NA ABDI
SULEIMAN, PEMBA.
BENK Kuu ya
Tanzania (BOT) imesema kuwa inakusudia kupeleka sheria bungeni, ili kuweza
kuwekea thamani zaidi fedha ya Tanzania, ambayo kwa sasa imekuwa ikitumiwa
vibaya katika mashuhuli.
Akifungua mkutano wasiku moja uliowashirikisha
masheha, madiwani na kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kaskazini Pemba, Afisa
Mdhamini Wizara ya Fedha na Mipango Pemba, Ibrahim Sale Juma alisema sheria
hiyo itaweza kumbana mtu yoyote atakaeweza kuitumia vibaya fedha hiyo.
Alisema Mtindo wa fedha kutumika katika maholi ya
sherehe kama mapambo, mavazi mwilini, kuzikanyaga chini ni uvunjifu wa sheria,
kwani sheria zipo na zinaongoza na kuelekeza namna gani ya kuzitumia fedha
hizo.
“Kumekuwa na mtindo siku hizi wananchi kuzitumia
wanavyotaka fedha zetu, sasa sheria ikipita basi mtu asije akaona anaonewa pale
itakapomtia hatiani, asije akasema ameonewa lengo ni kuiwekea ulinzi zaidi na
heshima fedha yetu ambayo ni tunu pekee ya Taifa”alisema.
Mdhamini Ibrahim alisema BOT haijatoa ruhusa ya
fedha, kuzitumia kama kuzivaa mwilini au kuzikanyaga au kutengeneza shati na koti,
kwani kufanya hivyo ni kuivunjia hadhi na heshma fedha ya taifa.
Aidha alisema kuwa fedha inavyotumika vibaya
hupelekea uharibifu wa kutokutumika tena fedha hizo, kuingia sokoni na kuweza
kuingia katika mzunguruko wa fedha na kupelekea, kuitia hasara BOT katika
kuchapisha fedha nyengine mpya.
“Elimu hii ya matumizi na umuhimu wa kuitunza fedha
zetu ni jambo zuri kupatiwa, tunaishukuru SMT na SMZ kwa maamuzi yake na leo
tunapewa elimu, jumuku letu sasa kuitunza na kuilinda fedha yetu”alieleza.
Aidha aliwataka wananchi kuhakikisha wanazilinda na
kuzitunza fedha hizo, masheha ndio wenye wananchi aliwataka kuhakikisha, wanatoa elimu kwa wananchi wao pale wanapowapa
vibali vya kufanya sherehe juu ya matumizi ya fedha.
Meneja msaidizi idara ya mawasiliano kwa umma kutoka
BOT, Victoria Msima alisema bot inajukumu la kutekeleza sera ya fedha na kusimamia
masoko yote ya fedha nchini na taasisi za kifedha, ikiwemo kuchapisha na
kusambaza fedha.
Alisema haipendezi kuona wananchi wanazitumia fedha
vibaya, kwa kuzitengenezea mapambo, nguo, kuzikanyaga chini, kufanya hivyo ni
kuishushia hadhi fedha ya taifa.
“Fedha ni tunu ya taifa kama ilivyo bendera ya nchi,
huwezi kuifanya vyovyote na kuitumia vibaya bendera ni kosa la jinai sawa sawa
na fedha, wajibu wetu kuwa makini katika matumizi ya fedha zetu”alisema.
Aidha aliwataka wananchi kuhakikisha wanazitunza
noti za
Taifa, kwani BOT sasa imeanza kufuatilia matumizi yote ya fedha,
ikiwemo wanaozitumia vibaya ili kuwatia hatiani na kuwa fundisho kwa wengine.
Akiwasilisha mada ya sarafu afisa kutoka BOT
Restituta Magnus, alisema benk inafanya kazi kubwa ya kusambaza fedha zote, kwa
kushirikiana na benk za biashara zilizopo nchini.
Alisema tayari elimu ya matumizi ya fedha hizo na
ugunduzi wa fedha ambazo sio halali, tayari imeshatolewa kwa wananchi wote
wakiwemo makundi maalumu ya watu wenye ulemavu.
Wakichangia katika kikao hicho Zulfa Abdalla Said,
alisema wanawake wa mkoa wakaskazini Pemba wanalaani Vikali kitendo
kilichofanywa na wanawake wenzao, kuzitumia fedha kama mapambo katika shuhuli
mbali mbali.
Alisema wakati umefika kwa viongozi wakamati ya
Ulinzi na usalama Zanzibar, kufanya uchunguzi juu ya tukio lililotokea na
kuenea katika mitandao ya kijamii, kutumika fedha kama nguo na muhusika
kumchukulia hatua za kisheria, ili kuwa fundisho kwa wengine, kwa lengo la
kuiwekea heshima fedha ya Tanzania.
Sheha wa selimu Ali Khatib Chwaya, aliitaka BOT
kuandaa sheria kali kwa wale wote watakaobainika kuitumia vyeba fedha ya taifa
na kuweza kuwatia hatiani, pale watakapobainika kwani fedha ndio alama tosha
kwa taifa lolote duniani.
No comments:
Post a Comment