Habari za Punde

Zanzibar Itaendelea Kuimarisha Uhusiano Uliopo Kati yake na Taifa la Palestine.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Balozi Mpya wa Palestine Nchini Tanzania Mr. Hamdi M.H. Abuali,alipofika Ikulu Zanzibar kujitambulisha na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar Dk.Shein, Ikulu Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amesema Zanzibar itaendelea kuimarisha ushirikiano uliopo kati yake na Taifa la Palestina, kwa maslahi mapana ya watu wa nchi mbili hizo.

Amesema uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya nchi mbili hizo ni wa muda mrefu, tangu enzi za muasisi wa Taifa hilo, Hayat
Yasser Arafat,  ukijikita katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Dk. Shein amesema hayo leo Ikulu mjini Zanzibar, alipozungumza na Balozi mpya wa Palestina nchini, Hamdi M.H. Abuali, aliefika kujitambulisha.

Alisema Serikali imeazimia kupanua wigo wa ushirikiano na Palestina katika nyanja za kiuchumi na kijamii, hususan kupitia sekta za Utalii, afya pamoja na biashara zitokanazo na kilimo.

Alisema pamoja na Taifa hilo kupitia katika changamoto mbali mbali za kiusalama, tayari imepata mafanikio makubwa, hivyo ipo haja kwa nchi mbili hizo kushirikiana katika suala la mafunzo pamoja na kubadilishana wataalamu.

Dk. Shein,aliwataka wananchi wa Palestina kujidhatiti na kuongeza juhudi katika harakati za kudai haki yao, kwa kuamini kuwa iko siku watafanikiwa.

Nae, Balozi Abuali alimuahakikishia Dk. Shein azma ya Taifa hilo kuendeleza ushirikiano uliopo kati yake na Zanzibar, ili kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Alisema  Palestina itafanya kila juhudi kuhakiksha kunakuwepo mafungamano mema kati ya nchi mbili hizo, ili kuona sekta zilizoainishwa zinakuwa chachu ya kuendeleza uchumi wa Zanzibar


Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822 
 E-mail: abdya062@gmail.com


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.