Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe.
William Tate Ole Nasha akizungumza na
waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu mashindano ya Kitaifa ya
Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) mwaka 2020 yatakayofanyika kati ya Machi 16 hadi 20
mwaka huu Jijini Dodoma .
Mkurugenzi mkuu wa
Idara ya wateja wakubwa Benki ya CRDB Bw. Prosper Nambaya akisisitiza kuhusu
Benki hiyo kuendelea kushirikiana na Wizara ya Elimu , Sayansi na Teknolojia
katikamashindano
ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) mwaka 2020 yatakayofanyika kati ya Machi 16 hadi 20
mwaka huuJijini Dodoma .
(Picha
zote na MAELEZO)
Na
Mwandishi wetu- Dodoma Mashindano ya Kitaifa
ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) mwaka 2020 kufanyika kati ya Machi 16 hadi 20 mwaka huu
.
Akizungumza leo
Februari 5, 2020, Jijini Dodoma, Naibu
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. William Tate Ole Nasha amesema kuwa
lengo la MAKISATU ni kuibua, kutambua , kuendeleza Ubunifu na Ugunduzi
unaofanywa na Watanzania ili kuchochea maendeleo katika sekta mbalimbali.
“Mashindano haya
yanatoa fursa kwa wabunifu na wagunduzi wa teknolojia mbalimbali kujitangaza na
kutangaza bunifu zilizozalishwa ambapo
kaulimbiu ya mwaka huu ni ” Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwa Uchumi wa
Viwanda”. alisisitiza Mhe Ole Nasha
Akizungumzia walengwa
wa mashindano hayo Ole Nasha amesema kuwa ni Shule za Msingi; Shule za
Sekondari; Vyuo vya Ufundi Stadi; Vyuo vya Ufundi wa Kati; Vyuo Vikuu, Taasisi
za Utafiti na Maendeleo pamoja na mfumo usio rasmi.
Akifafanua amesema
kuwa Serikali inatambua umuhimu wa mchango wa wabunifu na teknolojia katika
kurahisisha na kuongeza ufanisi kwenye utekelezaji wa shughuli mbalimbali za
kiuchumi na kijamii na uzalishaji kupitia viwanda.
Akizungumzia
mafanikio ya uendelezaji Sayansi na Teknolojia Mhe. Ole Nasha amesema kuwa hadi sasa Serikali imeweza kusimamia
uanzishwaji wa vituo atamizi vipya 17 kwa ajili ya kukuza na kuendeleza ubunifu
na hivyo kuanzishwa kwa makampuni mapya
94 yanayotokana na ubunifu na kuzalisha ajira za moja kwa moja kwa vijana
takribani 600 na ajira zisiszo za moja kwa moja zaidi ya vijana elfu kumi na tano.
Mafanikio mengine ni
pamoja na Serikali kuibua na kutambua wabunifu wachanga zaidi ya 415 na kati ya
hao wabunifu 60 mahiri wanaendelezwa ili ubunifu wao uweze kufikia hatua ya kubiasharishwa.
Aidha, Usajili wa
washiriki wa Mashindano haya ulianza tangu tarehe 2 Januari, 2020 na
unaratibiwa na Wizara ya Elimu , Sayansi na Teknolojia ikishirikiana na Taasisi
zake ambazo ni ; Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia ambayo inasajili wabunifu
wa makundi ya Vyuo Vikuu na Taasisi za Utafiti na Maendeleo.
Taasisi nyingine ni
pamoja na; Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) inayosajili
wabunifu wa makundi ya Vyuo vya Ufundi Stadi na Mfumo usio Rasmi; Baraza la
Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linalosajili wabunifu wa kundi la Vyuo vya
Ufundi wa Kati.
Mhe. Ole Nasha
aliishukuru Benki ya CRDB kwa utayari wao wa kushirikiana na Wizara hiyo katika
kukuza na kuimarisha ubunifu na teknolojia nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi
mkuu wa Idara ya wateja wakubwa Benki ya CRDB Bw. Prosper Nambaya
amesisitiza kuwa Benki hiyo itaendelea kushirikiana na Wizara
ya Elimu , Sayansi na Teknolojia katika mashindano ya Kitaifa ya Sayansi,
Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) mwaka 2020
yatakayofanyika kati ya Machi 16 hadi 20 mwaka huu Jijini Dodoma .
Mwongozo na Fomu za
maombi ya kushiriki zinapatikana katika tovuti za Wizara na Taasisi zake. sUsajili
unafanyika pia kupitia tovuti ya MAKISATU, http//makisatu.costech.or.tz.
No comments:
Post a Comment