Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia Mkutano Mkuu wa Nne wa Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi Zanzibar, uliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amesema Serikali inatambuwa kuwa kuwepo kwa vyama vya wafanyakazi nchini, kunaendana na sheria na Katiba ya Zanzibar ya 1984 pamoja na mikataba ya kimataifa.
Dk.
Shein amesema hayo katika ufunguzi wa Mkutano mkuu wa nne wa Shirikisho la
Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar (ZATUC), uliofanyika katika Ukumbi wa Sheikh
Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Mjini hapa.
Pamoja
na mambo mengine mkutano huo wa siku mbili umepanga kufanya Uchaguzi mkuu wa
kuwapata Viongozi wapya wataohudumu kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Dk.
Shein alisema Serikali inatambua kuwa wafanyakazi na vyama vya wafanyakazi ni
kundi muhimu Ulimwenguni na ili mafanikio yaweze kupatika kazini, ni
lazima pawepo wafanyakazi walio tayari kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi,
nidhamu, uadilifu na uzalendo katika mazingira bora.
Alisema
kutokana na hali hiyo Serikali imekuwa ikiridhia mikataba mbali mbali ya Kimataifa
pamoja na kutunga sheria na kanuni zinazohusiana na masuala ya wafanyakazi.
“Yote
hayo yanafanywa kwa madhumuni ya kufikia malengo na kuhakikisha wafanyakazi
wanatimiza majukumu yao katika mazingira yalio bora zaidi pamoja na kulinda
maslahi yao ”, alisema.
Alisema
Serikali imekuwa na mazingatio maalum juu ya wafanyakazi kwa kutambuwa kuwa
wanahusiana moja kwa moja na ukuaji wa uchumi, ukiwa ndio msingi wa ustawi wa
maisha ya wananchi.
Dk.
Shein alisema Serikali inazingatia umuhimu wa kuimarisha ushirikiano uliopo na Vyama vya
wafanyakazi kupitia ZATUC, ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka
2015-2020, Ibara ya 139.
Aidha,
Dk. Shein aliipongeza Jumuiya ya Waajiri Zanzibar (ZANEMA) kwa kuwa na
ushirikiano mkubwa na Serikali, hivyo kurahisisha ushughulikiaji wa changamoto
mbali mbali zinazowakabili wafanyakazi.
“Nikupongezeni
viongozi nyote wa Shirikisho mnaomaliza muda wenu wa uongozi, hakika sote
tunathamini kazi yenu kubwa na nzuri mliyoifanya katika kulitumikia Shirikisho
hili muhimu katika kipindi chote”, alisema.
Akigusia
Historia ya Vyama vya Wafanyakazi nchini, Dk. Shein alisema kuwa ilipitia
katika hatua mbali mbali, ambapo vyama hivyo vilitowa mchango mkubwa kwa
wananchi katika harakati za kupigania uhuru, kupinga ubaguzi na unyonyaji dhidi
ya wanyonge.
Akitowa
mfano, alisema kuundwa kwa chama cha ‘Zanzibar and Pemba Federation of Labour’
kulichangia sana kuwaunganisha wafanyakazi, kuhamasisha kazi za ujenzi wa taifa
na kupigania ustawi bora wa maisha ya wananchi, baada ya Mapinduzi ya Zanzibar
ya 1964.
Alisema
mnamo mwaka 1952 hadi 1957 Hayati Mzee Abeid Amani Karume alikuwa Mwenyekiti wa
Chama cha Mabaharia Zanzibar (Zanzibar Seamen Union), ambapo alishirikiana an
viongozi wa vyama vyengine katika kudai haki na kuondoa madhila.
Akizungumzia
kuhusiana na uchaguzi wa viongozi wakuu wa Shirikisho hilo, Dk. Shein alisema
ni haki kwa wajumbe wenye sifa kushiriki kwa uwazi pamoja na kuwachaguwa
wagombea waliojitokeza baada ya kujiridhisha kuwa wana sifa na uwezo wa kuwatumikia
wafanyakazi.
