Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mama Janeth Magufuli,
akimkabidhi mmoja wa wawakilishi msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini
Dar es salaam jana Jumatano Mei 22, 2019(Picha na Ikulu)
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.Mama
Janeth Magufuli, akiongea machache wakati wa hafla ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini
Dar es salaam
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.Mama Janeth Magufuli, akimsiliza Katibu Mkuuwa BAKWATA
Sheikh.Nuhu Muma akitoa shukurani wakati wa kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini
Dar es salaam
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi Katibu Mkuu wa BAKWATA Sheikh.Nuhu Muma msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini
Dar es salaam
Mke
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli,
akimkabidhi Mkurugenzi wa Hija wa BAKWATA
Sheikh Haidary Kambwile msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhita jijijini
Dar es salaam
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mama Janeth Magufuli akiwa katika picha ya kumbukumbu na Katibu Mkuu wa
BAKWATA Sheikh. Nuhu Mruma, Mkurugenzi wa Hijja wa BAKWATA
Sheikh.Haidary Kambwile pamoja na wawakilishi wa vikundi mbalimbali vya wenye uhitaji baada ya hafla ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji.
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli, amewasihi Waislamu nchini kuendelea kuliombea Taifa muda wote, hususan katika kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, na kuendeleza mshikamano bila kujali dini ama kabila tabaka zao.
Mama
Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 22 Mei, 2019 Jijini Dar es Salaam
wakati akitoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji.
Vyakula alivyotoa ni tani 5 za mchele,
tani 3 za sukari na tende. Hafla hiyo imehudhuriwa na Katibu Mkuu wa BAKWATA Sheikh Nuhu Mruma,
Mkurugenzi wa Hijja wa BAKWATA
Sheikh.Haidary Kambwile na wawakilishi wa vikundi mbalimbali vya wenye uhitaji.
Mama
Magufuli pia amemuomba Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema, azikubali funga za Waislamu wote na kuwalipa malipo stahiki wakati wa kitekeleza moja ya nguzo muhimu za Dini ya Kiislamu.
“Kipindi cha
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni kipindi cha toba. Ni kipindi cha
kutenda matendo mema na kujizuia na vitendo viovu” amesema Mama Magufuli.
Mama Magufuli amesema licha ya kwamba
Tanzania ina watu waimani za Dini tofauti lakini siku zote wananchi wake
wamekuwa wakishirikiana nyakati za dhiki na za raha bila ubaguzi.
Ametoa mfano kuwa licha ya tofauti za kidini zipo baadhi ya familia ambazo
Baba Muislamu na Mama ni Mkristo zinaishi kwa amani na kushirikiana katika masuala yote ya kifamilia na kwamba sifa hii ni moja nguzo muhimu za umoja wa Watanzania.
“Binafsi na kumbuka zamani nikiwa mdogo tulikuwa tunatafuta Mwislamu aje atuchinjie
kuku ama mbuzi ama ng’ombe” ,alisema na kuongezea:
“Ni
kutokana na utamaduni huo uliojengeka miongoni mwa Watanzania ,
leo nimeguswa kutoa sadaka yangu kwa ajili ya ndugu zangu wenye uhitaji…”
No comments:
Post a Comment