Habari za Punde

Naibu Waziri Wa Afya Atoa Taarifa Ya Uzinduzi Wa Mkakati Wa Kupunguza Vifa Vya Mama Na Mtoto Zanzibar

 Mratibu wa Huduma za Mama na Mtoto Wanu Bakari akitoa maelezo kuhusiana na Uzazi salama katika mafunzo ya Waandishi wa Habari yanayohusu huduma na kupunguza vifo vya  mama na Mtoto katika ukumbi wa Hospitali ya wagonjwa wa Akili Kidonge Chekundu Zanzibar.
 Mkuu wa kitengo cha Uhamasishaji na Mafunzo ya Uzazi salama Kassim Issa Kirobo akitoa mafunzo kwa Waandishi wa Habari kuhusiana na Uzazi  katika ukumbi wa Hospitali ya wagonjwa wa Akili Kidongo Chekundu Zanzibar.
 Mkurugenzi Kinga na Elimu ya Afya Dk,Fadhil Mohamed Abdalla akitoa hotuba ya makaribisho kwa Mgeni Rasmi katika mkutano wa Waandishi wa Habari kuhusu otoaji wa Taarifa ya uzinduzi  wa mkakati  wa Kupunguza Vifo vya mama na mtoto pamoja na uzinduzi wa Boti  ya kuwasaidia Wazazi watakaopata matatiza katika Visiwa  vya Pemba uzinduzi utakaofanyika  9/10/2019 Zanzibar ,hafla iliofanyika katika ukumbi wa Wizara ya Afya Mnazi mmoja mjini Unguja.
Naibu Waziri wa Afya Harusi Said Suleiman akitoa Taarifa kwa Waandishi wa Habari kuhusiana na  uzinduzi wa mkakati wa Kupunguza Vifo vya mama na mtoto pamoja na Uzinduzi wa Boti ya kuwasaidia Wazazi watakaopata matatiza katika Visiwa  vya Pemba Uzinduzi utakao fanyika  9/10/2019 Zanzibar ,hafla iliofanyika katika ukumbi wa Wizara ya Afya Mnazi mmoja mjini Unguja.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.