NAIBU
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso na Mbunge wa Jimbo la Pangani
(CCM) akizungumza na wananchi wa Jimbo hilo kwenye mkutano wa hadhara
uliofanyika sokoni mjini Pangani ambako pamoja na mambo mengine aliweza
kusikiliza kero zao zinazowakabili
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso na Mbunge
wa Jimbo la
Pangani (CCM) akizungumza na wananchi wa Jimbo hilo kwenye mkutano wa
hadhara uliofanyika sokoni mjini Pangani ambako pamoja na mambo mengine
aliweza kusikiliza kero zao zinazowakabili
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso na Mbunge
wa Jimbo la
Pangani (CCM) akiwa amebebwa juu na wananchi mara baada ya kumaliza
kuwahutubia
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso na Mbunge
wa Jimbo la
Pangani (CCM)kulia akiwa na Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa
Abdallah wakifuatilia hoja za wananchi kwenye mkutano huo
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso na Mbunge wa Jimbo la
Pangani (CCM) kushoto akimtunza mmoja wa wananchi
sehemu ya wananchi wa mji wa Pangani wakimfuatilia NAIBU Waziri
wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso na Mbunge wa Jimbo la
Pangani (CCM)
Wananchi wakimfuatilia NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa
Aweso na Mbunge wa Jimbo la
Pangani (CCM)
Na.Assenga Oscar
SERIKALI
ya awamu ya tano imeombwa kuangalia namna ya kuanza ujenzi wa barabara
ya Tanga-Pangani, Saadan hadi Bagamoyo ili kuweza kumaliza kilio cha
wananchi wa wilaya ya Pangani cha muda mrefu ikiwemo kufungua fursa za
kiuchumi na maendeleo kwa mkoa .
Ombi hilo lilitolewa na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso
wakati akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara wilayani humo ambapo
alisema pamoja na kuwepo kwa miradi mingi inayotekelezwa huko lakini
kilio kikubwa cha wananchi wake ni ukosefu wa barabara nzuri.
Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) alisema wakati Rais
Magufuli akiomba kura kwa wananchi hao mwaka 2015 aliwaahidi wananchi
ujenzi wa barabara hiyo na walikubali kumpa kura nyingi na imani kubwa
kwake kwa mategemeo ya kumpata mkombozi atakae weza kumaliza kero hiyo
ambayo imedumu katika awamu zote nne zilizopita bila ya mafanikio.
“Kwenye mkutano wangu wa leo hii nipo hapa nyumbani kama Mbunge wenu
kawaida na sikuja kama Naibu Waziri na jukumu la Mbunge ni kuwasemea
wananchi wake Mh Rais wananchi wangu kiukweli wanalia na suala la
barabara hii na hawajui hatma yake lini mradi huu utaanza”Alisema Aweso.
Hata hivyo alisema kuzorota kwa uchumi na maisha magumu kwa wananchi wa
wilaya hiyo unachangiwa kwa kiasi kikubwa na tatizo la kutokujengwa
barabara ambayo ingesaidia kufungua wilaya hiyo ambayo inaonekana kama
imesahaulika katika nyanja zote.
Hata hivyo akionyesha kuunga mkono ujenzi wa barabara hiyo Mkuu wa Mkoa
Tanga Martin Shigella alimueleza Waziri wa Fedha na Mipango Phillip
Mpango juu ya umuhimu wa barabara ya Tanga, Pangani hadi Saadan wakati
wa uzinduzi wa Tawi jipya la Benki ya Kiislam ya Amana
“Mh kilio kikubwa ni tatizo la barabara ya Tanga –Pangani Saadani
tunaomba mtusaidie suala hilo kwani hakuna ukombozi unatarajiwa na
wananchi wengi mkoani Tanga zaidi ya ujenzi wake”Alisema.
Shigella alimueleza hadharani Waziri huyo wa fedha kuwa Serikali
inapaswa kufanya kila njia kuhakikisha inatenga fedha za kutosha ili
kukamilisha mradi huo ambao bado hatma yake haijulikani utaanza lini.
Alisema Tanga ni Mkoa ambao unafunguka kiuchumi hasa katika swala zima
la viwanda na matarajio ya barabara hiyo inaweza kurahisisha shughuli
mbalimbali za kibiashara, usafirishaji wa mazao na utalii katika Mbuga
ya Saadan hivyo ni jukumu la Serikali kuhakikisha barabara hiyo
inajengwa.
“Waziri wa fedha tunaomba mchako wa fedha kwa ajili ya barabara hiyo
ufanyike kwa wakati ili kuwakomboa wananchi wa maeneo hayo na kukuza
pato la Mkoa,Wilaya na hata mtu mmoja mmoja”Alisema Shigella.
Awali akizungumzia suala la ujenzi wa barabara hiyo Waziri wa Fedha na
Mipango Dk Philp Mpango alisema wamiliki wa viwanda,wafanyabiashara
wakubwa na wadogowadogo wajitahidi kulipa kodi ili fedha hizo ziweze
kujenga miundombinu ndani ya Nchi.
Alisema Serikali kupitia ukusanyaji wa kodi zake inahakikisha inatenga
fedha kwa ajili ya ujenzi na ukatabati wa miundombinu ili kuondoa
kerokwa wananchi katika maeneo husika.
No comments:
Post a Comment