Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bi. Madina Mjaka , akitowa taarifa kuhusiana na Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidatu cha Nne Zanzibar, na Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Wizara Mazizini Unguja.
Kwa
heshima naomba kuwasilisha Taarifa kuhusu Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato
cha Nne mwaka 2018 kwa Skuli za Sekondari za Zanzibar. Taarifa hii inafanya pia
ulinganisho na matokeo kama hayo na Skuli za Tanzania kwa ujumla. Pia taarifa
hii italinganisha matokeo ya mtihani kama huo kwa mwaka 2017.
2.0
UANDIKISHAJI
WA WATAHINIWA
Mtihani wa Kidato cha Nne, mwaka 2018,
ulifanyika nchini kote kuanzia tarehe 05/11/2018 hadi 23/11/2018. Jumla ya
watahiniwa 426,988 waliandikishwa kufanya mtihani huo wakiwemo wasichana
219,171 (51.33%) na wavulana 207,817(48.67%).
Kwa upande wa skuli za Zanzibar, jumla ya
watahiniwa 17,098 waliandikishwa kutoka skuli 213, kati ya hizi skuli 164 ni za
Serikali ambazo zimeandikisha wanafunzi 15,168 na skuli 49 ni za Binafsi ambazo
zimeandikisha wanafunzi 1,930. Jumla ya
wanafunzi 16,654 walifanya mtihani mwaka 2018 sawa na asilimia 97.4 ya
watahiniwa walioandikishwa kati yao 9,886 ni wasichana sawa na asilimia 59 na
watahiniwa 7,212 ni wavulana sawa na asilimia 43.3. Aidha, jumla ya watahiniwa
444 sawa na asilimia 2.6 ya watahiniwa walioandikishwa hawakufanya mtihani.
3.0 MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2018
Jumla ya watahiniwa 322,965 sawa na asilimia
78.38 ya watahiniwa waliofanya mtihani kwa
Tanzania nzima wamefaulu. Wasichana waliofaulu ni 163,920 sawa na asilimia
77.58 wakati wavulana ni 159,045 sawa na asilimia 79.23. Kwa ujumla, asilimia
ya ufaulu imeongezeka kwa 1.29 ukilinganisha na
asilimia 77.09 ya mwaka 2017.
Kwa upande wa Skuli za Zanzibar, watahiniwa
16,654 sawa na asilimia 72.7 ya watahiniwa wote wa skuli za Zanzibar wamefaulu.
Kwa ujumla asilimia ya ufaulu imeongezeka kwa asilimia 1.9 ya mwaka 2017.
JADWELI NA 1: MADARAJA
YA UFAULU
DARAJA
|
TANZANIA
|
ZANZIBAR
|
||
IDADI
|
ASILIMIA
|
IDADI
|
ASILIMIA
|
|
I
|
13,524
|
3.77
|
225
|
1.4
|
II
|
39,665
|
11.07
|
997
|
6.0
|
III
|
60,636
|
16.92
|
2,039
|
12.2
|
I – III
|
113,825
|
31.76
|
3,261
|
19.6
|
IV
|
170,301
|
47. 51
|
8,845
|
53.1
|
I – IV
|
284,126
|
79.27
|
12,106
|
72.7
|
0
|
74,301
|
20.73
|
4,548
|
27.3
|
4.0
UFAULU
KIMASOMO
Takwimu
za matokeo zinaonesha kuwa ufaulu katika masomo ya Historia, Kiswahili,
Hesabati, Physics, Chemistry na Book-keeping umepanda kati ya asilimia 0.83
hadi 8.76 ikilinganishwa na mwaka 2017.
Watahiniwa
wengi wamefaulu zaidi katika somo la Kiswahili sawa na asilimia 89.32. Aidha, ufaulu
wa chini kabisa ni wa somo la Hesabati ambapo ni asilimia 20.02 tu ya wanafunzi
wote wa skuli walifanya somo hilo wamefaulu.