“Napenda
nisema kuwa si kila mtu anaweza kuwa kiongozi, kiongozi anatakiwa awe na sifa
maalum, hususan za uadilifu na aliye tayari kuwatumikia wengine, hivyo ni vyema
mkachaguwa viongozi bora na wenye uwezo”, alisema.
Aidha,
alisistiza kwa kuwataka wajumbe kutokufanya makosa ya kuwachaguwa vongozi walioweka
mbele maslahi yao binafsi au wenye kutafuta uongozi kwa njia za hadaa, kwani
hatua hiyo inaweza kuwagharimu wafanyakazi.
Aliwataka
kuchaguwa viongozi watakaokuwa kioo cha shirikisho , akibainisha kuwa viongozi hao ni wale wanaojitambuwa na kuwa mfano bora wa
utendaji wa majukumu, kauli zao na waliojipamba kwa maadili mema.
“Wanaohitaji
kuongoza ni lazima watambuwe kuwa wanabeba dhamana ya kuwatumikia wafanyakazi
na wajibu wa kuongoza ni kuonyesha njia na kuyafikia malengo, lakini pia ni vyema wakaelewa jukumu
walilonalo la kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazowakabili wafanyakazi”,
alisema .
Akinasibisha
na kauli yake, Dk. Shein alisema ZATUC inahitaji kuwa an viongozi wenye ushawishi
katika kuwaongoza wafanyakazi kuelekea kwenye mafanikio pamoja na kuzingatia
maslahi yao.
Aidha,
aliwataka wajumbe watakaochaguliwa
kushika nyadhifa mbali mbali kutumia hazina kubwa ya uzoefu kutoka kwa viongozi
waliotangulia pamoja na kupata ujuzi na ushauri kutoka kwao.
Alisema
kuna umuhimu kwa wajumbe kuendeleza
umoja na mshikamano uliopo kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi,
akitahadharisha kuwa sio jambo jema kuibuka makundi kati ya wagombea
walioshinda na wale walioshindwa.
Aliwahakikishia
wajumbe hao kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na viongozi wapya
watakaochaguliwa ili kuendeleza mafanikio yaliofikiwa na kufikia malengo ya
kuanzishwa kwa Shirikisho hilo.
Nae,
Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto Moudline Castico, alisema
serikali itaendelea kuwashughulikia kisheria Waajiri wasiofuata sheria na
miongozo ya Serikali katika kuwapatia stahiki za wafayakazi wao.
Aliwataka
wajumbe wanawake kujitokeza na kugombea nafasi mbali mbali za Uongozi wa
shirikisho hilo ili kuendeleza mafanikio yaliofikiwa.
Mapema,
Katibu Mkuu wa ZATUC Khamis Mwinyi Mohamed aliipongeza Serikali kwa kukubali
uanzishaji wa sheria mbali mbali zinazohusiana na wafanyakazi nchini.
Aliipongeza
Serikali kwa kuviwezesha vyama vya wafanyakazi kufanya shughuli zake bila
bughudha sambamba na hatua yake ya kuto nyongeza za mishahara kila baada ya
kipindi, sambamba na mishahara hiyo kupatikana kwa wakati.
Alisema
katika kipindi hicho (miaka mitano iliyopita), ZATUC kwa kushirikiana an
Serikali imekuwa na mchango mkubwa katika ukuaji na ustawi wa uchumi wa
Zanzibar.
Aidha,
aliipongeza Serikali kwa kuridhia mikataba mbali mbali ya Kimatifa pamoja na
mikakati mbali mbali ya vipaumbele na kiufundi vya Shirika la Kazi Duniani
(ILO).
Katika
hatua nyengine, akitowa salam kutoka Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi
Tanzania (TUCTA), Dk. Yahya Msigwa aliipongeza ZATUC kwa kuendeleza uhusiana na
ushirikiano na TUCTA hivyo kupanuwa wigo wa mafanikio ya wafanyaakzi nchini.
Abdi
Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment