WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akizungumza
wakati wa halfa ya kukabidhi mabati 200 kwa ajili ya kusaidia ujenzi
wa shule tano Jijini Tanga kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias
Mwilapwa
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia
akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia
ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa
Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati
200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya
ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Hamis
Mkoba
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa
Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati
200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya
Tanga Thobias Mwilapwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Hamis Mkoba
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee
na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu
kulia akimkabidhi Mabati 200 Naibu Meya wa Jiji la Tanga Mohamed Haniu
baada ya kumkabidhi Mkurugenzi wa Jiji hilo Daudi Mayeji
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii
Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ametoa mabati 200 yenye thamani
yash.milioni 4.2 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa shule tano za
Sekondari Jijini Tanga.
Halfa ya makabidhiano hayo
yalifanyika mjini Tanga kwenye shule ya Msingi Mwakidila ambapo
Mkurugenzi wa Jiji hilo alipokea mabati hayo ikiwa ni mkakati wa
Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga
kusaidia kuondosha changamoto ya uhaba wa madarasa.
Akizungumza mara baada ya
kukabidhi mabati hayo, Waziri Ummy aliwashauriwa wazazi na walezi
kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya watoto wao jambo ambalo linaweza
kuwasaidia kufanya vizuri kwenye masomo yao.
“Ndugu zangu
wazazi na walezi hakikisheni mnafuatilia maendeleo ya watoto wenu
wanapokuwa shuleni kwani nyie pia mnaweza kuchangia ufaulu wa mtoto
wako “Alisema.
Aidha pia Waziri Ummy amehaidi kuchangia
ujenzi wa madarasa kwenye shule ya Sekondari Kange ili kuchochea
ukuaji wa sekta ya elimu kwa mkoa wa Tanga .
“Lakini pia
niwashukuru watendaji wa Shirika la Tawode kwa kujitoa katika
kuchangia maendeleo ya Jamii ya Tanga kwa kutafuta wafadhili
mbalimbali wa ndani na nje ya mkoa huu”Alisema
No comments:
Post a Comment