Habari za Punde

Rest In Peace Ephraim Kibonde, *Alikuwa akitokea Bukoba Kwenye Maziko ya Ruge Mutahaba

Rest In Peace Ephraim Kibonde,


Na Said Mwishehe, Michuzi TV

PIGO jingine Clouds Media Group! Ndivyo unavyoweza kuzungumzia taarifa za kufariki Dunia kwa Mtangazaji wake maarufu Ephraim Kibonde.

Kwa mujibu wa taarifa za Uongozi wa Clouds Media Group kupitia kwa Sebastian Maganga ambazo wamezitoa mapema hii zinasema Kibonde amefarikia dunia leo asubuhi ya Machi 7,2019. Amesema taarifa nyingine kuhusu kifo cha Kibonde zitaendelea kutolewa ili kuufahamisha umma. 

Awali Mkuu wa Mwanza John Mongela alikuwa wa kwanza kutoa taarifa za kufariki kwa Kibonde ambapo amesema kifo chake kimetokana na kusumbuliwa na shinikizo la damu ambalo lilianza tangu akiwa mkoano Kagera.

"Ephraim Kibonde amefariki akiwa hapa mkoani Mwanza ambako alikuwa anasumbuliwa na presha tangu akiwa kwenye shughuli za mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Ruge Mutahaba," amesema Mongella.

Kibonde alikuwa miongoni kwa wafanyakazi wa Clouds Media walioambatana na waombolezaji wengine kwenda kumpumzisha kwenye nyumba yake ya milele aliyekuwa Mkurugezi wa Vipindi na Uzalishaji Ruge Mutahaba ambaye alifariki Dunia Februari 26 mwaka huu nchini Afrika Kusini.

Michuzi Media Group, ambayo ilipata kufanya mahojiano ya mwisho na marehemu Kibonde wakati wa msiba wa Ruge kupitia Michuzi TV,  inaungana na Watanzania wengine kutoa pole kwa familia ya marehemu Ephraim Kibonde,wafanyakazi wa Clouds Media Group,ndugu,jamaa na marafiki.
Bwana Ametoa,
 na Bwana Ametwaa.
Jina lake na lihimidiwe
AMINA

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.