Habari za Punde

Wajumbe wa Kamati Tendaji ya ZFA Wajiuzuli Uongozi.


Na.Abdi Suleiman -Pemba.
HATIMAE wajumbe kamati Tendaji ya chama cha soka Zanzibar ZFA Taifa, wamezikataa barua za kujiuzulu kwa Viongozi wa juu wa Chama hicho Zanzibar.
Wajumbe wa kamati hiyo waliokutana leo katika ofisi ya ZFA Pemba zilizomo uwanja wa michezo Gombani, huku kikao hicho kikiongozwa na Mwenyekiti wake Sharif Juma Saidi.

Akizungumza na waandishi wa habari za Michezo Pemba, mwenyekiti huyo alisema wajumbe wamezikataa barua za viongozi hao wa juu, kwa lengo la kuepuka kadhia ambayo inayoweza kuipata hapo mbele, kutokana na timu za Zanzibar zinatarajiwa kushiriki mashindano mbali mbali ya kimataifa.

Alisema awali kabla ya kuanza kikao hicho, walianza kwa kupitia vifungu mbali mbali vya katiba ya ZFA ya 2010, ikiwemo kupata idadi ya wajumbe wa Upande wa Pemba.

Alisema Pemba inawajumbe 14 na waliohudhuria katika kikao hicho ni wajumbe 13, huku wakitumia kifungu cha 12 katika katiba hiyo ili kupata maamuzi na kikao vya ZFA, pamoja na kusema kikao hicho kimepata Baraka kutoka kifungu cha 12:2(ii) na kuwa halali.

“Kilichotuleta hapa ni kupitia barua ya Makamu wa Rais wa ZFA Pemba Ali Mohamed Ali, aliyowasiliza ZFA juu ya kujuuzulu kwake Juni 13 mwaka huu”alisema.

Mwenyekiti huyo alisema baada ya kuipitia barua hiyo kwa mujibu wakatiba ya ZFA ya 2010, suara ya 12 kifungu cha 92 kimesema bila ya kujali sababu yoyote, mjumbe yoyote anayohaki ya kujiuzulu katika wadhifa alionao, 92:1 kimesema mjumbe hatajiuzulu mpaka apelike kwa tendaji katika ngazi inayohusika, ndipo kifungu cha 92:2 ndicho kilichowapa nafasi ya kusikiliza ombi la mjumbe.

“Sisi hapa hatukaja kujadili bali tumekuja kukubali ombi lake au kukataa ombi lake la kujiuzulu wadhifa wake tu”alisema.

Aidha alisema baada ya kufikia muwafaka wajumbe waliweza kutumia kifungu cha 36 katika katiba ya 2010 ya ZFA juu ya upigaji wa kura, ili kufikia maamuzi ambapo maamuzi yanaweza kufikiwa kwa njia ya upigaji wa kura, (i) upigaji wa kura utakuwa wa siri kwa kamati tendaji (ii) maamuzi yaweze kuafikiwa na wajumbe.

Alisema upigaji wa kura hizo wajumbe 13 waliohudhuria kikao hicho, kura mbili ziliharibuka na kura Tano ziliweza kukubali kujiuzulu kwa makamu huyo wa Rais wa ZFA, huku kura sita ziliweza kumkatalia maamuzi yake ya kujuuzulu wadhifa huo na wajumbe kumtaka katibu wa ZFA Taifa, kumuandikia barua ya kurudi tena katika nafasi yake ya uongozi.

“Kutokana na maamuzi hayo ya wajumbe ya upigaji wa kura, kikao hicho hakikuridhia kujiuzulu kwa makamo huyo” huku wakimtaka katibu Mkuu kumuandikia barua ikizingatiwa mbele kuna hatua ya nane bora ya ligi kuu ya zanizbar.

Wakati huo huo alisema Kamati hiyo ilikaa kikao Juni 12 ambapo wajumbe walikuwa 10 na kora iliweza kutimia kwa kupitia barua mbili, ikiwemo ya kujiuzulu kwa Rais wa ZAF Ravia Idarous Faina na Mkurugenzi wa Ufundi Abdullghan Mssoma ambayo ilikwenda kwa Rais.

Alisema kura 10 ziliweza kumkatalia kujiuzulu kwa Ravia na kumtaka katibu mkuu kumuandikia barua ya kurudi madarakani, huku Mzee Zam Ali akiridhiwa kujiuzulu kwake kutokana na sababu mbali mbali alizozieleza katika barua yake.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.