Habari za Punde

Rais Dkt Magufuli ashiriki misa ya kumuaga Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Mzee Benjamin William Mkapa

 Gari la Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ likiwa limebeba Jeneza lenye mwili wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa wakati likiwasili katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.


 Makanali wa JWTZ wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa wakati wakiingia katika sehemu ya Ibada katika Misa ya Dominika ya 17 ya Mwaka ‘A’ wa Kanisa Katoliki pamoja na Kumuaga Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mjane wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Mzee Benjamin William Mkapa Mama Anna Mkapa akiwa pamoja na familia yake katika Misa hiyo iliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwa pamoja na viongozi wengine wa Kitaifa wakishiriki Misa ya Dominika ya 17 ya Mwaka ‘A’ wa Kanisa Katoliki pamoja na Kumuaga Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.