RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein,
akikata uteke kuashiria kuifungua barabara ya Bububu hadi Mkokotoni iliyojengwa
kwa kiwango cha lami na kampuni ya Ujenzi kutoka Chini ya (CCECC) (kulia kwa Rais) Waziri wa Ujenzi
Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar.Mhe.Dkt, Sira Ubwa na Mwakilishi wa
Kampuni ya Ujenzi ya Kanda ya Afrika Mashariki Bw.Zhang Junle na (kushoto kwa
Rais) Katibu Mkuu Ndg. Mustafa Aboud Jumbe na Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo
ya Afrika (AfDB) Meneja Mkaazi Bw.Alex,M.Mubiru.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amewataka wale wote wanaosingizia demokrasia na kuhakiribu
kwa makusudi barabara wakiwemo vijana kuacha mara moja tabia hiyo.
Rais Dk. Shein
aliyasema hayo leo katika hotuba yake aliyoitoa kwenye hafla ya ufunguzi wa Barabara
ya Bububu-Mahonda-Mkokotoni yenye urefu wa kilomita 31, hafla iliyofanyika Mkokotoni,
Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini Unguja ikiwa ni shamra shamra za miaka
56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais Dk. Shein alitoa
wito kwa wale wote wakiwemo vijana wanaoharibu barabara kwa kusingizia
demokrasia kwani hawaijui wala haiitambua demokrasia hiyo hukua akiwataka
madereva kujua athari za oil na mafuta barabarani.
Aliwataka vijana
kutogombana na barabara na kuwaeleza kuwa wasigombane na kitu kisichosema na
kama kuna mtu kawaudhi basi wapambane na huyo aliowaudhi na si barabara na badala
yake barabara hiyo waitunze.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa barabara hiyo ni muhimu sana katika maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa
Kaskazini ambapo Wakoloni hawakuona umuhimu wake wakati wakiitawala Zanzibar.
Alisema kuwa kutokana
na hatua hiyo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliamua kwa makusudi kujenga
barabara hiyo ambapo mbali ya barabara wakoloni walidharau kuwapa Wazazibari huduma
za afya, elimu ardhi na nyenginezo.
Alieleza kuwa kutokana
na hatua hiyo ndipo wazee walipoamua kujitawala wenyewe ili mambo yote yaweze
kufanyika kwa maendeleo ya Wazanzibari wote.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa Mapinduzi yamefanyika kwa ajili ya kuondosha ubinafsi, umbwannyenye,
madhila na dhulma kwa wafanyakazi na wakulima.
Mapinduzi yameikomboa
Zanzibar na leo iko huru chini ya chama cha ASP, ambapo kama si Mapinduzi
maendeleo hayo yasingelipatikana na kuongeza kuwa maendeleo yameletwa na ASP na
leo CCM.
Alisema kuwa mbali ya
fedha zilizokopwa na Serikali ya Mapinduziya Zanzibar kutoka Benki ya AfDB zipatazo
Bilioni 33.824 pia, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetoa TZS Bilioni 4
katika ujenzi wa barabara hiyo.
Alisema kuwa miaka
minane imepita barabara ya Ole- Kengeja haijesha lakini juhudi za makusudi
zimechukuliwa katika kuhakikisha barabara hiyo inamalizika ambapo hivi sasa
kilomita 20 imeshatiwa lami na kuahidi kuwa barabara hiyo itakwisha na sherehe
za ufunguzi zitafanyika.
“Barabara hii iko kama
mgongo wa ngisi”,alisisitiza Dk. Shein. Aidha, Rais Dk. Shein alisema kuwa
barabara hiyo kwa ukumbwa wake na uzuri wake ni namba moja kwani imenawiri sana
kwani ina madaraja mengi na yako imara.
Rais Dk. Shein
aliipongeza Kampuni iliyojenga barabara hiyo pamoja na kuipongeza Wizara pamoja
na uongozi wake wote na wafanyakazi wa Wizara hiyo na kusisitiza haja ya
kutunzwa kwa barabara hiyo.
Alisema kuwa Mkoa wa
Kaskazini Unguja ni maarufu kwa ajali za barabarani na kuwataka madereva
kutahadhari sana na kuwataka wazee na wazazi kutokaribia barabarani na kutaka
watoto waelimishe juu ya athari za barabara pamoja na wale wanaolala barabarani
kuacha mchezo huo.
Alilitaka jenshi la
Polisi wa barabarani kufanya kazi za ulizni barabarani na kutodharau kazi zao
na kutaka waifanye kazi zao kwa heshima kubwa na busara ili kuepuka ajali za
barabarani.
Alitoa shukurani kwa
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kuikopesha Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kwa azma ya kujenga barabara za Unguja na Pemba na kuwataka wananchi
kuzitunza barabara zinazojengwa pamoja na miradi mengine inayojengwa na
Serikali kwani hizo ni mali za watu wote.
Sambamba na hayo, Rais
Dk. Shein alisema kuwa Serikali ina mpango wa kujenga mji mpya wa kisasa pamoja
na kujengwa kwa soko la kisasa katika eneo la Mkokotoni ambayo itakuwa
Mkokotoni mpya na kuwataka wananchi kuunga mkono juhudi hizo.
Mapema Rais Dk. Shein
alizindua barabara hiyo huko katika eneo
la Bububu kwa Nyanya sambamba na kukata utembe kuashiria uzinduzi rasmin wa
Barabara hiyo ya Bububu-Mahonda hadi Mkokotoni na kuwaeleza wananchi
walaiohudhuria katika eneo hilo azma ya Serikali ya kumalizia ujenzi wa
barabara hiyo kutoka eneo hllo hadi kituo cha Polisi Bububu.
Rais Dk. Shein
aliwaeleza wananchi hao kuwa si muda mrefu ujenzi huo utaanza na wajenzi
watakaojenga barabara hiyo ni Kampuni iliyojenga barabara ya Bububu-Mahonda
hadi Mkokotoni Kampuni ya “ China Civil Engineering Construction Corporation”
(CCECC).
Pia, Rais Dk. Shein
aliwasisitiza wazee na wazazi wanaoishi pembezoni mwa barabara hiyo kuhakikisha
inawaenga enga vizuri watoto wao katika kutumia barabara hiyo ili kuepuka ajali
zisizo za lazima.
Wakati huo huo, Rais
Dk. Shein alitoa zawadi kwa washindi walioshinda mashindano ya mbio za baskeli
zilianzia Bububu kwa Nyanya hadi Mkokotoni ambao miongoni mwao ni Ahmed Simai
Tajo Kutoka Dimani, Shukura Mwiga Faki kutoka Chaani na wa tatu ni Khamis Juma
Kheir kutoka Dimani ambapo kwa upamnde wa watoto wadogo ni Omar Ibrahim Omar
kutoka Kianga, Harith Mbarouk Abdalla kutoka Chaani na wa tatu ni Sheha
Abdallah Abubakar kutoka Kianga.
Nae Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano
na Usafirishaji Dk. Sira Ubwa Mamboya alisema kuwa matokeo mazuri ya ukuaji uchumi
yanategemea mambo mengi na moja wapo ni miundombinu imara ya barabara ambayo
hupelekea kukua kwa sekta nyingi za kiuchumi ikiwemo biashara, kilimo, utalii
na nyengine ambazo ni muhimu kwa uchumi.
Aliongeza kuwa alisema
akuwa ujenzi wa barabara hiyo ni juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya
kuimarisha miundombinu ya barabara kwa ajili ya kurahisisha huduma za usafiri
na usafirishaji mjini na vijijini.
Alisema kuwa barabara
nyingi zilizotajwa katika Ilani ya Uchaguziya mwaka 2015-2020 tayari
zimeshajengwa ikiwemo barabara hiyo ambapo alisema kuwa zipo barabara nyengine
ambazo zinaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami Unguja na Pemba ambazo ndani
ya mwaka huu wa 2020 zitakamilika.
Akizitaja barabara
ambazo zinatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu kuwani barabara ya Ole hadi
Kengeja Pemba, barabara ya Matemwe hadi Muyuni na Fuoni hadi Kombeni.
Alisema kuwa
kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo itapelekea kuongeza kasi ya maendeleo
kwa Mkoa wa KaskaziniUnguja na Mikoa mengine ya Zanzibar hali hiyo inatokana na
kuwepo kwa huduma bora ya usafiri na usafirishaji wa bidhaa mbali mbali sambamba na kukuza sekta ya
utalii na kupelekea kuongeza pato laTaifa.
Waziri Dk. Sira alisisitiza
kuwa Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12, 1964 ndio Dira ya mafanikio yote hayo
hivyo, aliwaomba wananchi wote kwa pamoja kuyaenzi na kuyalinda kwa manufaa yao
na vizazi vijavyo.
Mapema Katibu Mkuu wa
Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Mustafa Aboud Jumbe alisema kuwa
ujenzi wa barabara ya Bububu-Mahonda
hadi Mkokotoni ni miongoni mwa jitihada zinazochukuliwa na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar tokea Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964 ya kujenga ustawi
wa wananchi wake kwa kuimarisha na kuendeleza miundombinu ya barabara za mjini
na vijijini.
Aidha, alisema kuwa
ujenzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka
2015-2020 kama ilivyoandikwa kwenye ukurasa wa 139 kupitia Sura ya 88, Dira ya
Maendeleo (Vision 2020), MKUZA III, Sera ya Taifa ya Usafiri pamoja na Mpango
Mkuu wa Usafiri Zanzibar.
Alisema kuwa mradi huo
ulitiwa saini tarehe 8 Novemba 2017 baina ya Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na
Usafirishaji na Mjenzi ambaye ni Kampuni ya ‘China Civil Engineering Construction
Corporation’ (CCECC), kwa thamani ya TZS Bilioni 58.617.
Aliongeza kuwa
Msimamizi wa Mradi ni Kampuni ya H.P Gauff Ingenieure GmbH ya Ujerumani ambae
alifungiana Mkataba na Wizara hiyo tarehe 15 Julai 2017 kwa thamani ya Euro
Milioni 1.180.
Kwa maelezo ya Katibu
Mkuu huyo Mkataba huo unajumuisha ujenzi wa Barabara hiyo pamoja na ujenzi wa
barabara ya Pale-Kiongele yenye kilomita 4.6, Matemwe-Muyuni Kilomita 7.5 na
barabara ya Fuoni-Kombeni yenye kilomita 8.56.
Alisema kuwa muda wa
utekelezaji wa mradi huo ni miezi 24 ikijumuisha muda wa kuleta vifaa ambapo
mradi ulianza tarehe 1 Machi 2018 na unatarajiwa kukamilika 29 Februari 2020.
Katibu Mkuu huyo
alisema kuwa barabara hiyo ilikuwa katika hali mbaya kutokana kumaliza muda
wake na lami iliyokuwepo ilikuwa katika hali mbaya na yenye mashimo kiasi
ambacho ilihitaji kujengwa upya na kwa upande wa barabara za Pale-Kiongele,
Fuoni-Kombeni na Matemwe-Muyuni zilikuwa barabara za kifusi.
Sambamba na hayo,
alisema kuwa ujenzi wa barabara hiyo ulianza rasmi mwezi wa Juni, 2018 na
unatarajiwa kumaliza mwishoni mwa mwezi wa Februari 2020 ambapo ujenzi wake
umekamilika kwa kiwango cha lami mwanzoni mwa mwezi Disemba 2019.
Alieleza kuwa gharama
za mwanzo zilizotumika kwa ujenzi wa barabara ya Bububu-Mahonda hadi Mkokotoni
ni TZS Bilioni 28.513. Aidha, Serikali imefidia nyumba na vipando vya wananchi
kwa gharama za TZS Bilioni 4.014 ambapo watu 2,255 wamefidiwa ambapo pia, gharama za kuhamisha huduma za maji ni TZS Milioni
964 na uhamishaji wa miundombinu ya umeme ni Milioni 331 na kufikia Bilioni
33.824.
Alisisitiza haja kwa
wananchi kufuata sheria za barabara kwani katika kipindi kifupi cha ujenzi wa
barabara hiyo tayari ajali nane zimeshatokea ambazo miongoni mwao zipo
zilizosababisha vifo.
Aliongeza kuwa kwa
sehemu ya barabara kutoka Bububu Polisi hadi Kwanyanya (Chuini) yenye urefu wa
Kilomita 2.8, Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji
inamalizia taratibu za kumuongezea kazi Mkandarasi huyo wa Kampuni ya (CCECC)
ili aijenge sehemu hiyo na kuikamilisha kwa kiwango kilekile na unategeewa
ujenzi huo kumaliza kabla ya mwezi Juni 2020.
Kwa niaba ya Wizara ya
Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Katibu Mkuu huyo alitoa shukurani za dhati
kwa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kutoa mkopo wa utekelezaji wa mradi
huo wa barabara ya Bububu-Mahonda hadi Mkokotoni.
Nae Mwakilishi wa Benki
ya Maendeleo Afrika (AfDB), Alex Mubiru alisema
kuwa mnamo mwaka 2015 benki hiyo iliidhinisha jumla ya Dola za Kimarekani
milioni 350 kwa ajili ya kuimarisha barabara zenye urefu wa kilomita 492 katika
barabara za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania moja wapo ikiwa barabara hiyo.
Aidha, alisema kuwa
wakati AfDB inaundwa 1994 ilikuwa na ndoto ya ndoto ya Afrika iliyokuwa na
uchumi ambapo leo ndoto hiyo imetimiaa kwa upande wa Zanzibar.
Alisema kuwa ujenzi wa
barabara hiyo ni uthibitisho wa azma ya viongozi wa AfDB ambapo kilomita za
baraara iliyojengwa, jiwe lililowekwa na madaraja yaliyojengwa ni dhamira ya
viongozi wa benki hiyo ambapo leo hii inaona fahari sana katika kupata
maendeleo hayo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment