Habari za Punde

ZIMAMOTO YATOA UFAFANUZI KUHUSU MAFUNZO YA KINGA NA TAHADHARI DHIDI YA MAJANGA YA MOTO KWA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI.


WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Simu ya Maandishi: “ZIMAMOTO KUU”
Simu Nambari:  +255-22-2113537
Nukushi: +255-22-2184569
Tovuti: www.frf.go.tz






JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI
                      Jeshi la Zimamoto na Uokoaji      
       S.L.P.  1509
                                        DODOMA
                                 21 Mei, 2019


                     

 





                                                                                                                              
                                        
TAARIFA KWA UMMA
ADA YA MAFUNZO YA KINGA NA TAHADHARI DHIDI YA MAJANGA YA MOTO KWA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limeundwa na linatekeleza majukumu yake chini ya Sheria ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji namba 14 ya mwaka 2007 (Fire and Rescue Force Act No. 14 of 2007) na Kanuni zake za mwaka 2008. Majukumu makubwa ya Jeshi hili ni kuokoa Maisha na Mali katika majanga mbalimbali.
Sambamba na majukumu hayo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linafanya ukaguzi wa Kinga na Tahadhari dhidi ya majanga ya moto, na kutoa ushauri wa aina na namna ya uwekaji wa vifaa vya kinga na tahadhari. Ukaguzi huu unafanyika kwa mujibu wa sheria namba 14 ya mwaka 2007 ikisomwa pamoja na Kanuni ya Vyeti ya Usalama wa moto ya Mwaka 2008 na marekebisho ya mwaka 2014 (Fire and Rescue Force Safety Inspections and Certificates Regulations of 2008 GN.106 and its Amendment GN 63 of 2014.) pamoja na Kanuni ya Tahadhari dhidi ya moto kwenye majengo ya mwaka 2015 (Fire and Rescue Force Fire Safety Precaution in Building Regulations of 2015 GN 516.) Ukaguzi huu huambatana na tozo kwa mujibu wa sheria na kanuni.
Hivyo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linapaswa kutoa elimu katika sehemu mbalimbali kama vile viwanda, mahoteli, maduka, shule za msingi na sekondari, migodi, vituo vya mafuta n.k. Watumishi wa taasisi husika wanapaswa kulipia gharama za mafunzo (training fee) ambazo ni shilingi 20,000/= kwa kila mshiriki kama ilivyoainishwa katika kanuni za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Mafunzo hayo ya kinga na tahadhari ya majanga ya moto hutolewa bure kwa wanafunzi wa ngazi zote.

Jeshi linatoa rai kwa Wamiliki na Wakuu wa Shule za Kutwa na Bweni ambazo hazijapatiwa mafunzo ya kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto kuwasiliana na Makamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa husika ili waweze kupatiwa elimu hiyo.

Imetolewa na;
Kitengo cha Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Elimu kwa Umma
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji- Makao Makuu.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.