Habari za Punde

Mahafali ya NNe ya skuli ya Sunni Madressa Mkunazini

Na Khadija Khamis –Maelezo  Zanzibar 
Wahitimu wa kidatu cha nne wametakiwa  wasitosheke na ufaulu waliupata waongeze bidii katika masomo yao wanayoendelea  ili kufikia malengo yao ya baadae .
hayo aliyasema Dkt.Abdalla Ismail Kanduru katika Mahafali ya Skuli ya Sunni Madressa Mkunazini  wakati akikabidhi vyeti kwa wahitimu waliomaliza masomo yao ya kidatu cha nne .
Amesema licha ya matokeo mazuri yaliyopatikana  wanafunzi wazidishe juhudi katika masomo yao yan kidatu cha tano  kwa mustakbali ya maisha yao ya baadae.
Amesema wanafunzi wengi hivi sasa wanashawishika kuingia vyuoni na kukataa kusoma kidatu cha tano na sita jambo ambalo sio sahihi kwani kila siku sifa zinabadilika za kuingia Chuo Kikuu .
“Kila siku mambo yanabadilika nashauri yule alifanikiwa kuingia  kitatu cha tano aendelee waache kukimbilia kwenye vyuo jambo ambalo sio njia sahihi ya uwamuzi”.alisema Dkt Kanduru .
Alifahamisha kuwa wanafunzi walihitimu masomo yao  wasijibweteke hata kama wazee wao watakuwa na uwezo lazima wazidishe juhudi za kujitafutia maendeleo yao wenyewe katika maisha yao ya baadae.
Aidha aliwataka walimu na walezi kuzidisha mashirikiano katika usimamizi wa wanafunzi wao kwa lengo la kuongeza juhudi za ufundishaji na kuimarisha ongezeko la ufaulu wa wanafunzi  hao
Nae Mwakilishi wa Rais wa Jamat Murtaza Turk alisema juhudi za walimu na walezi wa wanafunzi pamoja na wajumbe wa bodi ya skuli hiyo  zimeweza kusaidia ufaulu mzuri wa skuli hiyo .
Alifahamisha kwamba katika wanafunzi 70 wa kidatu cha nne waliofanya mitihani yao, wanafunzi 10 wamepata devition 1 ,13 devition11 , 22 devition 111 na 25 ni devition 1V wameweza kufuta sero  kwa mwaka huu jambo ambalo ni faraja .
Aidha alisema kipindi cha mwaka jana kulikuwa na changamoto kubwa kwa wanafunzi kutofauli vizuri jambo ambalo lilichafua sifa nzuri  ya skuli hiyo .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.