Habari za Punde

Naibu Waziri Shonza: Wanatasnia ya Filamu Rasimisheni Kazi zenu


Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza  (aliyeketi watatu kushoto) akitizama filamu ya masanii wa filamu Maria Luya aliyomkabidhi wakati alipokuwa akifanya  kikao na wadau wa tansia ya filamu mkoa wa singida hawapo pichani,wa kwanza kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Dkt.Kiagho Kilonzo, na wapili kushoto ni Katibu Tawala Wilaya ya Singida  Wilson Shimo.

Na Anitha Jonas – WHUSM. -Singida.
Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni,  Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza amewasisitiza wanatasnia ya filamu kuhakikisha wanarasimisha kazi zao na kujisajili.

Mheshimiwa Shonza ametoa  agizo  hiyo  leo  Mkoani  Singida alipokuwa akifanya kikao na wadau wa tasnia ya filamu wa mkoa huo kwa lengo la kutaka kusikiliza kero zao na kuwaeleza wadau hao mikakati ya serikali katika kuboresha tasnia hiyo,kuthibiti uharamia  ili kuhakikisha wanafaidika na kazi zao.

Akiendelea kuzungumza katika kikao hicho Naibu Waziri huyo aliwasisitiza wanatasnia hao wa filamu kuzingatia suala la uandaaji wa muswada wa filamu na kupeleka miswada hiyo kwa maafisa utamaduni  kwa ajili ya ukaguzi na kupata ushauri wa filamu watakayoandaa  sababu hiyo ni moja ya njia itakayosaidia kuandaa kazi zenye ubora.

“Kwanza ningependa niwashauri muache kusambaza au kuuza kazi zenu kwa njia ya ‘flash’ katika vibanda vya kuuza filamu sababu hii bado ni njia inayowakandamiza na hauwezi kupata faida ya kazi yako, sasa hivi kazi hizo za filamu zinasambazwa kwa mfumo wa kidigitali mfano kwenye Swahilifilx na Netflix,kikubwa ni kazi yako iwe yenye ubora na iliyozingatia utaratibu wa kitaalamu katika kuandaa filamu ikiwemo wachezaji  kuvaa uhusika na kucheza katika maeneo yenye uhalisia wa filamu hiyo,”alisema Mhe.Shonza.

Naye Kaimu Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Dkt.Kiagho Kilonzo bodi  imekuwa ikitoa mafunzo kwa wadau wa tasnia hiyo kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kuandaa kazi bora zitakazo kuwa na ushindani  kwa  ndani na nje ya nchi  na kwa hivi karibuni wanatarajia kufanya mafunzo hayo mkoani Dodoma na kwa wadau wa Singida ambao hawajawahi kupata mafunzo hayo wanakaribishwa kushiriki.

“Bodi ya filamu katika kuimarisha masoko ya usambazaji wa filamu ndani na nje ya nchi imempata mdau kutoka Nigeria  mwenye Kampuni iitwayo ENVIVO ambaye yupo tayari kununua jumla kazi mia moja mpaka ifikapo mwezi Juni mwaka huu,zenye hadithi mbalimbali za kitanzania ambapo zitatafsiriwa kwa lugha kwa lugha ya Yoruba,Pijini  na Igbo kusambazwa,kikubwa katika kazi hizo ni ziwe zimebeba hadithi za kitanzania na zenye ubora na pia ziwezinaendana na  muswada,”alisema Dkt.Kilonzo.

Pamoja na hayo Dkt.Kilonzo aliwasihii wadau hao kuwa mfumo wa usambazajiwa kwa kazi za filamu kwa sasa umebadilika na filamu kwa sasa mara baada ya kukamilika inafanyiwa uzinduzi katika majumba ya sinema na huko itaonyeshwa kwa kipindi fulani na baadae inapelekwa katika mifumo mingine ya kidigitali na hatua ya kuiweka katika CD na Youtube niyamwisho hii ni katika kulinda kazi hizo na uharamia pia kuhakikisha msanii anapata faida ya kazi yake.

Kwa upande wa Afisa Utamaduni Mkoa Bw.Hendry Kapera alisema wasanii wengi wa filamu katika mkoa huo hawataki kujisajili wala kurasimisha kazi zao hii ni changamoto kubwa na wamekuwa wakijiweka mbali na maafisa utamaduni wa wakihofia kuulizwa kuhusu usajili na hii imechangia wao kuandaa kazi zisizo na ubora sababu hawapendi kushirikiana na maafisa hao.

Halikadhilika nae mmoja ya wasanii hao wa filamu kutoka Wilaya ya Ikungi  Bw.Salumu Ntandu aliomba bodi ya filamu kuwapatia mafunzo wadau hao wa mkoa huo na pia aliwasihii wasanii wenzake kuwa na umoja na kuacha migogoro kwani umoja wao ndiyo utakaoweza kutangaza kazi zao na kutangaza mkoa wao pale watakapo andaa kazi nzuri zenye ubora na kushirikishana katika kuitangaza na  kuizindua.

Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza  akizungumza na wadau wa tasnia ya filamu Mkoa wa Singida leo na kuwasisitiza kurasimisha kazi zao pamoja na kujisajili,katika  kikao cha kusikiliza kero za wadau hao na kuwaeleza mikakati ya serikali  katika kuimarisha  tasnia hiyo kilichoandaliwa na Bodi ya Filamu Tanzania.
Kaimu Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Dkt.Kiagho Kilonzo akizungumza na wadau wa tasnia ya Filamu Mkoa wa Singida leo kuhusu mikakati ya bodi ya filamu katika kuimarisha mazingira ya usambazaji wa kazi za filamu nje ya nchi ambapo wameipata kampuni kutoka Nigerea itakayo nunua filamu mia moja zenye hadithi za asili ya kitanzania,wapili kushoto ni Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza ,wa kwanza kushoto ni Katibu Tawala Wilaya ya Singida  Wilson Shimo na wa kwanza kuliani Afisa Utamaduni  Mkoa wa Sngida Bw.Hendry Kapera.
Msanii wa Komedi kutoka kikundi cha Magic Sanaa Group  Singida Mjini  kutoka Kata ya Mwenge  Bw.Yusuph Ally  akitoa maombi yake kwa uongozi wa  bodi ya filamu kuwapatia vitambulisho wasanii wa mkoa huo leo katika kikao cha Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza  na viongozi wa bodi ya Filamu hawapo pichani.
Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza  (aliyeketi wapili kushoto)  akimsikiliza Msanii wa Filamu Mkoa wa Singida Bi.Maria Luya akimweleza  stori ya kuhusu filamu yake iitwayo furaha kabla ya kumkadhi leo katika kikao chake na wadau hao wa filamu kilichofanyika Mkoani Singida,wa kwanza kulia ni Katibu Tawala Wilaya ya Singida  Wilson Shimo na wa pili  kulia ni Kaimu ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Dkt.Kiagho Kilonzo.
Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza  aliyeketi watatu kushoto  akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa tasnia ya filamu Mkoani Singida leo mara baaada ya kulamizika kikao cha kusikiliza kero za wadau hao na kueleza mipango ya serikali katika kuimarisha sekta hiyo na kuthibibiti uharamia wa kazi za filamu na kuhakikisha msanii ananufaika na kazi yake,wa pili kulia Kaimu ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Dkt.Kiagho Kilonzo pamoja na Katibu Tawala Wilaya ya Singida  Wilson Shimo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.