Habari za Punde

Mboriborini Yaibuka Kidedea Kombe la Ndondo Cup.

Na.Mwanajuma Juma.
TIMU ya soka ya Mboriborini imetwaa ubingwa wa bahari fm ndondo Cup kwa kuifunga pwani mchangani mabao 3-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa Amaan.

Fainali hiyo ya aina yake imechezwa saa 10:00 za jioni na kuhudhuriwa na mashabiki wengi waliovutia uwanja mzima.

Katika mchezo huo ambao mgeni rasmi alikuwa ni Naibu Katibu mkuu uvccm Zanzibar Mussa Haji Mussa Mboriborini   mabao yake yote hayo yalifungwa na Said Etoo.

Mshindi wa kwanza wa michuano hiyo aliondoka na shilingi milioni tatu, Kombe jezi na mpira, wa pili  alipata shilingi  milioni moja na nusu, jezi na mpira na mshindi wa tatu aliondoka na kitita Cha shilingi milioni moja na mpira.

Aidha zawadi ya Kipa Bora ilikwenda Sheha Kirara kutoka timu ya Pwani Mchangani , mchezaji Bora  Ridhwani Mohammed wa Mboriborini na mfungaji Bora ni  maulid wa Chaani Masingini kashinda  magoli sita.

Kwa upande wa zawadi ya Timu yenye nidhamu ilikwenda Six Center ya Mwera .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.