Wazazi, walimu wa Skuli za maandalizi, madrasa na vyuo vya Qur,aan, Masheha na Watu Mashuhuri wakiwa katika Ukumbi wa Skuli ya Maandalizi Madungu
Afisa WEMA Idara ya Maandalizi Msingi na Vyuo vya Qur-an Ukhti Amina Salum Khalifan akizungumza na Wazazi, walimu wa Skuli za maandalizi, madrasa na vyuo vya Qur- an, Masheha na Watu Mashuhur katika Ukumbi wa Skuli ya Maandalizi Madungu.
Mkurugenzi idara ya Maandalizi na Msingi Bi Safia Ali Rijali akizungumza na Wazazi, walimu wa Skuli za maandalizi, madrasa na vyuo vya Qur- an, Masheha na Watu Mashuhuri katika Ukumbi wa Skuli ya Maandalizi Madungu.
NA Ali Othman , Pemba
Mkurugenzi idara ya Maandalizi na Msingi
Bi Safia Ali Rijali amewataka wazazi kuhakikisha kwamba watoto wanaanza elimu
ya maandalizi kwa umri sahihi uliopendekezwa.
Bi Safia ameyasema hayo katika ukumbi wa
Skuli ya Maandalizi Madungu, wakati akizungumza na Wazazi, walimu wa Skuli za
maandalizi, madrasa na vyuo vya Qur- an, Masheha na Watu Mashuhuri kutoka
katika shehia mbali mbali ambazo zimebainika kuandikisha idadi ndogo ya
wanafunzi.
Amesema baada ya kutembelea baadhi ya
shehia hizo amebaini kwamba, wapo wazazi ambao kutokana na sababu mbali mbali
huacha kuwaandikisha watoto wao katika elimu ya maandalizi licha ya watoto hao
kufikia umri sahihi wakuandikishwa
Aidha, Bi Safia amewataka wazazi kushirikiana
kikamilifu katika malenzi na kutenga
muda wa kukaa na watoto na kuwahimiza kusoma, akiwaasa baadhi ya mababa kuacha tabia ya
kuwaachia wanawake swala la malezi kwa kisingizio cha kutokua na muda.
Akizungumzia swala la afya Bi Safia amewataka wazazi kujali afya za
watoto na kuhakikisha kwamba wanawapatia chakula bora na kuchukua hatua stahiki
dhidi ya ukatili wanaotendewa watoto katika jamii.
Wakati huo huo Afisa WEMA Idara ya
Maandalizi Msingi na Vyuo vya Qur-an Ukhti Amina Salum Khalifan amewataka
Wazazi, walimu wa Skuli za maandalizi, madrasa na vyuo vya Qur- an, Masheha na
Watu Mashuhuri kuhakikisha kwamba wanawasimamia vyema watoto ili wawe raia wema baadae.
Shehia ambazo zimebainika kuandikisha
idadi ndogo ya wanafunzi ni Birikau, Furaha, Kwale, Pembeni, Uwandani, Kilindi
Wilaya ya Chake Chake na Chokocho, Michenzani, Mkanyageni, Shidi, Mtuhaliwa, na
Makoongwe kwa wilaya ya Mkoani.
No comments:
Post a Comment