Na.Laila Abeid -Maelezo.
Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka sheria, taratibu na miongozo ambayo
inashirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali kuhakikisha usalama na ustawi
wa watoto nchini Tanzania.
Hata
hivyo, pamoja na yote hayo bado ukatili dhidi ya watoto umeendelea kushamiri
pamoja na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria. Hii inatupa picha kwamba bado
kunahitajika mkakati madhubuti wa kuhakikisha sheria zinazowekwa zinapunguza
masuala ya ukatili kwa watoto kama sio kwisha kabisa.
Serikali
na wadau wanaitakia nchi yetu mafanikio wafungue macho dhidi ya ukatili huu
kwani watoto wengi wanakutwa na majanga ya kubakwa na kulawitiwa wawapo njiani wanapoelekea shuleni ,
wanapocheza na wenzao au wanapoelekea dukani kufata mahitaji wanayoagizwa na
wazazi wao
Kwa
bahati mbaya sana wahusika wengi wanaowafanyia watoto ukatili ni sehemu ya
familia ya watoto husika. Mara nyingi unakuta ni aidha, wazazi, baba wadogo ,
wajomba, mama wa kambo, jirani, rafiki wa familia na jamii ya karibu na
anapoishi mtoto.
Baba
wa kambo mkazi wa buguruni amlawiti mtoto wa umri wa miaka 4 , Baada ya
kuachiwa na mkewe amuamshe iliaweze kumuandaa kwenda shule na muhusika
alikamatwa baaada ya mtoto kusema
kitendo anachofanyiwa na baba huyo, baadae muhusika alipewa dhamana na kutoka
kwa dhamana.
Aidha
kutokana na jamii kutokuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu sheria na taratibu za
kufuata mara baada ya mtoto kufanyiwa ukatili wa aina yeyote ile. Suala la
utamaduni au desturi na mila ya kuamua kumaliza kimyakimya masuala hayo ya ukatili kwa kisingizio cha kulinda
heshima ya mkosaji na kumlindia hadhi
katika jamii ndio chanzo cha kuongezeka kwa masuala hayo.
Changamoto
hizi zinawafanya wazazi kushindwa kuwatoa watoto wao kwenye mambo tofauti ya
kijamii kutokana na kuogopa kutokea kwa matatizo kama hayo. Aidha kesi
zikipelekwa katika sehemu husika, wenye ushahidi kutokwenda mahakamani au mara
nyingine mhusika kutoroka na baadae kesi
hufutwa bila kujua hatma ya mtoto aliyepata madhara.
Mpaka
sasa kuna idadi kubwa ya watoto waliobakwa na kulawitiwa ambapo mwaka 2015/2016
watoto aliobakwa na kulawitiwa walikuwa 394 na mwaka 2016/2017 kufikia 2,984 ,Tafiti zinaonyesha idadi ya
watoto waliobakwa itazidi kuongezeka kwa mwaka 2018 na 2019 na kuwa kubwa zaidi.
Suala
hili sio la Serikali peke yake ushirikiano unahitajika kutoka kwa jamii yote
kwa ujumla ili kushiriki katika kutokomeza uhalifu huu ambao unatupelekea kuwa
na Taifa lisilofaa hapo baadaye. Pia,
nguvu za ziada zinahitajika kuhakikisha watoto wanaokumbwa na majanga haya kusaidiwa
kisaikolojia ili kurudi katika hali yao ya kawaida itakayowafanya kuwa Rais
wema na wazazi hapo baadaye.
Mmoja
wa wazazi wa mtoto aliye fanyiwa ukatili wa kijinsia mkazi wa singida
alisema hatutakiwi kuwa na imani juu ya watu ambao wanatuzunguka kwani
wengi wanatufanyia mambo haya ni miongoni mwa hawa tunaoishi nao na hii
hutokana na matamanio yao ya kimwili.
Jamii
kwa ujumla inatakiwa iwemacho kupinga vikali ukatili huu unaowakumba
watoto wadogo kwani wao ndio taifa la
kesho na ndio tegemeo kubwa la taifa kwa mwaka ujao hivyo tunapofumbia macho
matukio kama haya na kutokukaa kimya
pale tunapogundua kama mtoto amefanyiwa ukatili basi lazima tuchukue hatua ya
kupeleka mashtaka ya kitendo hicho mbele ya sheria .
“Tunatakiwa
tufungue macho juu ya haya matukio yanayowakuta watoto wetu na pia tuwe makini
na jamii inayotuzunguka kwa ujumla kwani wengi wao ndio wanaohusika na vitendo
hivi kwa watoto na badae kutoka hivyo serikali tunaiomba iwe macho juu ya matukio kama haya “.
Mapendekezo
yangu kama raia mwema wa Tanzania viongozi mbalimbali wakiwemo wa dini na
viongozi wa serikali wanajitahidi kupiga vita juu ya ukatili wa namna hii kwa
jamii lakini hali bado ni tete kwani watuhumiwa wengi wa matukio haya wamekuwa
hawajui wala kuelewa juu ya vita vinavyoendelea dhidi ya ukatili kwa watoto .
Ushauri
wangu Sheria zitakazotungwa ziwe kali kwa kuweka amani na utulivu, pia serikali
ingetoa elimu juu ya matukio ya ulawiti na hasara zake kwa jamii pia kuwajulisha
juu ya sheria zinazotumika kuwaadhibu watendaji wa matukio ya ulawiti na
ubakaji ili kuweza kupunguza utokeaji wa matukio kama haya kwa asilimia kubwa .
Jamii
ikiwa macho dhidi ya matukio haya basi watoto wengi watakuwa salama dhidi ya
matukio ya ukatili pia kuwapeleka wahusika wa matukio haya polisi ili sheria
ifate mkondo wake basi yaweza pelekea nchi ikawa huru na amani .
05. Julai 2019
No comments:
Post a Comment