Habari za Punde

Makamu Mwenyekiti Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) Ndg. Ali Mohammed Ajiuzulu Uongozi na Kuonesha Barua Yake Kwa Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba.


Makamu Mwenyekiti wa ZFA Pemba Ndg. Ali Mohammed ametangaza kujiuzulu nafasi yake hiyo mbele ya Waandishi wa habari za michezo Kisiwani Pemba na kuonesha barua yake ya kujiuzulu. 


Na.Abdi Suleiman -Pemba.
HATIMAE sinema ya kujiuzulu kwa viongozi wa juu wa Chama Cha Soka Zanzibar (ZFA) imeendelea, ambapo Makamu wa Rais wa ZFA Pemba Ali Mohammed Ali ametangaza rasmi kujiuzulu wadhifa huo.

Makamu huyo ameungana na Rais wa chama hicho Ravia Idarous Faina, Makamu wa Rais Unguja Mzee Zamu Ali na Abdull Ghani Msoma.

Akizungumza na waandishi wa habari Kisiwani pemba, Makamu huyo alisema hatua hiyo imekuja baada ya jitathmini kwa kina na kuona tayari viongozi wenzake wameshaachia ngazi nyazifa dhao.

Alisema kujiuzu kwake ni kutoa nafasi kwa viongozi wengine watakao pata nafasi ya kukiongoza chama hicho kw aupande wa Pemba.

“Baada ya kuona viongozi wenzangu wa juu wamejuuzulu nyazifa zao, sina budi na mimi nijuuzulu kama walivyofanya wenzangu, kuanzia tarehe hii ya Leo 13/6/2018”alisema.

Aidha aliahidi kutoa mashirikiano kwa viongozi wapya watakao kuja kukiongoza chama hicho, pale atakapo hutajika mchango wake kwa kuhakikisha soka la Zanzibar linapiga hatua.

“Siku yoyote nitakayohitajika kusaidia kwa michango, mawazo au lolote lile mimi nipo tayari kutoa michango wangu, ili kuona mpira wa Zanzibar unasonga mbele”alisema.

Hata hivyo Makamu Ali Mohamed aliwaomba Radhi wale wote aliowakosea, katika kipindi chote cha uongozi wake katika chama cha mpira wa miguu Zanzibar upande wa Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.