STATE HOUSE
ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 18, February, 2019
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amesema
kazi za ujenzi wa Bandari ya Mafuta na Gesi katika eneo la Mangapwani Mkoa wa
Kaskazini Unguja, zimeanza.
Amesema
ujenzi huo utakaofanyika katika eneo lenye ukubwa wa kilomita sita pia
utahusisha ujenzi wa matangi ya kuhifadhia mafuta, sambamba na ujenzi wa
barabara pana kuelekea eneo la bandari ili kuziwezesha gari kupita vizuri.
Dk.
Shein amesema hayo katika Hoteli ya Sea
Cliff Mangapwani, alipozungumza na Kamati za Siasa za Wilaya Kaskazini 'B'
Unguja pamoja na viongozi wa ngazi mbali
mbali wa chama wa Wilaya hiyo, ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake za kutembelea
Wilaya zote za Unguja na Pemba, kukaguwa miradi
ya maendeleo na utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Aidha,
katika mkutano huo Dk. Shein alifanya majumuisho ya ziara yake hiyo na kutoa
nasaha kwa wanachama hao.
Alisema
ujenzi huo umeanza baada ya kukamilika hatua zote za kulipa fidia vipando vya
wananchi wa eneo hilo la Dundua, kuku hatua za kuwahamishia katika makaazi
mapya zikichukuliwa.
Amesema
wawekezaji wa mradi huo tayari wamekabidhiwa eneo kwa ajili ya ujenzi wa
matangi ya mafuta na kubainisha kuwa matangi yaliopo Mtoni hivi sasa
yatahamishiwa huko.
Dk.
Shein alisema miundombinu ya umeme nayo
tayari imeshawekwa katika eneo la mradi.
Katika
hatua nyengine Dk. Shein alisema ameridhishwa na taarifa ya utekelezaji wa
Ilani ya CCM ya Wilaya hiyo, na kuagiza kuainishwa idadi ya vikao
vilivyofanyika kupitia ngazi za shina na Matawi, kwa kigezo kuwa ndiko iliko nguvu
ya Chama hicho.
"Nimevutiwa
sana jinsi mlivyoweka muhtasari wa utekelezaji wa Ilani............nimeridhika
vipi mnavyoshirikiana kati ya viongozi wa Serikali na wale wa Chama",
alisema.
Akigusia
tatizo la uhaba wa ardhi linalokikabili Kiwanda cha Sukari Mahonda, Dk. Shein
alisema Serikali imekipatia kiwanda hicho eneo la ardhi huko Kichwele ili
kuendelea na uzalishaji wa miwa, baada ya eneo lake kuvamiwa an wananachi kwa
shughuli za kilimo.
Alisema
pamoja na hatua hiyo, bado Menejmeneti ya kiwanda hicho inadai eka 3,000 ambazo
zilichukuliwa na wananchi.
Dk.
Shein aliwataka wazee wa Wilaya hiyo kufahamu sababu hasa zilizopelekea Serikali kutoa eneo hilo
la Kichwele kwa Mwekezaji huyo.
Akigusia
suala la uimarishaji wa maji safi na salama katika Wilaya hiyo, Dk. Shein
alipongeza juhudi zilizochukuliwa na Uongozi wa Wilaya hiyo hadi huduma hiyo
kupatikana kwa asilimia 70, na kutaka juhudi zaidi zifanyike kuongeza
upatikanaji wa huduma hiyo ili zifikie asilimia mia moja, kabla ya mwaka 2020.
Alisema
tatizo la upatikanaji wa maji katika maeneo mbali mbali ya Wilaya hiyo, ikiwemo
Misufini na Bumbwini itaimarika pale visima vilivyochimbwa kwa ufadhili wa
Serikali ya Ras el Hemma vitakapounganishwa.