Mchanganuo
wa ufaulu kimasomo katika mtihani wa Kidato cha Nne 2018 ukilinganisha na mwaka
2017 unaonekana katika jadweli lifuatalo: -
JADWELI
NA 2: ASILIMIA YA UFAULU KWA MASOMO
WALIOFAULU
2018
|
WALIOFAULU
2017
|
|
ASILIMIA
|
ASILIMIA
|
|
CIVICS
|
57.25
|
58.75
|
HISTORY
|
57.29
|
55.99
|
KISWAHILI
|
89.32
|
84.42
|
ENGLISH
|
66.30
|
67.86
|
GEOGRAPHY
|
53.03
|
53.18
|
BIOLOGY
|
60.89
|
61.37
|
CHEMISTRY
|
62.15
|
53.39
|
PHYSICS
|
45.50
|
42.17
|
BASIC MATHEMATICS
|
20.02
|
19.19
|
COMMERCE
|
42.66
|
46.45
|
BOOK-KEEPING
|
44.67
|
40.82
|
Skuli
zetu za Mikunguni na Lumumba zimeonesha ufaulu mzuri kwa baadhi ya masomo kwa
upeo wa Tanzania.
Lumumba Sekondari
Dini 8/1045
|
Physics 20/ 4539
|
Chemistry 26/4784
|
Mikunguni Sekondari
Workshop technology 1/10
|
Electrical installation 1/10
|
Fitting and turning 1/10
|
Electrical Drafting 1/10
|
Building construction 2/10
|
Carpentry and joinery 2/10
|
TV and radio service 2/10
|
Mechanical drafting 2/10
|
5.0
SKULI
KUMI BORA NA SKULI KUMI ZA MWISHO
Ubora wa skuli umepangwa kwa kutumia kigezo cha wastani wa
pointi (Grade Point Average – GPA) katika ufaulu wa masomo kwa wanafunzi katika
skuli ambapo mchanganuo ni A=1, B=2, C=3, D=4 na F=5.
Kwa upande wa Zanzibar skuli kumi bora
zilizokuwa na wanafunzi 40 au zaidi ni hizi zifuatazo: -
NAFASI
|
JINA LA SKULI
|
IDADI YA WATAHINIWA
|
MKOA
|
1.
|
LUMUMBA
|
112
|
MJINI/MAGHARIBI
|
2.
|
FIDEL CASTRO
|
67
|
KUSINI PEMBA
|
3.
|
LAUREATE INT.
|
48
|
MJINI/MAGHARIBI
|
4.
|
TUMEKUJA
|
122
|
MJINI/MAGHARIBI
|
5.
|
SOS
|
55
|
MJINI/MAGHARIBI
|
6.
|
HIGHVIEW
|
57
|
MJINI/MAGHARIBI
|
7.
|
MAHAD ISTIQAMA
|
44
|
KUSINI UNGUJA
|
8.
|
MIKUNGUNI
|
48
|
MJINI/MAGHARIBI
|
9.
|
GLOURIOUS ACADEMY
|
72
|
MJINI/MAGHARIBI
|
10.
|
WETE SECONDARY
|
60
|
KASKAZINI PEMBA
|
NAFASI
|
JINA LA SKULI
|
IDADI YA WATAHINIWA
|
MKOA
|
1.
|
P/MCHANGANI
|
60
|
KASKAZINI UNGUJA
|
2.
|
UKUTINI
|
51
|
KUSINI PEMBA
|
3.
|
KIJINI
|
55
|
KASKAZINI UNGUJA
|
4.
|
NG’AMBWA
|
101
|
KUSINI PEMBA
|
5.
|
HAMAMNI
|
175
|
MJINI MAGHARIBI
|
6.
|
KANGAGANI
|
50
|
KASKAZINI PEMBA
|
7.
|
WAMBAA
|
56
|
KUSINI PEMBA
|
8.
|
KENGEJA
|
80
|
KUSINI PEMBA
|
9.
|
DONGE
|
124
|
KASKAZINI UNGUJA
|
10.
