RAIS wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein,
akizungumza na Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi zake Zanzibar.Mhe. Xie
Xiuowu, akiwa na Katibu wa Kamati Kuu ya Chama Cha Kikomunisti na” Vice General
Manager of China National Research Institute of Food Fermentation Industries
Co.Ltd “ Bw. Dong Weihong, walipofika Ikulu kwa mazungumzo leo.
JAMHURI ya Watu wa China imepongezwa kwa kuendeleza utamaduni
wake wa kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta za maendeleo kwa kuleta
wataalamu kutoka nchini humo kuja kutoa mafunzo hapa Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ametoa pongezi hizo leo Ikulu mjini Zanzibar wakati
alipofanya mazungumzo na Katibu wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha
China (CPC) Dong Weihong ambaye pia ni Makamo Mkuu wa Taasisi ya ‘China
National Research Institute of Food Fermentation Industries’ ya China.
Dk. Shein alieleza
kuwa Jamhuri ya Watu wa China imeanza
kuleta wataalamu wake hapa Zanzibar tokea miaka ya 60 mara baada ya Mapinduzi
matukufu ya Januari 12, 1964 hivyo, ujio wa wataalamu na wakufunzi kutoka nchi
hiyo kuja kutoa mafunzo ya mapishi na
ukarimu yatakayoendeshwa na Taasisi hiyo ni muendelezo wa utamaduni huo.
Katika mazungumzo
hayo, Rais Dk. Shein alisema kuwa Jamhuri ya Watu wa China na Zanzibar zina
historia ya muda mrefu katika kushirikiana kwa azma ya kuwaleta wataalamu na
wakufunzi wake hapa Zanzibar kwani imeshawaleta wataalamu wake hapa Zanzibar
katika sekta mbali mbali zikiwemo afya, kilimo, viwanda, elimu na nyenginezo.
Aidha, Rais Dk. Shein
alieleza kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo Zanzibar ina furahishwa
na juhudi za nchi hiyo za kuendeleza uhusiano na ushirikiano wake katika
kuendeleza na kuimarisha sekta za maendeleo.
Rais Dk. Shein
alieleza kuwa mashirikiano hayo ya pamoja kati ya Taasisi hiyo na Zanzibar
katika kufikia uwamuzi wa kuleta wataalamu wake kwa mara ya tatu hapa Zanzibar
kuja kutoa mafunzo ya mapishi, ukarimu pamoja na huduma nyengine za nyumbani ni
jambo la busara.
Alieleza kuwa juhudi
hizo ni hatua moja wapo za Jamhuri ya Watu wa China kuunga mkono mikakati ya
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuendeleza sekta za maendeleo ikiwemo
sekta ya utalii kwani utaalamu huo wanaoutoa kwa jamii ya kizanzibari pia, ni
kivutio kimoja wapo cha watalii kutoka nchini China na nchi nyenginezo.
Rais Dk. Shein alisisitiza
kuwa juhudi hizo zina manufaa makubwa hivi sasa na hata hapo baadae kwani ni
kivutio kimoja wapo cha kupanua wigo katika masuala mazima ya vmapishi ya vyakula
vya aina mbali mbali.
Rais Dk. Shein
alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza uhusiano na
ushirikiano wake na Jamhuri ya Watu wa China katika kuhakikisha sekta za maendeleo
zinaimarika sambamba na kuimarisha udugu na urafiki uliopo.
“Ni jambo la
kufurahisha sana kwani Jamhuri ya Watu wa China walianza kutusaidia kwa
kutuletea wataalamu wa afya, kilimo, viwanda, elimu lakini leo inatuletea
waatalamu wa mapishi na ukarimu kwa kweli ni jambo la kupongezwa sana”,alisema
Dk. Shein.
Aidha, Rais Dk. Shein
alisema kuwa kufanyika mafunzo hayo hapa Zanzibar kunatoa ahueni na nafuu ya
gharama za uendeshaji na utoaji nafasi kubwa zaidi kwa watendaji watakaopata fursa
ya mafunzo hayo.
Pia, Rais Dk. Shein
alieleza kuwa mafunzo hayo yataimarisha uhusiano na ushirikiano katika
kuimarisha sekta ya elimu na utalii kwa kupitia Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar
kiliopo Maruhubi ambacho hivi sasa kimeunganishwa na Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
(SUZA).
Mapema Balozi mdogo wa
China Xie Xiaowu alimueleza Dk. Shein kuwa Jamhuri ya Watu wa China inathamini
uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Zanzibar na kuahidi kuendelea kutoa
nafasi za masomo nchini humo sambamba na kuleta wakufunzi kuja kutoa mafunzo
Zanzibar.
Balozi Xie Xiaowu
alimueleza Rais Dk. Shein kuwa urafiki wa Jamahuri ya Watu wa China na Zanzibar
ni wa miaka 55 hivi sasa, hivyo unaonesha wazi kuwa una historia kubwa na kuna
kila sababu ya kuendelezwa na kudumishwa kwa nguvu zote.
Nae Katibu wa Kamati
Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na Makamo Mkuu wa Taasisi ya ‘China
National Research Institute of Food Fermentation Industries’ kutoka China Dong
Weinhong amempongeza Dk. Shein kwa juhudi zake za kuhakikisha mafunzo hayo
yanafanyika.
Kiongozi huyo alieleza
kuwa juhudi hizo za Rais Dk. Shein ni lazima ziungwe mkono kwani zinaonesha
wazi kuwa ana hamu na nia ya kwuasaidia wananchi wake katika sekta zote za
maendeleo na kuahidi kuwa Taasisi hiyo itasimama bega kwa bega na yeye. Aliongeza
kuwa hatua hiyo inazidi kujenga uhusiano na ushirikiano mwema kati ya Jamhuri
ya Watu wa China na Zanzibar.
Mafunzo hayo
yanatarajiwa kuanza kesho Septemba 11, 2019 hadi Oktoba 10, 2019 ambayo
yatawashirikisha watendaji 45 kutoka Taasisi za Serikali na Binafsi wakiwemo
kutoka Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Baraza la Mapinduzi,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Chuo Cha Utalii Maruhubi, Uwanja wa Ndege
na Hoteli ya Verde.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment