Zanzibar, Agosti 13, 2020. Wateja waZantel wataweza kununua tiketi za usafiri wa boti za
Azam kwa njia ya Ezypesa baada ya kampuni hiyo kuingia ubia na Kampuni ya
usafirishaji ya Kilimanjaro Fast Ferries Ltd inayotoa huduma za usafiri wa
boti.
Kampuni
hiyo ni moja ya watoa huduma za usafiri wa majini kati ya Zanzibar na Dar es
Salaam ikiwa na boti nne zinazochangia katika urahisishaji wa huduma za usafiri
kwa wenyeji na wageni.
Akizungumzia hatua hiyo, Mkuu wa Masoko na
Huduma za Kifedha wa Zantel, Sakyi Opoku alisema hatua hiyo imelenga kurahisisha
upatikanaji wa huduma za ukataji tiketi kwa abiria hivyo kuboreshamaisha ya
wateja wao.
“Kwa
kupitia Ezypesa tunahakikaisha wateja wanafanya malipo yao kwa urahisi zaidi,mahali
popote na wakati wowote.Ushirikiano wetu na Kilimanjaro Fast Ferries unawapa
wateja uhuru wa kununua tiketi na kupunguza muda na mchakato wa kununua
tiketi,” alisema Opoku.
Ili kupata huduma hiyo, mteja wa Zantel,
atapiga namba ya Azam bure 0800 785 555 na atapewa namba ya kumbukumbu ya
malipo.Kisha ataenda kwenye menyu ya Ezypesa *150*02#na kuendelea na
malipo, kisha ingiza namba ya Kampuni777444 kisha kumbukumbu namba,kiasi na mwisho thibitisha malipo.
“Tunaamini njia hii ni suluhisho na itaboresha namna
wateja wanavyopata huduma za usafiri hususan wasafiri wa ndani kwani kwa sasa
hakuna haja ya kwenda tena katika ofisi bali ukiwa na simu yako tu unaweza
kujihakikishai uhakika wa kupata usafiri,” alisema Opoku.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Marine
Ltd, Abubakar Salim alisema kampuni hiyo imewekeza katika mifumo ya malipo
mtandaoni ambayo inatumika duniani kote, ambayo imesaidia kuboresha upatikanaji
wa huduma za usafiri.
“Ushirikiano baina yetu na Ezypesa
umetanua wigo wa njia za malipo ambazo zinampa mteja uhuru wa kununua tiketi
mahali popote alipo, wakati wowote bila malipo ya ziada,” alisema Salim.
Wateja watakaofanya malipo kwa Ezypesa
watachukua tiketi zao katika ofisi za Azam Marine siku ya kusafiri ambapo
watatakiwa kuonyesha ujumbe (SMS) ya uthibitisho wa malipo.
Zantel ni Kampuni
inyaoongoza kwa utoaji wa huduma za mawasiliano Visiwani Zanzibar kwa miaka
mingi hivi sasa ikiongoza kwa ubora miundombinu ya mawasiliano, huduma pamoja
na bidhaa.
Huduma ya kifedha ya
Ezypesa ni ya kwanza nchini Tanzania kutoa huduma za kibenki za kawaida pamoja
na za kiislamu kwa ushirikiano na benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ).
Aidha, Zantel ni kampuni
inayoongoza kwa utoaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania kupitia uwekezaji kwenye
teknolojia ya fibre optic cable ambayo inaiunganisha Tanzania na nchi nyingine
za Afrika Mashariki na duniani umeiwezesha Kampuni hiyo kuleta mapinduzi ya
haraka ya kidigitali hapa nchini.
Aidha,Miundombinu
hiyo imeiwezesha Zantel kutoa huduma za
kimataifa za sauti na data kwa jumla kwa kampuni nyingine na nchi jirani hivyo
kuchagiza ukuaji wa teknolojia ya digitali.
No comments:
Post a Comment