|
KINOWE
|
64
|
KASKAZINI PEMBA
|
5.1 WATAHINIWA 10
WA ZANZIBAR WALIOFANYA VIZURI ZAIDI MWAKA 2018
WANAFUNZI KUMI BORA
|
||||
S/N
|
JINA LA MWANAFUNZI
|
JINSIA
|
ALAMA
|
SKULI
|
1
|
HASSAN
HAMID USSI
|
M
|
7
|
LUMUMBA
|
2
|
YAHYA ALI
HEMED
|
M
|
8
|
LUMUMBA
|
3
|
YUSSUF
UBWA MOHAMMED
|
M
|
9
|
LUMUMBA
|
4
|
MOHAMMED
ABDALLA MBAROUK
|
M
|
9
|
LAUREATE
|
5
|
FAIZA SULEIMAN
KHAMIS
|
F
|
10
|
LUMUMBA
|
6
|
HIDAYA
SAID RASHID
|
F
|
11
|
LUMUMBA
|
7
|
ALI JUMA
SAID
|
F
|
11
|
LUMUMBA
|
8
|
MOHAMMED
FADHIL JUMA
|
M
|
11
|
LUMUMBA
|
9
|
HASSAN
MRISHO SHARIA
|
M
|
11
|
JKU
|
10
|
SAID
MBAROUK SHEBA
|
M
|
11
|
JKU
|
6.0
TATHMINI YA JUMLA YA MATOKEO YA KIDATO
CHA
NNE 2018
Matokeo
ya jumla ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2018 ya watahiniwa wa skuli
yanaonesha kuwa ufaulu kwa jumla umeongezeka kwa asilimia 1.29 kutoka asilimia
77.09 mwaka 2017 hadi asilimia 78.38 mwaka 2018. Aidha, takwimu zinaonesha kuwa
idadi ya watahiniwa waliopata ufaulu mzuri wa daraja la I-III imeongezeka
ambapo mwaka wa 2016 ilikua ni asilimia 27.60, mwaka 2017 asilimia 30.15 na
mwaka 2018 imekua ni 31.76. Kwa upande wa Zanzibar takwimu zinaonesha kuwa
idadi ya watahiniwa waliopata ufaulu mzuri wa daraja la I-III imeongezeka kutoka
asilimia 18.8 mwaka 2017 na kufikia asilimia 19.6 mwaka 2018.
Pamoja
na kuongezeka kwa asilimia ya ufaulu, takwimu zinaonesha kuwa ufaulu wa masomo
ya Physics, Basic Mathematics, Commerce na Book-keeping upo chini ya asilimia
hamsini (50%).
Hakuna
tokeo lolote la kufutwa au kuzuiliwa matokeo ya mitihani katika skuli za Unguja
na Pemba.
9.0
HITIMISHO
Matokeo
ya mtihani wa Kidato cha Nne ya mwaka 2018 kwa skuli za Zanzibar ni ya wastani. Idadi
ya watahiniwa waliopata sifa za kujiunga na masomo ya Kidato cha Tano na
Taasisi ya Ufundi ya Karume imeongezeka kutoka 3,033 (2017) hadi 3,261 (2018).
Hata
hivyo idadi ya wanafunzi waliofaulu kwa madaraja ya kwanza hadi tatu ni ndogo
(19.6%) ikilinganishwa na wale wanaofaulu kwa daraja la nne (53.2%). Hali hii
imepelekea mikoa ya Zanzibar kuwa ya mwisho katika wastani wa ufaulu kwa upeo
wa Tanzania.
Wizara
itaendelea na juhudi zake za kuzipatia skuli vifaa vya kufundishia pamoja na kuajiri
walimu wenye sifa ili kuinua kiwango cha ufaulu.
Aidha,
Wizara inaendelea kuwaomba wazazi na jamii kwa jumla kuendelea kushirikiana
nasi katika kufuatilia maendeleo ya Watoto ili lengo la Wizara la kutoa elimu
bora lifikiwe.
“Together, we can!”
Ahsanteni.
No comments:
Post a Comment