Na.
Immaculate Makilika- MAELEZO
Benki ya Dunia imeitaja Tanzania kuwa miongoni mwa
nchi 50 duniani za uchumi wa kipato cha kati, ikiwa ni ya pili baada ya Kenya katika
nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, baada ya ukuaji wa uchumi unaosukuma
pato la mwananchi kukua (Per capita GNI) mwaka 2020.
Tanzania imeingia kwenye uchumi wa kati miaka mitano kabla ya lengo la Dira ya Taifa
ya Maendeleo ya 2025, jambo ambalo ni la kujivunia.
Akizungumza
katika Mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan
Abbasi alisema kwa mujibu wa Dira ya Taifa ya
Maendeleo, 2025 katika ukurasa wa pili, kipengele 1.2 “Uchumi
wa kipato cha kati umehusishwa na kuwa na nchi ambayo umaskini unapungua,
uchumi imara unaojengwa na kuimarika kwa uzalishaji viwandani unaimarika na
wananchi wanapata maendeleo”.
Dkt.
Abbasi alisisitiza kuwa uchumi wa
kipato cha kati umegawanyika katika madaraja mawili daraja la chini ambapo ni
kuanzia dola za Kimarekani 1036 hadi 4045 na daraja la juu ni dola 4046 hadi 12,535 na mwaka huu Tanzania
imepanda daraja kuwa uchumi wa kipato cha kati daraja la chini, pamoja na nchi
za Algeria na Benin.
Aidha,
Dkt. Abbasi alifafanua siri 10 zilizoisaidia Tanzania kutajwa kufikia daraja la
uchumi wa kipato cha kati na Benki ya
Dunia hapo Julai 1, 2020 kuwa ni nchi yenye amani na utulivu, na hivyo ni msingi muhimu nyuma ya mafanikio ya nchi ya Tanzania kuingia katika uchumi wa kipato cha kati
kwani bila amani hakuna kufanyakazi,
hakuna kuzalisha na hakuna kuongeza kipato.
Na hivyo viongozi, wanahabari na wananchi kwa ujumla wamesisitizwa
kuwekeza akili zao katika kuimarisha amani iliyopo na kukataa chokochoko
zozote zile zinazoweza kuharibu misingi ya maendeleo.
Siri ya pili
ni mipango thabiti ya maendeleo, ambapo Dkt. Abbasi alisema kuwa moja
ya kanuni muhimu ya kuendelea ni kuwa na mipango inayokuwekea malengo
makubwa (Olympic targets). Serikali itaendelea kuweka mipango mbalimbali ya
maendeleo ya muda mrefu na mfupi, akitolea mfano mwaka 2020 Serikali ilianza
kutekeleza Dira ya Taifa ya
Maendeleo ya 2025 ambayo moja ya malengo ni kufikia
uchumi wa kati.
Kwa
mujibu wa Dkt. Abbasi siri ya tatu ni utekelezaji
usioyumba, katika miaka 59 ya Uhuru na mitano ya
Awamu ya Tano Serikali imejitahidi kusimamia eneo hilo kwa kuhakikisha mipango inayowekwa inatekelezwa
kwa kina (3feet implementation).
Siri
nyingine ni maamuzi magumu, “Moja
ya mafanikio ya Serikali ya Tanzania kwa Awamu zote na sasa tumeimarisha katika
Awamu ya Tano ni wakati fulani Serikali kufanya uamuzi mgumu ambao wakati
fulani ulionekana kuwa ni ndoto lakini baadaye ukaleta mafanikio makubwa kwa
jamii, tumepambana na wala rushwa na wahujumu uchumi, tumewekeza katika
miundombinu mikubwa, tumekataa pia baadhi ya nadharia za kimagharibi kwenye
utendaji wetu na utungaji wetu wa sera za maendeleo” alisema Dkt. Abbasi.
Aidha,
Dkt. Abbasi alitaja siri nyingine kuwa ni azma ya
kujitegemea, nidhamu katika matumizi, kutekeleza miiko ya uongozi, kuwekeza kwenye miradi
inayochechemsha uchumi, maendeleo
ya vitu na sekta binafsi yenye tija.
No comments:
Post a Comment