Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiongoza mkutano wa Uongozi wa Wizara ya Biashara na Viwanda Zanzibar kuwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango Kazi kwa mwezi wa Julai hadi Disemba 2019 /2020, uliofanyika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar, uliofanyika 17-2-2020.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali
Mohamed Shein amesema Serikali ya Mapinduzi awamu ya saba itakamilisha ujenzi
wa kiwanda cha Mwani kisiwani Pemba kama ilivyowaahdi wananchi wake.
Alieleza kuwa pamoja na bei ya zao la karafuu kupanda na
kushuka katiuka soko la Dunia, Serikali itaendelea kusimamia ahadi yake na
kuwalipa wakulima kiwango kile kile cha bei (asilimai 80 ya bei ya soko la
Dunia) .
Alisema Wizara ya Viwanda na Biashara inachangia ipasavyo
maendeleo ya utalii hapa nchini.
Aidha, ameutaka uongozi
wa Wizara hiyo kupitia vitengo vyake vya elimu kujikita katika suala la utoaji
wa elimu ili kuwaelimisha
wafanyabiashara juu ya sheria mbali mbali zilizopo badala ya kusubiri wakosee
na kuwachukulia hatua.
Dk. Shein ametoa pongezi kwa Uongozi na watendaji wa Wizara
hii kwa kuandaa vyema taarifa ya mpango kazi na utekelezaji mzuri wa majukumu
yao na hivyo kuwa na mchango mkubwa katika uchumi na maendeleo ya Taifa.
Nae, Waziri wa Biashara na Viwanda Amina Salum Ali,
akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi kwa Wizara hiyo kwa kipindi
cha Julai – Disemba 2019, alisema katika
kipindi hicho Wizara ilikadiria kununua jumla ya tani 3,500 za Karafuu , lakini
hadi kufikia Disemba 2019 ilifanikiwa kununua jumla ya tani 1,638.5 zenye
thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 20.3, na kuainisha kuwa kiwango kikubwa
cha karafuu hizo ziliuzwa katika nchi za India na Singapore.
Alisema shirika la Biashara la Taifa (ZSTC) limeanzisha
maandalizi ya uanzishaji wa Kiwanda cha kuchakata Mwani katika eneo la Viwanda
Chamanangwe, huku taaluma ya kilimo
hicho ikitolewa kwa baadhi ya wakulima wa maeneo ya Makangale, Tumbe na
Chokocho kwa upande wa Pemba, wakati kwa upande wa kisiwa cha Unguja ni Bweleo,
Pwani mchangani na Muungoni.
Aidha, alisema Wizara imefanya utafiti mdogo wa kuangalia soko
la Uyoga hapa nchini, ambapo matokeo ya utafiti huo yakionyesha zaidi ya
asilimia 90 (hoteli zipatazo 65) zinatumia Uyoga kama chakula cha wageni wao.
Alisema kwa asilimia 70 Hoteli hizo hutumia Uyoga huo kutoka
nje ya nchi (canned), wakati baadhi ya Hoteli huagiza kutoka Mikoa ya Iringa na
Arusha.
Vile vile alisema Wizara imefanikiwa kuwalipa fidia wananchi 106 wanaotoka vijiji vya Kiuyu na
Mchangamdogo waliokuwa wakimiliki mashamba madogo na makubwa katika eneo la
Viwanda Chamanangwe, wakati wale waliobaki wakitakiwa kusubiri uhakiki wa
majina yao.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail: abdya062@gmail.com.
No comments:
Post a Comment