Katibu Mkuu Wizara ya Sheria na Katiba Zanzibar Mhe. Georde Joseph Kazi, akihutubia wakati wa mkutano wa Wadau wa Sekta ya Sheria Zanzibar, wakijadili utafiti wa uwezekano kuazishwa kwa Jukwaa la Wanasheria Zanzibar, uliofanyika katika ukumbi waHoteli ya Zanzibar Beach Resort mazizini Zanzibar.
Na. Raya Hamad - WKS
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg George
Joseph Kazi amesema kuundwa kwa jukwaa
la wadau wa sekta ya sheria kutasaidia kuwaunganisha wadau wa sekta hiyo na kuleta maendeleo endelevu
katika kada hio muhimu
kwa maslahi yaTaifa.
Ameyasema hayo kwenye mkutano uliowakutanisha viongozi na
watendaji kutoka sekta ya sheria uliojadili
taarifa ya utafiti juu ya uwezekano wa kuanzisha jukwaa la pamoja kwa wahusika washeria
Zanzibar
Mhe.George Kazi amewataka wajumbe hao kutoa michango na mawazo yao
na kufanya upembuzi ili kuona mahitaji muhimu
yatakayosaidia kufahamu sekta ya
sheria, kwa kutambuwa kuwa sekta ya
sheria ndio kiini katika masuala yote ya maendeleo ya nchi .
Mbali ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu , Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, Tume ya kurekebisha Sheria na
Mahakama lakini kumekuwa na ongezeko
kubwa la wanasheria hata hivyo kinachokosekana
ni kutokuwa na jukwaa la pamoja linalowaunganisha wanasheria hao.
Jukwaa ambalo litasimamia na kuangalia maendeleo ya sekta ya
sheria hali ilivyo na jinsi gani itakuwa na uratibu ambao utasaidia kujuwa mambo mengi ya kuangalia wapi tulipotoka
,tulipo na tunakoelekea, matatizo gani
yanayoikumba sekta sheria iwe ya Jinai
na Madai kwa ajili ya maendeleo chanya
ya sekta ya hiyo.
Katibu George amesema
sekta ya sheria inaendelea kukuwa kwa kasi hivyo wizara imeona ipo haja ya kuwa
na chombo ambacho kitasaidia kuzidisha kasi ya uwajibikaji ili kila mmoja
atimize wajibu wake “muhimu kujielewa kama wanasheria kufahamu jukumu walilonalo
na kazi wanazozifanya ikiwemo kufanya
tathmini ya kile wanachokifanya badala ya kufanya kazi kwa mazoea, hii
itasaidia kuleta chachu katika sekta ya
sheria kujenga utamaduni wa kujisomea na
kufahamu mambo mapya yanayotokea hivyo jukwaa hili litatusaidia tuweze kujitambua”alisema
George
Ameendelea kusema kuwa kupitia Jukwaa upo uwezekano wa
kufanya utafiti na kufahamu kiwango cha ongezeko la wanasheria, kuwafahamu
mawakili na mahakimu na kuona sekta ya sheria imekuwa kwa kiwango gani na je ni kweli wamebobea kuwa wataalamu wanaofikia
kiwango na vigezo vinavyohitajika katika
kada ya sheria Kuwepo kwa Jukwaa moja litawezesha pia kutoa mapendekezo na kuwasilisha taarifa zao ambazo zitapelekea Wizara kuweza kuzifanyia
kazi kwa pamoja .
Nao wawasilishaji kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ndg Mohammed Khamis na ndugu Mussa Kombo wamesema lengo la kuwa na chombo hiki nikusaidiana
mawazo na ushauri ilikuona uwajibikaji unaimarika na sio kuingilia majukumu
yaVyombo vya kisheria pia kuondosha
migongano ya kisheria baina ya taasisi na kutekelezwa kwa vitendo mawazo na
ushauri utakaotolewa .
