Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya
Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akizungumza jambo wakati wa kikao
chake na Balozi wa Jamhuri ya Korea Nchini, Tae-ick Cho (katikati) wakati wa
mazungumzo yao yaliyofanyika leo (Ijumaa Julai 5, 2019) katika Ofisi za NBS Jijini
Dar es Salaam. Kulia ni Mtaalamu wa Utafiti wa Ubalozi wa Korea, Hae-ju Yong
Balozi wa Jamhuri ya Korea,
Tae-ick Cho akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi
ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa yaliyofanyika leo Ijumaa Julai 5,
2019 katika Ofisi za NBS Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja Takwimu za
Kilimo wa NBS, Titus Mwisummba na Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa NBS, Bw.
Daniel Masolwa.
Balozi wa Jamhuri ya Korea,
Tae-ick Cho akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi
ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa yaliyofanyika leo Ijumaa Julai 5,
2019 katika Ofisi za NBS Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja Takwimu za
Kilimo wa NBS, Titus Mwisummba na Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa NBS, Bw.
Daniel Masolwa.
Balozi wa Jamhuri ya Korea, Tae-ick
Cho akimwonesha nakala ya jarida Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu,
Dkt. Albina Chuwa kuhusu miradi
mbalimbali ya Maendeleo inayotekelzwa na Serikali ya Nchi hiyo Tanzania.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa NBS, Bw. Daniel Masolwa. Mkutamo
baina ya Balozi huyo na NBS ulifanyika leo Ijumaa (Julai 5, 2019) katika Ofisi
za NBS Jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Jamhuri ya Korea,
Tae-ick Cho (kushoto) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya
Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa (katikati) na baadhi ya watendaji wa
NBS akiwemo Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi- Daniel Masolwa kulia, mara baada
ya kumalizika kwa kikao baina yao leo (Ijumaa Julai 5, 2019) katika Ofisi za
NBS Jijini Dar es Salaam.
(PICHA
NA MAELEZO)
Na
Mwandishi Wetu, Maelezo Dar es Salaam,5.
JULAI, 2019
BALOZI
wa Jamhuri ya Korea, Tae-ick Cho amesema Serikali ya Nchi hiyo itaendelea
kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takiwmu (NBS) kwa ajili ya kuimarisha
miundombinu yake ikiwemo mifumo ya Tekonojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na
kumalizia Ujenzi wa Ofisi za NBS katika Mikoa ya Dodoma na Kigoma.
Akizungumza
na Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dkt. Albina Chuwa leo Ijumaa (Julai 5, 2019) Jijini
Dar es Salaam, Balozi Cho amesema Serikali yake ipo tayari kutoa ushirikiano
unaohitajika katika kuhakikisha kuwa NBS inatekeleza majukumu yake.
Balozi
Cho alisema Serikali ya Jamhuri ya Korea inatambua umuhimu wa takwimu katika
shughuli za kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Nchi
zinazoendelea ikiwemo Tanzania, hivyo itahakikisha kuwa mahitaji yote ya msingi
kwa yanayohitajika na NBS ikiwemo uimarishaji wa miundmbinu ya TEHAMA inapewa
kipaumbele.
Mwezi
Juni mwaka 2018, tulianza mazungumzo ya ushirikiano na NBS kupitia Wizara ya
Fedha na Mipango, hivyo utekelezaji wa masuala yote ya msingi katika mazungumzo
hayo yapo katika hatua nzuri na nitawasiliana na Serikali yetu ili kuona jinsi
ya kusukuma jambo hili kwa haraka zaidi.
Aidha
Balozi Cho aliongeza kuwa Serikali ya Korea itahakikisha kuwa makubaliano hayo
yanaanza kutekelezwa kwa haraka kwa kuwa inatambua ukubwa na umuhimu wa majukumu
ya NBS katika uzalishaji na upatikanaji wa takwimu kwa ajili ya kuharakisha
shughuli za Maendeleo ya wananchi.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dkt. Albina Chuwa alisema NBS kupitia
Wizara ya Fedha na Mipango tayari ilianza hatua za awali za makubaliano ya
ushirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Korea na hivyo kupitia sheria ya misaada
ambapo wameahidi kujenga na kuimarisha miundombinu ya Ofisi za NBS zilizopo
katika Mikoa ya Kigoma na Dodoma.
“Katika
Mkoa wa Kigoma wameahidi kujenga Ofisi hiyo na kusimika miundombinu ya TEHAMA
wakati katika Mkoa wa Dodoma wameahidi kuweka miundombinu ya TEHAMA katika
Jengo la Ofisi zetu za Dodoma” alisema Chuwa.
No comments:
Post a Comment