Na
Mbaraka Kambona,
Mwenyekiti
wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) amesema uamuzi wa
Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli wa kuwasamehe wafungwa 3973 ni hatua
muhimu katika kudhibiti kusambaa kwa maambukizi
ya maradhi yanayosababishwa na
Virusi vya Korona.
Jaji
Mwaimu aliyasema hayo leo Mei 7, 2020 Ofisini kwake jijini Dodoma alipokuwa
akitoa mtazamo wake juu ya jitihada za Serikali za kudhibiti kuenea kwa maradhi
hatari ya Korona.
Alieleza kuwa
msamaha huo ni muhimu hasa katika nyakati hizi ambapo Tanzania na nchi nyingine
Dunia zipo katika kupambana na vita kubwa ya mlipuko wa maradhi
yanayosababishwa na virusi vya Korona.
Jaji
Mwaimu aliendelea kusema kuwa msamaha huo utasaidia sana kupunguza msongamano kwa wafungwa na mahabusu unaoweza
kuhatarisha afya zao.
“Kimsingi
msamaha huu wa Rais utasaidia kulinda
haki ya afya kwa wananchi. Sisi Tume tunaona uamuzi huu wa Rais Magufuli umebebwa na nia njema ya kutaka kuwalinda
wananchi anaowaongoza”, alisema Jaji Mwaimu
Aliendelea
kusema kuwa Serikali inaweza kuendelea
kupunguza misongamano kwa kutumia
mifumo mbalimbali ya Sheria iliyopo kwa kutoa adhabu mbadala ikiwemo matumizi ya Sheria
ya Parole ambayo inaruhusu vifungo vya nje kwa wale wafungwa wenye tabia njema.
Katika
hatua nyingine, Jaji Mwaimu aliwashauri baadhi ya askari Polisi ambao wamekuwa wanalalamikiwa kuwa na tabia ya
kubambikiza kesi wananchi kuacha kufanya hivyo kwani ni moja ya chanzo cha
misongamano isiyo ya lazima magerezani.
Aidha,
Jaji Mwaimu alimpongeza Mkurugenzi wa Mashtaka kwa ziara zake za hivi karibuni
magerezani ambapo lengo lake ni kupunguza misongamano magerezani kwa kufuta
kesi za Mahabusu baada ya kuona baadhi yao kesi zao hazina msingi wala ushahidi wa kutosha.
Hata
hivyo alimuomba DPP aendelee na jitihada hizo ili kupunguza misongamano magerezani.
Pia
Mwenyekiti anaona kuwa Mahakama ina mchango katika kupunguza misongamano
magerezani kwa kutoa dhamana kwa makosa
yanayodhaminika kwa masharti nafuu.
Vile
vile alisema kuwa ameliomba Jeshi la Polisi kwa mamlaka iliyonayo kutoa dhamana
kwa watuhumiwa waliopo katika vituo vyao ambao wana makosa madogomadogo ambayo
yanaweza kudhaminika ili kupunguza misongamano katika mahabusu zao.
Aprili
26, 2020 kwenye Maadhimisho ya miaka 56 ya Muungano, Mheshimiwa Rais, Dkt. John
Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa 3,973 ambapo kati ya hao 256 walikuwa
wanakabiliwa na adhabu ya kunyongwa na wamebadilishiwa adhabu hiyo.
No comments:
Post a Comment