Nae Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar ndugu Ibrahim Mzee
Ibrahim ameanisha mambo manne ambayo yakitekelezwa
ipasavyo yatakuwa nichachu yamaendeleo ikiwemo vyombo vya mashtaka kufahamu majukumu
yao yakiutendaji, pia kufuatwa kwa Maadili na taratibu zake, usimamizi pamoja na suala la uwajibikaji na ushirikiano
baina ya vyombo vya Sheria vilivyopo nchini.
Aidha amesema kinachounganisha taasisi hizi zote za sheria ni
muongozo wa taasisi na kila chombo kinamamlaka yake na imewekewa sheria hivyo kuwepo kwa jukwaa hili kutasaidia
kuondosha baadhi misuguano na kuwa na sauti ya pamoja katika utekelezaji wa
masuala ya utowaji haki na sheria na
mwisho wa yote ni taasisi yenyewe
iliyopewa mamlaka kuona vipi inabadilika kwa kufuata taratibu
Mkurugenzi Mipango
Sera na Utafiti Bi Daima Mohamed
Mkalimoto amewataka wawasilishaji ya
mada kuyapitia majukumu ya Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na bajeti ya
Wizara ili kujenga hoja kwa msingi imara itayosaidia
kuundwa kwa kwa jukwaa la pamoja .
Bi Daima ametoa
mapendekezo kwa kuona tunaanajifunza pia mazuri
yanayotekelezeka kutoka kwa wengine na kusema kuwa uhai wa sekta ya sheria utaonekana
kwa kuangalia zaidi na kuona umuhimu wa kuweka
jukumu la kulinda rasilimali za nchi
kuangalia mikataba kiundani kutoa mapendekezo pia kuweka uwiyano katika jamii hata katika ngazi za Mikoa na Wilaya ili na wao waweze kuangalia masuala ya
kisheria katika maeneo yao.
Kamishna wa Kazi Bi Fatma
Iddi Ali amesema kuundwa kwa Jukwaa la
pamoja kwa sekta ya sheria hakutakuwa na muingiliano bali ni kuondoa ukakasi
lakini utazingatia umuhimu wa taasisi zinazoguswa kwani kila taasisi
inayosimamia sheria ina taratibu zake namiongozo yake ya kiutendaji
Aidha
amesisitiza juu ya namna yakumuandaa na
kumuuangalia mwanasheria na kazi anazozifanya ili aweze kuwa na maadili mazuri
anakoelekea kwa vile mwanasheria ndie anaetegemewa kuwa Jaji, Mrajisi wa
mahakama , Hakimu, Wakili ama kwa namna
yeyote kuwa msimamizi katika masuala ya sheria na utowaji wa
haki, Bi Hamisa Mmanga Makame Mkurugenzi mipango uendeshaji na rasilimaliwatu
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ameipongeza serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara
ya Katiba na Sheria kutokana na jitihada zilizopo ukilinganisha na miaka yanyuma
hivi sasa kila siku kunapiga hatua na maendeleo yanaonekana kupitia sekta ya sheria.
Wakili wa Mahakama kuu Zanzibar Bw Zaharani Mohamed Yussuf ametoa msisitizo kushirikishwa kikamilifu kwa
Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana ambao nao wanasimamia utatuzi wa migogoro, mali hivyo kuwepo kwachombo
hiki kutarahisisha utowaji wa haki kwaupande wao na kwa wanajamii .
Mkutano huo uliowakutanisha viongozi na watendaji
kutoka sekta ya sheria uliojadili
taarifa ya utafiti juu ya uwezekano wa kuanzisha jukwaa la pamoja kwa wahusika
wa sekta ya sheria Zanzibar umeandaliwa
na Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Shirika la Mendeleo la Umoja
wa Mataifa UNDP umefanyika kwenye ukumbi
wa mkutano uliopo Zanzibar Beach
Resort Mazizini.
Muwezeshaji kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar Ndg Mohammed Khamis akitoa mada kuhusu taarifa ya utafiti juu ya uwezekano wa kuanzisha jukwaa la pamoja kwa wahusika sekta ya sheria Zanzibar
No comments:
Post a Comment