Habari za Punde

Tetesi za Soka Ulaya.: Pogba, Cahill, Henry, Strootman, Ramires, Grealish

Beki wa Uhispania na Barcelona Gerard Pique, 31, anasema itakuwa vyema sana iwapo kiungo wa kati wa Manchester United aliyeshinda Kombe la Dunia akiwa na Ufaransa Paul Pogba, 25, atahamia Nou Camp siku zijazo. (AS)
Beki wa England anayechezea Chelsea Gary Cahill, 32, yuko tayari kusalia na kupigania nafasi yake baada ya kuonekana kuwekwa pembeni katika kikosi cha Maurizio Sarri. (Telegraph)
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal na Ufaransa Thierry Henry, 41, anatarajiwa kuikataa nafasi ya kuwa meneja wa Bordeaux kwa sababu ya wasiwasi kuhusu ukosefu wa fedha katika klabu hiyo ya Ligue 1. (Sun)


Beki wa West Ham Reece Oxford, 19, anatafutwa kwa mkopo na klabu ya Eibar inayocheza ligi kuu Uhispania, klabu ambayo iko tayari kulipa ada ya £1.8m ya uhamisho wa mkopo. (Marca)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.