Habari za Punde

Wafundisheni Ueledi Wapelelezi-Masauni

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(kulia),akiangalia moja ya darasa linalotumika kufundishia wanafunzi katika Shule ya Polisi Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo chuoni lengo kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma zinazotolewa na Jeshi la Polisi,wapili kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Salum Hamduni.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni akikagua dawati katika  moja ya darasa linalotumika kufundishia wanafunzi katika Shule ya Polisi Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo chuoni lengo kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma zinazotolewa na Jeshi la Polisi,wapili kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Salum Hamduni.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Salum Hamduni(kulia) baada ya kukagua moja ya chumba vinavyotumika kutoa huduma ya malazi kwa   wanafunzi katika Shule ya Polisi Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo chuoni lengo kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma zinazotolewa na Jeshi la Polisi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Polisi baada ya kuwasili  katika Shule ya Polisi Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo chuoni lengo kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma zinazotolewa na Jeshi la Polisi
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Na Mwandishi Wetu
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni ameutaka uongozi wa Shule ya Polisi Tanzania kuwafundisha ueledi wapelelezi ili kuweza kupunguza msongamano wa mahabusu na kesi ambazo zinasababishwa na upelelezi usio na kiwango.
Masauni ameyasema hayo mkoani Kilimanjaro wakati wa ziara ya kutembelea Shule ya Polisi Tanzania lengo ikiwa kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma za Jeshi la Polisi.
“Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli alipokua akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria aligusia suala la wapelelezi kuwa chanzo cha mlundikano wa mahabusu katika magereza yetu na mimi hii leo nimetoka gereza la Arusha nimeongea na wafungwa na mahabusu nao wanalalamikia upelelezi wa kesi zao kupindishwa na mbaya zaidi wengine wamehukumiwa vifungo kwa ajili ya upelelezi usio makini.Ni tatizo kubwa haiwezekani Rais huyu alalamike kila siku sasa maagizo ya serikali kwa chuo hiki jitahidini kupika vizuri wapelelezi wenu vizuri,tumpumzishe Rais wetu ana mambo mengi,timizeni tu wajibu wenu”amesema Masauni
Akizungumza katika ziara hiyo Kaimu Kamandanti Kamishna Msaidizi Omar Khamis Omar amesema wamechukua maelekezo ya serikali na wanaahidi kuyafanyia kazi ili yaweze kuleta tija huku akitaja idadi ya wanafunzi waliopo shuleni hapo wakisomea fani mbalimbali.
“Shule yetu kwa sasa ina wanafunzi 856 kati yao wanaume 725 na wanawake ni 131 ambao wako katika mafunzo mbalimbali na wote wanaendelea vizuri na masomo” amesema Kamishna Msaidizi Omar
Katika ziara hiyo Naibu Waziri Masauni alipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya shule hiyo ikiwemo sehemu za kulala,madarasa,uwanja wa paredi,vyumba vya komputa na ukarabati bwalo la chakula.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.