Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Mamlaka
ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA)
imesema kuwa Serikali imejipanga
kumaliza tatizo la maji katika jiji la Dar es Salaam ifikapo mwaka 2020. Ambapo upatikanaji
wa huduma za maji utakuwa asilimia 95
kwa maji safi na asilimia 30
kwa majitaka.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es
salaam, kuhusu mafanikio ya Taasisi hiyo katika kipindi cha miaka mitatu ya
Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Afisa
Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Cyprian Luhemeja alisema kuwa tatizo la maji
katika jiji la Dar es Salaam litaisha ifikapo mwaka 2020 kwa kuwa Serikali
imeandaa mfumo mpya utakaosadia wananchi kupata huduma ya maji kwa uhakika.
“Katika
mradi wa mfumo wa usambazaji wa majisafi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam mpaka
Bagamoyo ambapo mabomba yenye urefu wa
Kilomita 1,426 yatalazwa na
wateja wapya zaidi ya 300,000
wataunganishwa”
Mhandisi Luhemeja, aliongeza kuwa “vilevile mradi wa mifumo midogo midogo inayojitegemea
ya usambazaji maji kwenye maeneo yasio na mtandao (off grid water supply
schemes) ambapo kutakuwa na maunganisho ya wateja wapya 100,000 yatasaidia kumaliza tatizo hilo”
Aidha, alitaja mikakati mingine ambayo Serikali
imeiweka kwa ajili ya Jiji la Dar es
Salaam kuwa ni kuimarisha mifumo ya usambazaji wa majisafi maeneo ya kusini mwa
Dar es Salaam (Part 4D na 4E) ambapo mabomba yenye urefu wa Kilomita 400
yatalazwa na wateja wapya zaidi ya 71,600 wataunganishwa, ikiwa ni sambamba na
mradi wa kudhibiti upotevu wa maji.
Pia, alisema mafanikio ya Serikali katika kipindi
cha miaka mitatu ni pamoja na miradi ya ujenzi wa mifumo mipya ya majitaka
na mitambo ya kisasa ya kuchakata majitaka katika maeneo ya Jangwani, Kurasini
na Mbezi Beach, ikiwa ni pamoja na kumalizia uchimbaji wa visima vya Kimbiji na
Mpera na kujenga mifumo ya usambazaji maji .Pamoja na kujenga bwawa
la Kidunda ili kuwa na uhakika wa maji kwenye
mto Ruvu katika kipindi chote cha mwaka.
No comments:
Post a Comment