Habari za Punde

Wajumbe Baraza la Wawakilishi watembelea eneo la kujenga Ofisi za SMZ Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine akiwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Abdallah Hassan Mitawi, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar hiyo Mhe. Ali Selemani Ali na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais Lupi Mwaikambo wakiwa katika eneo la kiwanja kilichokabidhiwa kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.


Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar wametembelea kiwanja kwa ajili ya kujengwa Ofisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) katika eneo la Mahoma Makulu Jijini  Dodoma.
Ziara hiyo pia ilihusisha wataalamu kutoka Serikali hiyo na viongozi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Zanzibar Mhe. Mihayo Juma Nhunga ambaye aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwakabidhi pa kiwanja hicho.
Mhe. Nhunga alisema kuwa SMZ inafarijika kupata kiwanja hicho ambacho kina ukubwa wa hekta 30 na kuwa itaanza haraka ujenzi wa izo uhusiano wa pande mbili za Muungano utaendelea kuimarika.
Serikali hizi mbili zina uhusiano na ushirikiano mzuri na tunaona namna Serikali ya Jamhuri ya Muungano ilivyojitoa na kutupatia kiwanja hiki na tunaona thamani ya Dodoma sasa tofauti na zamani hivyo tunaanza haraka ujenzi wa ofisi zetu tuhamie hapa," alisema.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Ali Selemani Ali wanashukuru kwa kupata ardhi hiyo na kuwa ina thamani kubwa kwa Serikali ya Zanzibar hivyo undugu baina ya pande hizo mbili utaendelea kuimarika.
Mhe. Ali aliahidi kuwa kama Kamati wataishauri SMZ kuanzisha ujenzi wa Ofisi za serikali hiyo kwa kasi ili waweze kuhamia na kuanza shughuli zake katika Jiji la Dodoma.
Akitoa shukrani zake kwa ujumbe huo Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine aliyeambatana na wakurugenzi wa Idara ya Muungano  aliwakarisha kuanza ujenzi na kuhamia.
Balozi Sokoine alisema kuwa kukamilika kwa ujenzi wa Ofisi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kutaimarisha Muungano na undugu baina ya wananchi wa pande hizo mbili.
"Tunafarijika sana tunapoona mnafika hapa kwenye kiwanja chenu mara kwa mara na kuona namna mtakavyoanza ujenzi na kukamilika kwa Ofisi hizi kutaleta ushirikiano mzuri baina yetu sote," alisema.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Zanzibar Mhe. Mihayo Juma Nhunga akizungumza wakati wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar walipotembelea eneo la kiwanja walichokabidhiwa SMZ na Serikali ya Muungano.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar hiyo Mhe. Ali Selemani Ali akizungumza mbele ya wajumbe wa Kamati hiyo na viongozi mbalimbali walipofika katika eneo walilokabidhiwa.
Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar wakikagua eneo walilokabidhiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Wajumbe wakiangalia ramani ya eneo hilo walilokabidhiwa kutoka kwa mtaalamu wa ardhi.





No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.