajali zinapotokea. 
Sehemu ya Askari wazamiaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakiongozwa na Koplo Omary Katonga (kulia) wakionesha utimamu mbele ya Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo (hayupo picha) mara baada ya kufanikiwa kumuokoa mhanga aliyekuwa kazama katika kina kirefu cha maji, wakati wa mazoezi ya uzamiaji katika eneo la Daraja la Mwalimu Nyerere mapema leo asubuhi, lengo ni kujiweka tayari kwa ajili ya Maokozi majini pindi ajali zinapotokea.
(Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji)

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA - JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.