Habari za Punde

WAZIRI WA AFYA ZANZIBAR AENDELEZA ZIARA YA KUTEMBELEA VITENGO MBALIMBALI HOSPITAL YA MNAZI MMOJA

 Mkuu wa wodi ya watoto Hospital ya Mnazi mmoja Fatma Ali Moh’d akimpatia maelezo Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed mwenye Kaunda suti wakati Waziri huyo alipofanya ziara za Vitengo vya Hosptal hiyo.
 Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed akimjulia hali mtoto Khairat Juma anaesumbuliwa na ugonjwa wa kuvuja damu, kulia ni Mkuu ya wodi ya kina mama na watoto Hospital ya Mnazi mmoja Dkt. Nasra S Ali.
 Mkurugenzi Mkuu Hospitali ya Mnazi mmoja Ali Salum Ali akielezea changamoto wanazokabiliana nazo katika utendaji wao wa kazi kwa uongozi wa Wizara ya Afya.
  Mkuu ya Wodi ya kina mama na watoto Hospitali ya Mnazi mmoja Dkt. Nasra S Ali akielezea upungufu wa Wauguzi katika Wodi hiyo wakati uongozi wa Wizara ulipofanya ziara katia vitengo vya Mnazi mmoja.
 Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Harusi Said Suleiman akielezea maendeleo yaliyofikiwa licha ya changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika Hosptial ya Mnazi mmoja.
Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed akizungumza na uongozi wa Wizara na Watendaji wa Hospital ya Mnazi mmoja mara baada ya kufanya ziara katika vitengo mbalimbali vya Hospital hiyo. Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.