Habari za Punde

Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi yafamya ziara Wizara ya Afya

 Waziri wa Afya wa Zanzibar Hamad Rashid Mohamed akiikaribisha Kamati  ilipofika ofisini kwake Mnazi mmoja kwa ajili ya kutoa mrejesho wa ziara yake iliyofanya katika Vitengo vya Wizara hiyo.
 Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Mwinyihaji Makame Mwadini akizungumza machache kabla ya Wajumbe wa Kamati yake kuchangia taarifa ya ziara yao kwa Vitengo vya Wizara hiyo.
 Katibu wa Wizara ya Afya Asha Abdulla akisoma taarifa ya Utekelezaji wa kazi za Wizara kwa kipindi cha mwezi Octoba-Disemba 2017/2018 mbele ya Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi.
 Mjumbe wa Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Mwanaasha Khamis Juma katikati akichangia taarifa iliyotolewa ya Kamati yao kwa Wizara ya Afya.
Mjumbe wa Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Masoud Ibrahim ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Bububu akipitia taarifa ya Utekelezaji wa kazi za Wizara ya Afya kwa kipindi cha mwezi Octoba-Disemba 2017/2018. Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Wizara ya Afya mnazi mmoja. Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.