Habari za Punde

Mke wa Rais wa Tanzania Mama Janeth Magufuli Awatembeleza wa Marais Kijiji cha Makumbusho na Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam.

Mtoto wa Baba wa Taifa Madaraka Godfrey Nyerere akionesha cherehani ambayo Mwalimu Julius Nyerere alikuwa akiitumia kushonea nguo za familia yake kwa Mke wa Rais Mama Janeth Maguful,  Mke wa Rais wa Comorro Mama Assoumani  Mke wa Waziri Mkuu wa Eswatini Mama Dlamini, mke wa Rais wa Namibia Mama Mama Monica Geingos na Mke wa Rais wa Afrika Kusini Dkt. Tshepo Motsepe   wakati Mama Magufuli alipowatembeza wake hao wa viongozi wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC kujionea vitu mbalimbali katika  Makumbusho ya Taifa na Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 17, 2019
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiongozana na mke wa Rais wa Namibia Mama Monica Geingos (kushoto) Mke wa Rais wa Afrika Kusini Dkt. Tshepo Motsepe(wa pili kulia) na Mke wa Waziri Mkuu wa Eswatini Mama Dlamini  (kulia) wakati alipowatembeza wake hao wa viongozi wakuu wa Jumuiya ya endeleo ya Kusini mwa Afrika SADC kujione nyumba za kiasili kwenye Kijiji cha Makumbusho Kijitonyama jijini Dar es salaam leo
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa katika picha ya kumbukumbu mbele ya nyumba ya kiasili na Mke wa Rais wa Comorro Mama Assoumani  Mke wa Waziri Mkuu wa Eswatini  Mama Dlamini mke wa Rais wa Namibia Mama Moca Geingos na Mke wa Rais wa Afrika Kusini Dkt. Tshepo Motsepe   wakati alipowatembeza wake hao wa viongozi wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC kujione nyumba za kiasili kwenye Kijiji cha Makumbusho Kijitonyama jijini Dar es salaam leo Jumamosi.
Picha na Ikulu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.