Aidha,
Dk. Shein alisema tatizo la Barabara za Matetema hadi Kazole, Mangapwani na
Zingwezingwe zitashughulikiwa katika kipindi hiki, mara baada ya vifaa vya
ujenzi vilivyoagizwa na Serikali kuwasili baadae mwaka huu.
Kuhusiana
na changamoto ya elimu katika Wilaya hiyo na Mkoa wa Kaskazini kwa ujumla, Dk.
Shein aliutaka uongozi wa Mkoa huo na
Wilaya kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kuona mikakati ipi ifanyike kuimarisha kiwango cha
elimu na ufaulu kwa wanafunzi wa mkoa huo.
Aidha,
aliipongeza Wilaya hiyo kwa makusanyo bora ya mapato na kuvuka kiwango
kilichowekwa kwa zaidi ya asilimia mia 200.
Dk.
Shein Shein ambae pia ni Mkaamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, alisema CCM imebeba
dhima kubwa ya kuwatumikia wananchi, akibai isha kazi hiyo kuanza kufanyika
vizuri, huku akiwaonya baadhi ya
viongozi Wilaya hiyo kwa kutofanya
vizuri.
Dk.
Shein aliwataka viongozi ambao kwa namna moja au nyengine bado hawajetekeleza
ahadi walizotowa kwa wananchi wakati wa kampeni kutumia kipindi kilichobaki
kukamilisha ahadi zao.
Vile
vile akasisitiza dhana ya kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya chama hicho,
mbali na kuwepo kwa Demokrasia katika utoaji wa maoni.
Mapema,
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk. Juma Abdalla Sadala, alizipongeza Kamatiza
Siasa katika ngazi mbali mbali Wilayani humo kwa kuwafikia wanachama walio
chini na kushajihisha uingizaji wa wanachama wapya.
Hata
hivyo,alisema juhudi za kufanya vikao kupitia ngazi za mashina na matawi
zinahitajika, hususan wakati huu kuelekea uchaguzi mkuu ujao wa 2020.
Aidha, alisema bado kuna changamoto kwa baadhi ya
viongozi wa Majimbo (wabunge na Wawakilishi) Wilayani humo, kushindwa
kutekeleza kikamilifu ahadi walizoweka wakati wa kampeni za uchaguzi.
Dk.
Juma alisema suala la mazingira nalo ni changamoto nyengine inayoikabili Wilaya
hiyo.
Nae,
Mkuu wa Wilaya Kaskazini 'B' Unguja, Rajab Ali Rajab alisema Uongozi wa Wilaya
kwa kushirikiana na kamati ya Ulinzi na Usalama imefanya juhudi ya kuimarisha
ulinzi ili kutoa fursa kwa wananchi kutekeleza ipasavyo shughuli zao kiuchumi.
Alisema
Wilaya hiyo imeimarisha huduma za kijamii kwa kuwapatia wazee 729 shilingi
5,000 kila mmoja kwa kila mwezi, sambamba na kusimamia upatikanaji wa pensheni
jamii, ambapo wazee 1940 wamenufaika.
Aidha,
alisema kutokana na juhudi za Uongozi wa Wilaya hiyo wananchi wamepata mwamko
wa kukabiliana na vitendo vya
udhalilishaji, hivyo kiwango cha uhalifu huo kushuka na kubainisha kuwa katika
mwaka 2018 kesi 65 ziliripotiwa, wakati ambapo hadi hivi sasa ni kesi 7 pekee
zilizoripotiwa.
Vile
vile Mkuu huyo wa Wilaya, alisema kutokana na juhudi zilizochukuliwa,
ukusanyaji wa mapato kupitia Halmashauri umeongezeka na kuvuka malengo ya
Serikali, akibainisha katika mwaka wa fedha wa 2017/2018 shilingi Bilioni 1.2
zilikusanywa, wakati ambapo katika mwaka wa fedha wa 2018/19 , hadi kufikia
sasa zaidi ya shilingi Milioni 711 zimeshakusanywa.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment