Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein Atunuku Nishani za Mapinduzi Viwanja vya Ikulu Jijini Zanzibar.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimtunuku Nishani ya Mapinduzi kwa Viongozi na Wananchi Wenye Sifa Maalum,Ndg.Zaidi Juma Ussi, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Ikulu Jijini Zanzibar.ikiwa ni shamrashamra za kuadhiumisha Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ametunuku Nishani ya Mapinduzi, Nishani ya Utumishi Uliotukuka pamoja na Nishani ya Ushujaa kwa Viongozi, Watumishi wa Umma, Maafisa na Wapiganaji wa Idara Maalum za SMZ na wananchi mbali mbali wenye sifa maalum.

Hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya Ikulu jijini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali, Vyama vya siasa, viongozi wakuu wastaafu akiwemo Rais Mstaafu wa Awamu ya Sita wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Amani Abeid Karume, Makamo wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohamed Kharib Bilal.

Viongozi wengine waliohudhuria ni Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, Waziri Kiongozi Mstaafu Shamsi Vuai Nahodha, Mawaziri na viongozi wengine wa Serikali, wananchi na wanafamilia, hafla ambayo ni muendelelezo wa shamra shamra za miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12, 1964.

Mapema akitoa tamko la Kwanza la kuashiria kuanza shughuli hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum alisema kuwa Rais Dk. Shein ametunuku Nishani 37 ya Mapinduzi, Nishani 10 ya Utumishi Uliotukuka na Nishani 25 ya Ushujaa kwa Viongozi, Watumishi wa Umma, Maafisa na Wapiganaji wa Idara Maalum za SMZ pamoja na wananchi mbali mbali.

Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa sherehe hiyo ilihudhuriwa na watunukiwa 72 ambao kati ya hao 22 ni Marehemu ambao Nishani zao zimepokelewa na wawakilishi wao na 50 wako hai ambapo nishani zao watapokea wenyewe au zitapokewa kwa niaba yao.

Alisema kuwa Watunuku wote sifa zao zimekidhi matakwa ya Nishani hizo ambapo Nishani ya Mapinduzi hutolewa kwa mtu ambaye aliasisi au alishiriki au aliyatukuza na aliyaenzi Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12, 1964.

Aliongeza kuwa Mtunukiwa ni pamoja na Kiongozi au mtu mwengine aliyehai au aliyefariki ambaye aliiletea sifa Zanzibar katika fani mbali mbali na kuonesha maadili mema ya kusifika na kuigwa ambapo katika Sherehe hizo, Nishani ya Mapinduzi inatunukiwa katika kundi la Viongozi na Wananchi wenye sifa maalum.

Kwa maelezo ya Katibu Mkuu huyo Nishani ya Utumishi uliotukuka hutolewa kwa Mtumishi wa Umma au Idara Maalum za SMZ aliyehai au aliyefariki ambaye ametimiza Utumishi wake kwa muda wa miaka isiyopungua 20 mfululizo na kwa Mtumishi wa Idara Maalum za SMZ miaka isiyopungua 20 ya kuwa Ofisa na katika kipindi chote hicho amekuwa na tabia njema.

Aliongeza kuwa Mtumishi huyo awe ametumikia Taifa kwa Uzalendo wa hali ya juu na kufanya kazi kwa kujitolea, uwajibikaji, uadilifu, ujasiri na umakini katika kusimamia majukumu na utendaji kazi.

Aidha, Katibu Salum alieleza kuwa Nishani ya Ushujaa inatolewa kwa Mtumishi wa Idara Maalum za SMZ au mtu mwengine yoyote aliyehai au aliyefariki ambaye ametenda kitendo cha Ushujaa, Ujasiri na Uzalendo ambacho kimesaidia kuokoa mali au uhai wa mtu au kujitolea maisha yake kwa ajili ya ulinzi wa Taifa.

Pamoja na hayo, Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa Vitendo hivyo vya ushujaa viwe wazi ambavyo mtunukiwa alivifanya na kuthibitishwa, mahala popote pale penye hatari na ameendelea kuwa muaminifu na mtiifu kwa nchi na Serikali yake.

Katika hafla hiyo, Dk. Shein alitoa Nishani ya Mapinduzi kwa Viongozi na wananchi wenye sifa husika akiwemo Asha Abdalla Juma, Meja Jenerali Mstaafu Khamis Rajab Semfuko, Kamishna wa Polisi Mstaafu Marehemu Mussa Khamis Ramadhan, Kanal Mstaafu Ahui Hassan Ahui, Kapteni Mstaafu Mohammed Mahamoud Juma, Kamanda Mstaafu Abdi Makame Mbai, Msaidizi Mwandamizi Kamishna wa Polisi Mstaafu Saada Ibrahim Makungu.

Wengine ni Msaidizi Kamishna wa Polisi Mstaafu Marehemu Issa Haji Pandu, Luteni Kamanda Mstaafu Ali Yussuf Mohamed, Luteni Kamanda Mstaafu Shafi Mohamed Hanif, Kapteni Mstaafu Marehemu Hassan Juma Reli, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Mstaafu Sofia Hebber Masewa na Khatib Mwinyichande.

Rais Dk. Shein pia, amewatunuku  Profesa Ali Seif Ali Mshimba, Amour Abdalla Khamis, Said Salim Bakhresa, Ahmada Yahya Abdulwakil, Haji Mbarouk Ameir, Haji Nasibu Haji Nyanya, Khalid Ali Kombo, Khatib Haji Khalid, Hassan Juma Khamis, Simai Jafar Bai, Zaidu Juma Ussi, Salmin Juma Jecha, Haji Seti Haji.

Wengine waliotunukiwa Nishani hizo ni Lela Nassor Khamis, Songoro Omar Kirobo, Khadija Hassan Aboud, Fatuma Issa Juma, Daud Suleiman Ali, Marehemu Kheir Idd Milao, Marehemu Ahmada Ali Shamata, Marehemu Hassan Juma Hassan, Marehemu Khamis Haji Mpera, Marehemu Ame Vuaa Ame na Marehemu Abdi Ramadhan Shemhaji.

Rais Dk. Shein pia, ametoa Nishani ya Utumishi Uliotukuka kwa Watumishi wa Serikali, Mahkama na Baraza la Wawakilishi wakiwemo Maryam Abdallah Yussuf,  Zuleikha Kombo Khamis, Janeth Nora Sekihola, Saleh Ali Salim, Luteni Kamanda Subira Mohamed Hassan, Marehemu Juma Ali Juma, Marehemu Silima Mkindwi Khamis, Marehemu Abdallah Waziri Ramadhan, Marehemu Balozi Ali Othman Korosheni na Marehemu Abel Anthony De Silva.

Sambamba na hayo, Rais Dk. Shein ametunuku Nishani ya Ushujaa kwa Watumishi wa Idara Maalum za SMZ  akiwemo Luteni Kanali Mstaafu Ali Ussi Ali, Luteni Kanali Mstaafu Justice Issack Anthony, Meja Mstaafu Mohamed Hamza Yussuf, Kapteni Mstaafu Fatma Abdalla Mussa, Kapteni Mstaafu Juma Ali Jongo, Kapteni Mstaafu Ramadhan Mango Jilungui, Luteni Mstaafu Abdalla Hassan Rehani, Waranti Ofisa Mteule Daraja la I Mstaafu Kona Haji Juma, Ofisa Mteule Daraja la 2 Mstaafu Othman Bakari Kwae.

Wengine ni Ofisa Mteule Daraja la 2 Mstaafu Abdallah Ali Abdallah, Sajin Taji Mstaafu Suleiman Mgeni Suleiman, Sajin Taji Mstaafu Rehani Uled Khamis, Sajin Mstaafu Iddi Khamis Omar, Sajin Mstaafu Ali Khatib Ali, Koplo Mstaafu Ali Haji Issa, Sea 1. Ali Mossi Haji na Hija Hassan Hija.

Pamoja na hao, Rais Dk. Shein pia, alimtunuku Koplo Marehemu Said Abdulrahman Juma, Private Marehemu Sharif Salim Suleiman, Police Constable Marehemu Haji Muslim Simai, Mrehemu Bakari Juma Hussein, Marehemu Ali Juma Ame, Marehemu Hafidh Silima Kona, Marehemu Issa Daud Omar na Marehemu Mohamed Abdallah Mohamed.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.