Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kiwanda cha wakala wa Serikali wa uchapaji Zanzibar Nd,Mohamed Suleiman alipofanya ziara leo ya kutembelea katika Ofisi hiyo iliyopo Maruhubi Wilaya ya Magharibi "A" Mkoa wa Mjini Magharibi.
Na.Rajab Mkasaba Ikulu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein
alitembelea Ofisi ya Wakala wa Serikali wa Uchapaji Zanzibar iliyopo Maruhubi
nje kidogo ya mji wa Zanzibar na kusisitiza haja ya kuchapishwa kopi nyingi za
Gazeti la ‘Zanzibar Leo’ ambalo ni gazeti la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Alieleza kuwa ipo haja
ya kuliimarisha zaidi soko la ndani la gazeti hilo kabla ya kuliimarisha soko
la nje huku akitumia fursa hiyo kueleza uwezo mkubwa wa kiwanda hicho ambacho
kina mashine mpya na za kisasa ambazo hakuna kiwanda hata kimoja cha binafsi
hapa nchini chenye mashine hizo.
Aidha, Rais Dk. Shein
alieleza kuwa katika kwianda hicho kuna mashine ambazo katika bara la Afrika ni
viwanda vichache ambavyo unaweza kuzikuta mashine hizo ambapo kwa hivi sasa
mashine hizo kwa upande wa gazeti zina uwezo wa kuchapishwa magazeti kopi
30,000 kwa saa moja.
Alisisitiza kazi kubwa
ya kuliuza gazeti hilo na kuhakikisha wananchi waliowengi wa Unguja na Pemba wanapata gazeti hilo na kuhakikisha
asilimia kumi ya wananchi wa Zanzibar wanapata gazeti hilo. Mapema Dk. Shein
alipata fursa ya kukagua eneo hilo la Ofisi ya Wakala na kuziona mashine zake.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment