Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapiunduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar, katika ukumbi wa VIP Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, baada ya kuwasili akitokea Ras Al Khaimah, baada ya kumaliza ziara yake ya wiki moja.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amerejea nchini leo akitokea Nchi za Umoja wa
Falme za Kiarabu (UAE) ambapo alifanya ziara nchini Ras Al Khaimah pamoja na
Abudhabi ikiwa ni muwaliko wa kiongozi wa Ras Al Khaimah Sheikh Saud Bin Saqr Al Qasimi kwa ziara ya wiki moja.
Ziara hiyo ya Rais Dk.
Shein ilianza tarehe 23 na kumaliza jana tarehe 28 Septemba mwaka huu 2019 ambapo
katika ziara hiyo, alipata fursa ya kuzungumza na mwenyeji wake Mtawala wa Ras-Al-Khaimah Sheikh
Saud Bin Saqr Al Qasimi pamoja na kuzungumza na Sheikh Mohammed
bin Zayed Al Nahyan, Mrithi wa Mtawala wa Abu Dhabi na Naibu Amiri Jeshi Mkuu
wa Vikosi vya Ulinzi wa Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE)
Katika uwanja wa
ndege wa Kimataifa
wa Abeid Amani Karume Rais Dk. Shein alipokewa na viongozi mbali mbali wa vyama
vya siasa na Serikali pamaaoja na viongozi
wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama wakiongozwa na Makamo wa Pili wa Rais wa
Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd.
Mara
baada kuwasili kiwanjani hapo, Rais Dk. Shein alifanya mazungumzo na Waandishi
wa habari wa vyombo mbali mbali vikiwemo vya Serikali na binafsi ambapo katika
maelezo yake alieleza mafanikio makubwa ya ziara hiyo ikiwa ni pamoja na
mapokezi mazuri aliyoyapata yeye na ujumbe wake aliofuatana nao.
Aidha,
Rais Dk. Shein alieleza hatua zilizofikiwa na Kampuni ya Mafuta ya “RAK GAS”
inayojishughulisha na utafiti wa mafuta na gesi asilia hapa Zanzibar na
kusisitiza kuwa kazi iliyofikiwa ni nzuri na kila hatua itakayofikia wananchi
wataelezwa.
Rais
Dk. Shein aliwataka wananchi wasihadaiwe na wale wanaopenda kusema kuwa Rais
amefunja sharia na katiba na kusisitiza
kuwa suala la mafuta na gesi liko vizuri wala hakuna Sheria wala Katiba
iliyovunjwa.
Rais
Dk. Shein pia, alieleza namna ya Kiongozi wa Abudhabi Sheikh Mohammed bin Zayed
Al Nahyan alivyomuhakikishia kuwa yuko tayari kuiunga mkono Zanzibar katika
kutafuta nishati mbadala ambayo kwa upande wa Zanzibar nishati hiyo inatazamiwa
kuwa itakuwa nishati ya jua.
Alieleza
kuwa tayari Zanzibar kazi imeshaanza kufanywa katika kuhakikisha nishati
mbadala ya jua ndio kipaumbele ambapo kwa mashirikiano ya Shirika la Maendeleo
la Umoja wa Mataifa (UNDP) pamoja na Umoja wa Ulaya (EU).
Pamoja
na hayo, Rais Dk. Shein alieleza kuwa tayari kuna wawekezaji ambao wako tayari
kuja kuekeza katika umeme wa jua ambapo kwa upande wa Serikali imo katika
kuandaa mipango madhubuti.
Rais
Dk. Shein alieleza hatua zinazochukuliwa na Serikali ikiwa ni pamoja na kutoa
fedha zake wenyewe kwa ajili ya uendeleza wa ujenzi wa jengo jipya la abiria la
uwanja wa ndege huku akieleza hatua za ujenzi wa bandari mpya ya Mpigaduri ambayo
alieleza azma ya Serikali kuanza ujenzi japo wa awali kabda hajamaliza muda
wake.
Alieleza
kuwa tayari fedha za Mkopo kutoka Benki ya Exim ya Indonesia umepatikana
sambamba na ujenzi wa bandari ya mafuta na gesi huko Mangapwani ambao
unatarajiwa kuanza hivi karibuni.
Kwa
upande wa msaada wa fedha Bilioni 23 zilizotolewa na Mfuko wa Khalifa Fund,
Rais Dk. Shein alisema kuwa mbali ya fedha hizo pia, Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kwa upande wake itatoa fedha kama hizo na kufikia Bilioni 46 kwa ajili
ya kuwawezesha vijana wakiwemo wajisiriamali na wanawake
Alisisitiza
azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya
wafanyabiashara ikiwa ni pamoja na kuimarisha uhusiano na ushsirikiano kati ya
wafanyabiashara wa Zanzibar na wale wa Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
Akiwa
UAE, Rais Dk. Shein alikutana na viongozi
mbali mbali wakiwemo wa Kampuni ya Kimataifa ya Utafiti na Uchimbaji wa Mafuta
na gesi asilia ya Ras Al Khaimah “Rak Gas”, Kampuni ya RAKEZ, Kampuni ya Mji wa
Bahari wa Ras Al Khaiman, Mamlaka ya Uendelezaji Utalii ya Ras Al Khaimah, uongozi
wa Taasisi ya Sera na Utafiti ya Kiongozi wa Ras Al Khaiman.
Kiongozi wa Ras Al Khaimah Sheikh Sheikh Saud Bin Saqr Al Qasimi
alimuandalia Rais Dk. Shein dhifa maalum ya kitaifa ya chakula cha mchana mara
baada ya mazungumzo yao huko nyumbani kwake mnamo Septemba 23 pamoja na
kumuandalia dhifa maaluma ya kitaifa ya chakula la usiku huko katika hoteli ya Kimataifa ya “The ritz
Carlton” katika jangwa la Wadi ya hifadhi ya asili iliyopo nje kidogo ya mji wa
Ras Al Khaimah
Rais Dk. Shein akiwa Ras
Al Khaimah atatembelea maeneo ya mji wa Ras Al Khaiman ikiwa ni
pamoja na maeneo mengine ya kitalii katika mji huo na eneo la kiwanda cha Kampuni
ya Kimataifa ya Utafiti na Uchimbaji wa Mafuta na gesi asilia ya Ras Al
Khaimah.
Aidha, Dk. Shein atakwenda
Abu Dhabi kwa ajili ya kushuhudia utiaji wa saini Mkataba wa Mashirikiano kati
ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya UAE kupitia Mfuko wa
‘Khalifa Fund’ kwa ajili ya kwuasaidia vijana.
Katika
ziara hiyo, Dk. Shein amefuatana na viongozi mbali mbali akiwemo Mke wa Rais wa
Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, Waziri wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi Issa Ussi Haji Gavu, Waziri wa Fedha na Mipango Balozi Mohamed
Ramia Abdiwawa, Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Salama Aboud Talib.
Wengine
ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Said Hassan Said, Balozi Mohamed Haji Hamza
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa
upande wa Zanzibar pamoja na watendaji wengine wa Serikali.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment