NA/ HAJI NASSOR, PEMBA
WANAWAKE waliomo kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini
kijiji cha Mkumbi shehia ya Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba, ambao wamekujisanya
pamoja na kuzalisha sabuni, wamesema wameshaondoka na utamaduni wa kukopa fedha
kwa jirani, na sasa wanatumia kupitia ushirika wao.
Wamesema
kwa sasa ushirika wao pamoja na kwamba bado ni mchanga, lakini umeshaanza
kuwanesha njia ya mafanikio, kwa kule kuwa na sehemu ya uhakika wa kukopa fedha
kwa ajili ya kuendeshea maisha.
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi, wanaushirika hao wa ‘mwanzo mgumu” walisema kabla
ya kuja kwa TASAF na kuwawezesha kifedha walikuwa wakipata usumbufu pale wanapotaka
fedha hata shilingi 500/= kwa ajili ya kuondowa shida zao.
Walieleza
umaskini wao hasa ulikuwa kwenye kipato, jambo ambalo lilikuwa likiwakosesha
raha na furaha ya maisha hasa pale wanapohitaji fedha kwa ajili kutatua shida
zinazowakabili.
Mmoja
kati ya wanachama hao, Fatma Rashid Hassan, alisema sasa ule utamduni wa
kumpigia magoti jirani au wafanyabiashara kwa kukopa fedha ameshaanza kuusahau,
kwa vile ushirika wao umekuwa mkombozi.
Alisema
fedha wanazowezeshwa na TASAF wao huzifanya kama za kununulia Madira na
vipodozi pekee, bali waliamua kujikusanya pamoja idadi ya watu 15, na kuanzisha
ushirika ambao leo wameshaanza kula matunda yake.
“Mimi
sasa sikumbuki kumkopa mtu fedha kwa Tshilingi 100,000/= hadi Tshilingi 200,000/=,
maana nikichacha napiga hodi kwenye ushirika wetu, jambo ambalo zamani sikuwahi
kuzishika fedha kama hizo zikawa zangu,”alieleza.
Nae,
Mwanajuma Makame Khatib, alisema ipo tofauti kubwa kabla na baada ya kuingia
katika ushirika huo, kufutia kupokea fedha za TASAF za kunusuru kaya maskini.
Alieleza
kwa sasa anajihisi nae ni sehemu ya mtu
mwenye maisha mazuri, kwa kule kuwa na uhakika wa kitu anachokihitaji jambo
ambalo hapo kabla ilikuwa vigumu.
“Kwa
kweli kwa sasa mimi binafsi sasa najihisi nimeshakomboka na umaskini hasa kwa
hali ya maisha niliokuwa nayo kabla ya kuja TASAF na kuanzisha ushirika huu wa
utengenezaji sabuni, maana ilikuwa tatizo na kipato,”alieleza.
Hata
hivyo alisema amekuwa na msaada mkubwa ndani ya familia yake kwa kuchangia
fedha za mahitaji ya kila siku wa wastani wa Tshilingi 5000/= kwa siku.,
Mapema
Mwenyekiti wa ushirika wa uzalishaji sabuni Mwanaidi Khamis Kombo, alisema bado
wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa soko la uhakika, ingawa kwa sasa
wameanza kuuzia wanachama wenyewe.
Mwenyekiti
huyo alisema, bado mafunzo waliopewa ya utengenezaji sabuni, bado hayajatosheleza
na wanahitaji mafunzo zaidi ya uzalishaji sabuni iliobora.
“Kwa
kweli soko bado dogo, lakini inawezekana linasababishwa na kwamba
hatujaitangaaza sana sabuni yetu, maana bado ushirika wetu ni
mchanga,”aliekeza.
Nae
Katibu wa ushirika huo wa ‘mwanzo mgumu’, Fatma Juma Kombo, alisema waliamua
kujiingiza kwenye utengenezaji wa sabuni ili kujikombowa na umaskini.
Alieleza
pamoja na kuwa na mradi huo wakati
wowote wataanza na kilimo cha mboga mboga pamoja na ufugaji, ili kusaka njia ya
kuhakikisha TASAF, ikimalizika wao wasirudi tena kwenye umaskini.
“Hali
zetu za kimaisha kwa kweli zimeimarika ukilinganisha hapo zamani, na kama soko
letu la sabuni litasimama badi sisi hatutoitwa tena kaya maskini,”alifafanua.
Mapema Mratibu wa TASAF Pemba, Mussa Said
Kisenge, amekuwa akirudia kauli yake ya kuwataka wananchi waliomo kwenye mpango
wa kunusuru kaya maskini kubuni miradi ambayo itawakomboa na umaskini.
Alisema
haitopendeza hata kidogo, kuona wananchi hao waliomo kwenye mpango huo,
wanarudi tena kwenye umaskini mkubwa, mara TASAF itakapo ondoka kuwawezesha
kifedha
Katika
mikoa miwili ya Pemba, TASAF inawalengwa 14,378 wanaopokea fedha ambapo tayari
wameshanzisha vikundi 942 vikiwemo vinavyojishughulisha na kilimo, ufugaji wa
wanyama, utengenezaji sabuni, uhifadhi wa mazingira na kilimo cha Alizeti.
No comments:
Post a Comment