Habari za Punde

WIZARA YA AFYA YAPOKEA MSAADA WA PIKPIKI KUTOKA (IOM)

Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wahamaji (IOM) Dkt. Qasim Sufi akimkabidhi Pikipiki  Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Halima Maulid Salum katika hafla iliyofanyika  Wizara ya Afya Mnazimmoja  .
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Halima Maulid Salum akitilIana saini na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wahamaji (IOM) Dkt.Qasim Sufi wakati wa   makibidhiano ya msaada wa pikipiki hafla iliyofanyika  Wizara ya Afya Mnazimmoja  .
Baadhi ya Maafisa wa Wizara ya afya wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kupokea msaada wa pikipiki kutoka Shirika  la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wahamaji  (IOM) hafla iliyofanyika  Wizara ya Afya Mnazimmoja  .
PICHA NA FAUZIA MUSSA/ MAELEZO

Na.Issa Mzee, Maelezo  09/07/2020
Wizara ya  afya imepokea msaada wa pikipiki mbili zenye thamani ya dola 2727 kutoka shirika la Umoja wa Wataifa la kuhudumia Wahamaji (IOM) kwa lengo la  kuwasaidia wafanyakazi kufuatilia maradhi ya Corona.
Akikabidhi msaada huo Mkuu wa Shirika la Wahamaji Tanzania Dkt. Qasim Sufi huko Wizara ya Afya Mnazimmoja, amesema lengo la msaada huo ni kuiwezesha na kuirahisishia serikali ya Zanzibar katika jitihada za kupamabana na maradhi hayo.
Aidha amesema shirika hilo litazidi kutoa ushirikiano katika sekta ya afya ili kupambana na maradhi mbalimbali ikiwemo  ya kuambukiza .
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Halima Maulid Salum amesema pikipiki hizo zitawawezesha  kufutilia mwenendo mzima wa maradhi .
Alisisitiza kwamba zitawasaidia katika kufanya tafiti za maradhi mbalimbali  hasa maeneo ya ndani ambayo ni vigumu kufikika kwa kutumia usafiri wa gari  .
“baadhi ya sehemu hasa vijijini inakua usumbufu kufika kwa gari, hivyo  msaada huu utatusaidia kwa kiasi kikubwa ” alisema Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya
Nae Mkurugenzi  kinga Dk Fadhil  Mohamed amelishukuru  shirika hilo kwa  msaada huo na kuwataka wafanyakazi  kuzitumia vizuri pikiki hizo ili kufikia malengo.
Amewataka watendaji  waliokabidhiwa pikipiki hizo kuzitumia ipasavyo na kuzitunza ili ziweze kudumu

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.