Habari za Punde

AWAMU YA KWANZA YA UHAKIKI WA JUMUIYA ZA KIJAMII NA TAASISI ZA KIDINI WAANZA JIJINI DAR ES SALAAM.

Kaimu Msajili wa Jumuiya za Kijamii na Taasisi za Kidini kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Jesca Shengena akitoa maelekezo kwa Makamu Mwenyekiti wa Kanisa la Mungu Mfalme, Makange Kitua (kushoto), wakati wa zoezi la Uhakiki  wa  Jumuiya  za  Kijamii na Taasisi za Kidini linaloendelea katika Ofisi Ndogo ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam
Afisa  wa  Kitengo  cha  Jumuiya  za  Kijamii  na  Taasisi  za  Kidini kutoka Wizara  ya  Mambo  ya  Ndani ya Nchi, Neema Ngalawa akihakiki taarifa za Taasisi ya Kidini ya Peaceful Life Ministries wakati wa zoezi hilo linaloendelea Ofisi  Ndogo  ya  wizara  hiyo  jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mchungaji Msaidizi  wa  Kanisa hilo, Paskazia Makofi.
Makamu Mwenyekiti wa Kanisa la Mungu Mfalme, Makange Kitua akitoa maelezo ya  taasisi  yake  kwa  Afisa wa Kitengo cha Jumuiya za Kijamii na Taasisi za Kidini kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Neema Ngalawa (kulia),  wakati  wa  zoezi la uhakiki linalofanyika Ofisi Ndogo ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam
Afisa  wa  Kitengo  cha  Jumuiya  za  Kijamii  na  Taasisi  za  Kidini kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Thomas Sanira akimsikiliza  Katibu Mtendaji  wa  Jumuiya  ya  Istiqama, Issa  Suleiman(kulia), wakati wa zoezi la uhakiki wa taasisi hizo linaloendelea Ofisi Ndogo ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.